CCM iko hoi kiuchumi!

CCM iko hoi kiuchumi!

tpmazembe

JF-Expert Member
Joined
Jan 5, 2012
Posts
2,469
Reaction score
588
Chama Cha Mapinduzi (CCM) kilivyokuwa hoi kiuchumi. Ni vema ikafahamika chama kinachokabiliwa na mchoko wa uchumi, hakiwezi kufanya siasa.

Katika vielelezo hivyo nilivyopewa na msiri wangu hapa Lumumba, CCM kinaonekana kinakabiliwa na mzigo wa madeni; taasisi mbalimbali za umma, mabenki na watu binafsi zinakidai chama hiki mabilioni ya fedha.

Wakati chama kikidaiwa fedha zote hizo, Akaunti zake zimekauka. Fedha zimetafunwa kama mchwa. Anayeonekana kuwa ndiye mtia saini mkuu wa fedha za chama, ni Mwigulu Nchemba, anayejiita Mchumi Na. 1. Tufuatilie kwa pamoja.

Itaendelea kila tutakapofanikiwa kupata nyaraka nyingine.


Akaunti ya Katibu Mkuu CCM CRDB Azikiwe A/C No. 01J1028138800.

Watia Saini

Mhe. Wilson C. Mukama - aliyekuwa Katibu Mkuu wa CCM
Mhe. Mwigulu L. Nchemba (Mb) - aliyekuwa Katibu wa NEC - UF Ndg. Judith F. Tumbao - Mhasibu Mkuu

Salio la fedha kwa tarehe 16/11/2012 ni Shs. 5,816,806.49

Akaunti ya No. 01J1005069302. Salio la fedha tarehe 16/11/2012 ni Shs. NIL.

Watia Saini

Mhe. Wilson C. Mukama - aliyekuwa Katibu Mkuu wa CCM
Mhe. Mwigulu L. Nchemba (Mb) - aliyekuwa Katibu wa NEC – UF Ndg. Judith F. Tumbao - Mhasibu Mkuu

Akaunti ya Mkuu wa Utawala CCM Makao Makuu Dodoma - ipo CRDB Tawi la Dodoma A/C No. 01J1081476900.

Salio la fedha kwa tarehe 16/11/2012 ni Shs. 113,167.54

Watia saini

Mhe. Mwigulu L. Nchemba (Mb) - aliyekuwa Katibu wa NEC - UF Mhe. J.Z. Chiligati (Mb) - aliyekuwa Katibu Mwenezi.


Chama Cha Mapinduzi, kimebeba mzigo wa madeni. Msiri wangu hapa Lumumba amenidokeza kuwa chama kinadaiwa hadi na vyombo vya habari.

Kimeshindwa kuwasilisha makato ya wafanyakazi wake; madeni kutoka taasisi za fedha yamelundikana hadi kufikia zaidi ya Sh. 1.3, huku nikielezwa kuwa Akaunti zake zimefilisika. Mabilioni haya ya fedha yametafanwa na wakubwa wakiongozwa na Mwigulu Nchemba.

Soma kiambatanisho hiki hapa chini kilichotoka kwa Mwigulu Nchemba kwenda kwa Zakia Meghi. Ni wakati Nchemba alipokuwa akikabidhi madaraka ya Katibu wa Uchumi na Fedha kwa Zakia Meghji.


MAKABIDHIANO YA IDARA YA UCHUMI NA FEDHA
KATI YA MHE. MWIGULU L. NCHEMBA (MB)(MNEC)
NA MHE. ZAKIA H. MEGHJI (MB) KATIBU
WA HALMASHAURI KUU YA TAIFA
WA UCHUMI NA FEDHA


2. IDARA YA UCHUMI NA FEDHA
Halmashauri Kuu ya Taifa iliyokutana mjini Dar es Salaam tarehe 27 - 29 Januari, 2004 pamoja na mambo mengine ilipitisha muundo mpya wa Idara ya Uchumi na Fedha. Awali Idara hii ilijulikana kama Idara ya Fedha na Mali za Chama. Badiliko hili la muundo linazingatia mambo yafuatayo:-
.
(a) Kwa mujibu wa Mwelekeo wa Sera za CCM katika miaka ya 2010 - 2020 na Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya mwaka 2010 Chama kinatakiwa kusimamia kwa nguvu mpya Sera zake za Uchumi hususan modenaizesheni ya Uchumi na uwezeshaji wa wananchi kiuchumi.

(b) Aidha suala la Vitega Uchumi na Uwekezaji katika Chama linatakiwa kupewa umuhimu na msukumo mkubwa ili kukiimarisha Chama kimapato na hatimaye kiweze kujitegemea.

HESABU ZA CHAMA NA KAMATI YA KUHAKIKI MALI ZA CHAMA

(a) HESABU ZA CHAMA
Hesabu za Chama zimekaguliwa na wakaguzi wa nje TAC-Associates kwa mwaka wa Fedha 2009/2010 na 2010/2011. Hesabu hizo zimeshawasilishwa kwa Mwenyekiti kwa ajili ya kuwekwa saini na baadaye kuwasilishwa kwa Msajili wa Vyama vya Siasa na Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali. Zoezi la kuziwasilisha kwenye vikao vya Chama litafuata baadaye. Kwa mujibu wa hesabu hizo, Chama kina mali zenye thamani ya Shs. 49.2bn/= hadi tarehe 30.06.2011. Thamani ya mali inashuka kila mwaka kutokana na Chama kutofanya uthamini wa mali zake. Mara ya mwisho uthamini ulifanyika mwaka 1992. Kwa hiyo Wakaguzi wameshauri kuwa Chama kifanye upya zoezi la uthamini. Kutokana na ukubwa na upana wa kazi hii, zoezi hili linahitaji wataalam wengi, kwa sababu hiyo Chama huwa kinawatumia Chuo cha Ardhi kwa kuwa wao wanawatumia wanafunzi wao katika kuifanya kazi hii na hivyo kuharakisha zoezi hilo.

(b) KAMATI YA KUHAKIKI MALI ZA CHAMA
Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Taifa iliyokutana Aprili, 2007 mjini Dar es Salaam iliunda Kamati ya Wataalam kwa ajili ya uhakiki mali za Chama. Majina ya Wataalam hao ni:-

(1) Ndg. Peter Machunde - Fedha na Vitega Uchumi
(2) Ndg. George Fumbuka - Fedha na Vitega Uchumi
(3) Ndg. Sam Mapande - Mwanasheria
(4) Ndg. Kanyoni Salum Kanyoni - Mhandisi
(5) Ndg. Jacquiline Noni - Mfanyabiashara
(6) Ndg. Simon Mapolu - Mchumi
(7) Ndg. Janeth Mbene - Mchumi
(8) Ndg. Ussi Faki - Mkaguzi
Katibu wa Kamati hiyo alikuwa Ndugu L.L. Burugi - Meneja Miliki wa Chama.


Kamati ilianza kazi tarehe 19/6/2007 na kukamilisha tarehe 28/10/2007. Kazi ya Kamati hii ililenga mali za Kudumu za Chama zilizopo Makao Makuu, Mikoani na katika Wilaya zilizopo kwenye Makao Makuu ya Mikoa. Aidha, zoezi hili lilihusisha pia mali za Jumuiya za Chama katika maeneo hayo pamoja na kufanya tathmini ya mwenendo wa Makampuni ya Chama.

12. BAADHI YA MADENI AMBAYO CHAMA KINADAIWA
(1) MADENI YA BENKI NA TAASISI ZA FEDHA
NBC Ltd. - 143,763,404.00
NSSF - 831,822,961.50
Ukaguzi wa Hesabu - 72,240,000.00
1,107,826,365.50

Deni la NBC ni la tangu mwaka 1994 kupitia Kampuni ya Chama TANTI kwa kuweka rehani nyumba 10 za CCM zilizoko Area ‘C’ - Dodoma.

Mkopo wa NSSF unahusu Jengo la CCM Shinyanga. NSSF walimalizia kujenga Jengo. Mazungumzo yalifanyika kati ya CCM/NSSF na kufikia makubaliano ya Chama kununua Jengo hilo kwa shs. 1,109,097,282/= kiasi cha 25% kimelipwa.

Deni la ukaguzi linatokana na ukaguzi wa hesabu za mwaka 2009/2010 na 2010/2011.


(2) MADENI YA VYOMBO VYA HABARI

1. Clouds Entertainment Media Group 13,080,000.00
2. Radio Tumaini 424,800.00
3. ITV 3,778,360.00
4. Sahara Media Group Ltd 44,244,000.00
5. Sports Dream Co. Ltd 810,000.00
6. KIUTA 9,430,350.00
7. Colour Print 22,619,792.00
8. Business Times Ltd (Majira) 4,988,945.00
9. Habari Corporation 6,850,000.00
10. Mwananchi Communication Ltd 9,620,000.00
11. TSN 8,271,160.00
12. Guardian Ltd 11,702,160.00
13. TBC 7,687,360.00
14. Uhuru Publication Ltd 55,049,040.00
15. WAPO Radio 1,000,000.00
16. Zanzibar Leo 4,500,000.00

17. Raia Mwema 1,129,000.00
18. FTV Production 1,980,000.00
Jumla Tshs. 201,866,807.00
 
Yap..ndio maana Mwigulu amepelekwa Wizara ya Fedha ili afanye mipango ya kuchota fedha. Wafanyakazi wapo hatarini kukopwa mishahara yao!
 
Sasa kama ameshindwa kuinua uchumi wa chama chake, vipi kuhusu uchumi wa taifa? Nina wasiwasi.
 
Yaani huwezi amini akaunti ya chama tawala imebaki na salio kama AKAUNTI YA SHULE YA KATA! ndio maana wanashangaa chopa za CDM! kwa mtindo huo chama karibu kinawafia wapenda sifa.
 
eeh Mungu na ashindwe kutimiza hicho kilompeleka huko Hazina..tusije kula nyasi bure
 
huu bila shaka ni upotoshaji wa makusudi maana haujaweka ruzuku inayolipwa kila mwezi. CHADEMA pekee inakamata zaidi ya 200,000,000. Hivyo watakuwa wanakamata zaidi ya 1 billion
 
Mbona siwaoni wale misukule wa ccm kwenye hii thread? waje hapa watuambie kwanini chama chao tusikitokomeze 2015. Chama Cha Matapeli-Tanzania.
 
Na safari hii tutakaba hata penati, hatutaki EPA nyingine. Sana sana kwa ulimbukeni na pupa za Mwigulu pale ni yuko kwenye kitanzi, akilogwa ajaribu kutengeneza EPA nyingine ajue Keko/Karanga vinamsubiri.

By the way hii ripoti chanzo chake ni nini hasa?
 
Siyo siri nimeogopa hizi data zilivyopatikana kama ni credible. No wonder deni la taifa limeongezeka toka trilioni 10 mwaka 2005 hadi trilioni 27 leo 2014. Na Saada Mkuya anatetea hali hii. Kazi tunayo!
 
huu bila shaka ni upotoshaji wa makusudi maana haujaweka ruzuku inayolipwa kila mwezi. CHADEMA pekee inakamata zaidi ya 200,000,000. Hivyo watakuwa wanakamata zaidi ya 1 billion

Shule za kata zimeharibu vijana wa kitanzania, hata kutofautisha mapato na madeni inakuwa ngumu. Hatari sana hizi shule, taifa linaangamia.

Mwigulu ole wako uhamishie huu ukilaza wako kwenye kodi zetu, tutazaa na wewe.
 
Ndio maana mkulu Jk amempeleka nchemba huko Wizara ya fedha ajafanye epa mpya
 
Kwa style hii mtapamdishiwa kodi na vikodi kuibuka ibuka bila mpangilio
 
Kaka usiseme shule za kata zimeharibu watu mbona watu kama mm nimesoma shule hzo lakini naamini ni great thinker?ila huyo mtu kaamua kujivua akili tu kwa ushabiki wake uliomtia kipofu, wito tuziheshimu shule za kata ila tusiache kupambana ziboreshwe na kutoa elimu ilio bora zaidi
 
Siku chama hichi kitakapo kufa rasmi... nitafanya sherehe mwezi mzima.na ndio utakuwa ukombozi wa Tanganyika yenye neema
 
Back
Top Bottom