CCM ijibu hoja za CHADEMA - Sumaye

''Sumaye alisema CCM inahitaji viongozi waadilifu, wachapakazi, na wasio waoga kumshauri rais juu ya masuala mbalimbali ili kuuwa na mabadiliko ya kiutendaji yanayoendana na joto la kisiasa lililopo.''

Nimesoma hoja ya mheshimiwa SUMAYE,NAMHESHIMU SANA TENA SANA.NINACHOTAKA KUSEMA HAPA NI HOJA YA MSINGI KWAMBA SUMAYE NI MJUMBE WA HALMASHAURI KUU YA CCM AMABAYO KWA MUJIBU WA KATIBA YA CCM HALMASHAURI KUU NDIYO CHOMBA KIKUU CHENYE MAAMUZI JUU YA MUSTAKABALI WA KISIASA NA HATA UCHUMI KWENYE CHAMA TAWALA,ANAPOSEMA CCM WAJIBI HOJA YEYE ANAJITOA? ATWAMBIE KAMA YEYE NI CHADEMA AU CUF TUJUE MAPEMA. BILA SHAKA WATANZANIA WOTE WANAJUA KWAMABA UOZO WA MAADILI UMETOKEA KATIKA SERIKALI YA MKAPA NA SUMAYE ALIKUWA KIONGOZI MKUU WA SERIKALAI,NANI HAJUI MIKATABA YOTE MIBOVU ILIANZIA KWA SUMAYE NA MKAPA NA KWAMBA SERIKALI YA SASA INABEBA MAKOSA YAO?YEYE NA WENZAKE NDO WALIOINGIA MIKATABA YA KUUZA KILA KITU MPAKA NYUMBA ZA WATUMISHI NA LEO WANAISHI HOTEL ! UADILIFU WA SUMAYE UKO WAPI? ONDOA BORITI JICHONI KWAKO KABLA HUJAONA LA MWENZAKO.
hii hoja yako humu haitozingatiwa kabisa..weng wetu humu ni mashabiki zaid
 
Huyu Sumaye kukaa kimya akasahaulisha watu madudu yake leo anatoka kama vile yeye sio sehemu ya sisiemu? Hebu tuelezeni huyu bwana amesafishwa lini au kaoga maji ya uzima!
 
Anasema Isiiachie serikali peke yake...

Akizungumza na Mwananchi bila kujua kwamca CCM wangekuwa wanazungumzia suala hilo, Sumaye alisema, CCM inatakiwa kukabiliana kisiasa na hoja za
CHADEMA na si kuiacha serikali ipambane nao.

Kwa mujibu wa Sumaye, kazi ya siasa ni ya chama na si seikali, hivyo CCM wanapaswa kuwa msatari wa mbele kupambana na
CHADEMA kwa sera na kujibu hoja zao zote ili kuongeza imani ya wananchi kwa chama hicho.

"Wale CHADEMA wanafanya kazi ya siasa na hawa CCM wamekaa kimya, wanaiacha serikali ndio inatoa majibyu, hali hiyo si nzuri, chama kinapaswa kujibu hoja zote na kama hakina majibu, kiyaombe kwa serikali" alisema Sumaye.


Sumaye alisema CCM inahitaji viongozi waadilifu, wachapakazi, na wasio waoga kumshauri rais juu ya masuala mbalimbali ili kuuwa na mabadiliko ya kiutendaji yanayoendana na joto la kisiasa lililopo.


Source: Mwananchi

Maoni yangu:
Ni Kweli Wanahitaji kujibu hoja, So far si Kikwete, si Pinda, si Chiligati, Si Wassira alojibu hoja, wote waliishia kulalama tu na kuwatisha chadema, wanatakiwa kujibu hoja.

Lakini Jamaa naye anajiandaa nini 2015.

Huyu hana jipya! wala hana usafi wowote wa kukosoa CCM kwa sasa! alipokuwa Waziri Mkuu wa Mkapa mbona hakuishauri CCM ijibu hoja za CUF? badala alituma Jeshi la Wananchi na Polisi Zanzibar na kuuwa makumi ya Waandamanaji na wafuasi wa CUF mwaka 2001! pia hatujasahau kauli yake aliyotoa huko Moshi mwaka 2000 kuwa ukiweka Bendera ya CCM mbele ya duka lako basi patakuwa salama lakini ukiweka bendera ya upinzani mbele ya biashara yako basi ukipata tatizo usilaumu mtu!

Leo huyu Mzee Sumaye hana sura na sifa ya kuibeza CCM! tunamshauri anyamaze kimya na aendelee kula mafao yake na awaachie watu wenye sifa za kuikosoa CCM lakini siyo yeye au Lowasa!!

Hawa vigogo wa Kimasai bado uchungu wa kuukosa Urais na Uwaziri mkuu unawasumbua! hivyo sishangai leo wanajitokeza waziwazi kuikosoa CCM!!!!!
 
Dola acheni kuufumbia macho ukweli. Dola itaendelea tena kwa neema zaidi na watoto wenu watathaminiwa zaidi kuliko sasa hali ilivyo. Acheni CDM wafanye kazi ya kuwaadabisha hawa ambao wameshajizolea mali kwa wingi na wanashangaa wakiambiwa hali ni ngumu kwa maisha maana wao ni neema tu. Tuko pamoja sana Makamanda Wetu na kilio cha wengi ni kilio cha MUNGU. Chochote tu lazima kitokee kuwakomboa raia wa Tanzania waishi kwa neema iliyotapakaa kila kona lakini inaishia kwa viongozi wa ccm na watoto wao.
 
anasema isiiachie serikali peke yake...

akizungumza na mwananchi bila kujua kwamca ccm wangekuwa wanazungumzia suala hilo, sumaye alisema, ccm inatakiwa kukabiliana kisiasa na hoja za
chadema na si kuiacha serikali ipambane nao.

Kwa mujibu wa sumaye, kazi ya siasa ni ya chama na si seikali, hivyo ccm wanapaswa kuwa msatari wa mbele kupambana na
chadema kwa sera na kujibu hoja zao zote ili kuongeza imani ya wananchi kwa chama hicho.

"wale chadema wanafanya kazi ya siasa na hawa ccm wamekaa kimya, wanaiacha serikali ndio inatoa majibyu, hali hiyo si nzuri, chama kinapaswa kujibu hoja zote na kama hakina majibu, kiyaombe kwa serikali" alisema sumaye.


sumaye alisema ccm inahitaji viongozi waadilifu, wachapakazi, na wasio waoga kumshauri rais juu ya masuala mbalimbali ili kuuwa na mabadiliko ya kiutendaji yanayoendana na joto la kisiasa lililopo.


source: mwananchi

maoni yangu:
Ni kweli wanahitaji kujibu hoja, so far si kikwete, si pinda, si chiligati, si wassira alojibu hoja, wote waliishia kulalama tu na kuwatisha chadema, wanatakiwa kujibu hoja.

Lakini jamaa naye anajiandaa nini 2015.
bora yako we bwana sumaye kwani enzi yenu kuna vitu vingi mliifanyia nchi hii,lakini ushauri wangu wa bure hyu kijana msimuache peke yake mshaurini kwani nchi ishamshindwa,fanyeni hivyo kwa maslahi ya taifa na si kumuacha atupeleke pabaya
 
tatizo lao haya jamaa wa ccm hawana hoja za kujibu badala yake wanakimbilia vitisho, hawasomi alama za nyakati. huu si muda wa kutishana cha muhimu ni kuandaa hoja kama sumaye alivyosema, wakiona hawana kama ilivyo kawaida yao, maana ni unga hamnamo!!! waifuate serikali iwasaidie, vitisho haviwasaiidii sana. tofauti na hapo ni kuwa wanajiua wenyewe.
 
ccm is dead tunaongozwa na serikaki mfu! serikali inashindwa kukamata wezi wa ma bilioni eti inawapa siku warudishe pesa walizokwiba kweli huo ndo uadilifu kweli? no wonder hata shirika la ndege linatushinda kuendesha soon tutafanya arobaini ya ccm. chadema hoyeee!!!
Tulishaandika humu the thing (CCM) is dead!, watu hawaamini, dhambi ileile alofanya Ben na Truway ndo anaifanya JK, Makamba,Lowassa na Rostam kwa sababu wanajua mwishi wa siku watawapiga sound mtapoa, wamezoea ni tabia yao hawawezi kuacha ni sawa na kula nyama ya mtu, lazima wang'oke,watang'okaje? ndo swali la msingi sasa, kama ni damu likianza vuguvugu lakuwang,oa itamwagika vibaya! Badilisheni katiba, tume huru ya uchaguzi muwatoe 2015, je mnaweza kusubiri miaka 4, mana NJAA ZINAUMA SAAANA!
 
Sumaye kasema kweli... CCM wajibu hoja za CDM kuhusu hali mbaya ya maisha na siyo kusingizia uvunjifu wa amani. CCM ndio wanaovunja amani kwa kushindwa kuwahudumia waajiri wao(wananchi)
 
Sisiemu watamalizana wao kwa wao sisi yetu macho. Ukweli ni kwamba utendaji kazi wa jk haukukaliki hata ndani ya ccm.
 
Hivi kweli kuna tofauti kati ya Serikali+CCM+Vyombo vya Dola= Chama Dola. Kisha nani akashtaki wapi. Msituletee yale ya Swala kushtakiwa kwa kina Simba, Chui na Fisi!

Nimeisoma taarifa inayomnukuu Waziri Mkuu wa zamani, Mh. F. Sumaye ninaamini ni maelezo mazuri ambayo badala ya kwenda kuishtaki CHADEMA kwa CHAMA DOLA basi chama hicho kingeliichukulia maelezo hayo ambayo yako gazeti la Jumapili la Mwananchi kama document muhimu ya kufanyiwa kazi ili chama hicho kiweze kupata tena dira ya kinakwenda wapi baada ya kujua kimetoka wapi? Niulize jamani, hivi CCM ina Strategic Plan toka izaliwe? Kuuliza si kosa ninaamini ninaweza kukisaidia chama changu ambacho milango yote ya kuingia ndani ili na sisi tugombee uongozi imefungwa na walaji na wajuaji tele wanakichimbia chama kaburi bado kihai!
 
Hawana cha kujibu kutokana na usanii wa hali ya juu Serikalini na ndani ya CCM ndiyo maana wameona ni bora watoe tishio la kukifuta CHADEMA.
 
- Mh. Sumaye yuko sawa sawa, CCM tunatakiwa kujibu hoja za Chadema, badala ya kutafuta visingizio visivyo na kichwa wala miguu kama kuna ubovu urekebishwe now na sio kudanganyana, CCM tuliambiwa na Wapiganaji tukakataa kuwasiliza sasa tusilie yale yale ya wapiganaji yakitokea Chadema, wanasema akili za CCM nyingi huondoa maarifa! Modern smart politics zinataka hoja kujibiwa kwa hoja!

William @ NYC, USA.
 
Hii sinema ya mwaka 2015 ya Kushait wawili na Nilotic mmoja itakuwa ya millenia edition.....Nadhani spirit ya late Sokoine and Baba wa taifa ime revive...Mshindi atakuwa yule aliye wahi vazi la nabii Elija (Mweka mwenge wa uhuru kuleee Kilimanjaro...naona mmoja kesha pewa fimbo alipoenda kuomba baraka...) alipopalizwa na gari la moto maana huyo ndo atakuwa na anointing ya kukausha maji ya mto Yordan inayotaka kupeleka red sea taifa letu ili tuzame na tusitoke milele....Sijawahi kuwa nabii lakini leo natabiri kwenye hii set ndiyo universal set ya presidency where we would be able to get the president....Haya chini ya mstari kaa tayari gooooooooooooooooooooooooo!
 
Hii sinema ya mwaka 2015 ya Kushait wawili na Nilotic mmoja itakuwa ya millenia edition.....Nadhani spirit ya late Sokoine and Baba wa taifa ime revive...Mshindi atakuwa yule aliye wahi vazi la nabii Elija (Mweka mwenge wa uhuru kuleee Kilimanjaro...naona mmoja kesha pewa fimbo alipoenda kuomba baraka...) alipopalizwa na gari la moto maana huyo ndo atakuwa na anointing ya kukausha maji ya mto Yordan inayotaka kupeleka red sea taifa letu ili tuzame na tusitoke milele....Sijawahi kuwa nabii lakini leo natabiri kwenye hii set ndiyo universal set ya presidency where we would be able to get the president....Haya chini ya mstari kaa tayari gooooooooooooooooooooooooo!
Mkuu,
Umeongea kimafumbo zaidi, na inahitaji zaidi ya common-sense ku'decode message hii.
Embu jaribu kuileta kwa engo ingine ili akina yakhe waambue!
 
Kwani Hoja zenyewe zinazotakiwa Kujibiwa na CCM kwenye Majukwaa ni zipi basi? Kama ni Dowans Suala hilo liko Mahakamani, ni Makosa kulijadili nje yake kabla hukumu haijatoka, Kama ni Kupanda bei ya Umeme na Mgao Tanesco imeshatoa Maelezo, Kama ni Mabomu ya Mbagala Serikali imeshatoa Tamko na Tunasubiri matokeo ya Uchunguzi ili ijulikane Hatua za Kuchukua na Watakao wajibishwa (ingawa CDM wameshatoa Hukuma kabla hata Mabomu yenyewe hajamalizika Kulipuka!) Wakati wa Kampeni, kila Chama kiliwasilisha hoja zake kwa Wananchi, CDM kiliwasilisha hoja zake (Wenyewe wakiziita "MABOMU") kwa Wananchi, CCM ilizijibu kwa Nguvu zote katika ngazi zote, Aidha CCM ilionesha ilichokifanya katika kila Kijiji, Kata, Mkoa na Taifa ndani ya Miaka 5 iliyopita na Mapungufu yake na Kile ambacho CCM itafanya kwa Miaka 5 ijayo endapo itapewa Ridhaa na Wananchi kuongoza tena, Kule ilikofanya Makosa ilipoteza Wabunge na Madiwani, kule ilikofanya Vizuri ilishinda (Kama Ina Uwezo mkubwa wa Kuiba kura si Ingeiba kote) Matokeo ya Jumla CCM ilishinda Urais, Wabunge na Madiwani Wengi
sana. Kazi ya CCM hivi sasa ni Kuisimamia Vizuri Serkali yake itekeleze Yale yaliyoahidiwa Kipindi cha Kampeni (ilani yake ya Uchaguzi) imepewa Kikatiba Miaka 5 kuyatekeleza. Sasa cha Ajabu hata miezi mingapi Haijapita, tayari CDM Inapanda Majukwaani na Mabarabarani na kutaka hoja zilezile za Wakati wa Kampeni zijibiwe tena, Kwa hiyo CCM isifanye kazi zake na Kujipanga upya Bali na yenyewe iingie Barabarani na kuanza Malumbano na CDM kwa Sababu tu CDM inataka hivyo, kwani wao ni Nani? Ikumbukwe CDM kutoka na Hoja na Sera zake wakati wa Kampeni ilipata Walioikubali kwenye Urais wapatao 2.2millioni ambao ni Watu wengi na Wengi wao ndio hao Tunaowaona Kwenye Maandamano yao, Lakini jiulizeni CCM nayo ilipata Wangapi? 5.2 Millioni, hata ingechakachua Vipi, isingeweza kuiba Kura nyingi kiasi hicho, Je, CCM nayo ikiwaingiza hao Barabarani Hali itakuwaje? Jamani msione Simba kalowa Mkadhania ni Paka! Mmesahau Sumaye huyuhuyu na Bosi wake Mkapa alivyowafanya Wapinzani walipoandamana kule Pemba Unguja na Buguruni walipoandamana Kupinga Matokeo? Au hamumuelewi anapodai Hoja za CDM zijibiwe? Hamjui kwamba anamuona Kikwete na Pinda wamekuwa wapole sana kwa Wapinzani na anataka Wajibu Mapigo Kama Alivyofanya Yeye na Mkapa? Mnataka Hivyo?
 
Kwani Hoja zenyewe zinazotakiwa Kujibiwa na CCM kwenye Majukwaa ni zipi basi? Kama ni Dowans Suala hilo liko Mahakamani, ni Makosa kulijadili nje yake kabla hukumu haijatoka, Kama ni Kupanda bei ya Umeme na Mgao Tanesco imeshatoa Maelezo, Kama ni Mabomu ya Mbagala Serikali imeshatoa Tamko na Tunasubiri matokeo ya Uchunguzi ili ijulikane Hatua za Kuchukua na Watakao wajibishwa (ingawa CDM wameshatoa Hukuma kabla hata Mabomu yenyewe hajamalizika Kulipuka!) Wakati wa Kampeni, kila Chama kiliwasilisha hoja zake kwa Wananchi, CDM kiliwasilisha hoja zake (Wenyewe wakiziita "MABOMU") kwa Wananchi, CCM ilizijibu kwa Nguvu zote katika ngazi zote, Aidha CCM ilionesha ilichokifanya katika kila Kijiji, Kata, Mkoa na Taifa ndani ya Miaka 5 iliyopita na Mapungufu yake na Kile ambacho CCM itafanya kwa Miaka 5 ijayo endapo itapewa Ridhaa na Wananchi kuongoza tena, Kule ilikofanya Makosa ilipoteza Wabunge na Madiwani, kule ilikofanya Vizuri ilishinda (Kama Ina Uwezo mkubwa wa Kuiba kura si Ingeiba kote) Matokeo ya Jumla CCM ilishinda Urais, Wabunge na Madiwani Wengi
sana. Kazi ya CCM hivi sasa ni Kuisimamia Vizuri Serkali yake itekeleze Yale yaliyoahidiwa Kipindi cha Kampeni (ilani yake ya Uchaguzi) imepewa Kikatiba Miaka 5 kuyatekeleza. Sasa cha Ajabu hata miezi mingapi Haijapita, tayari CDM Inapanda Majukwaani na Mabarabarani na kutaka hoja zilezile za Wakati wa Kampeni zijibiwe tena, Kwa hiyo CCM isifanye kazi zake na Kujipanga upya Bali na yenyewe iingie Barabarani na kuanza Malumbano na CDM kwa Sababu tu CDM inataka hivyo, kwani wao ni Nani? Ikumbukwe CDM kutoka na Hoja na Sera zake wakati wa Kampeni ilipata Walioikubali kwenye Urais wapatao 2.2millioni ambao ni Watu wengi na Wengi wao ndio hao Tunaowaona Kwenye Maandamano yao, Lakini jiulizeni CCM nayo ilipata Wangapi? 5.2 Millioni, hata ingechakachua Vipi, isingeweza kuiba Kura nyingi kiasi hicho, Je, CCM nayo ikiwaingiza hao Barabarani Hali itakuwaje? Jamani msione Simba kalowa Mkadhania ni Paka! Mmesahau Sumaye huyuhuyu na Bosi wake Mkapa alivyowafanya Wapinzani walipoandamana kule Pemba Unguja na Buguruni walipoandamana Kupinga Matokeo? Au hamumuelewi anapodai Hoja za CDM zijibiwe? Hamjui kwamba anamuona Kikwete na Pinda wamekuwa wapole sana kwa Wapinzani na anataka Wajibu Mapigo Kama Alivyofanya Yeye na Mkapa? Mnataka Hivyo?

Huu ndo ugonjwa wa CCM, watu wengi walio wanachama wa CCM kuamini katika historia. Ndo maana CCM kinaangamia na wenye akili kila siku wanaonya CCM kinakufa, ila wenye chama wanaendelea kujifariji kuwa kwa kuwa chama kina dola hakiwezi kutoka.

Haya madai yanayorudiwa rudiwa kuwa CCM ilieleza sera zake wakati wa uchaguzi na watu wakakichagua kwa hiyo hakihitaji kueleza chochote ndo madai ambayo yanaonesha jinsi ambavyo CCM inakosa mwelekeo. Hivi unajua CCM wameahidi ahadi ngapi? Wamezitekelezaje au wanazishughulikiaje?

Kuna wengi vile vile wanaojifariji kuwa Chadema wanavutia watu wengi ni kama mwaka 1995. Wanashindwa kukumbuka kuwa 1995 ilibidi mwalimu mwenyewe aingilie kati na kumnadi mgombea wa CCM kwa nguvu sana. Bila mwalimu kuvua gloves na kuwavaa akina Mrema leo hii hadithi ingekuwa nyingine.

Halafu hao wanaosema sera zinaisha wakati wa uchaguzi, ni watu wasio elewa siasa. Siasa haziishi na uchaguzi, siasa zinaanza na uchaguzi. Ukishinda, walioshindwa hawalali wanaendelea kukushambulia kila unapoonesha udhaifu, uchaguzi unaofuata ukifika kama hukusimama, unaondoka.

Sasa siasa za kudumu ndo zimeshaingia. Chadema ina wanasiasa karibia hamsini ambao full time kazi yao kubwa ni kufanya siasa. wanasiasa wa CCM wamejazana serikalini wakila urojo. Unafikiri hawa wa Chadema watawaachia tu muda hawa wa CCM wale urojo serikalini na wapate usingizi?

Mazoea yana taabu yake. CCM ilishazoea vyama vya siasa vya msimu na sasa mambo yameanza kuwa tofauti badala ya kuunda mkakati mbadala mnachofanya ni kutishia kufuta vyama vinavyofanya siasa.

Ugonjwa wa CCM ni ule ule wa kuendekeza mfumo na taratibu za chama cha Kikomunisti, wakati mfumo ule umeshatupwa jalalani. CCM bado mnaendelea kuamini kuwa kuwepo kwenu serikalini ni advantage kwa hiyo hamhitaji kufanya chochote mbali ya kukaa na kusubiri uchaguzi unaofuata. Kuna hatari ya CCM kugeuka kuwa ndo chama cha msimu, kwani baada ya uchaguzi viongozi wote wa chama wanahamia serikalini, chama kinabaki kinaelea.

Matokeo yake ni ulevi wa madaraka na kutaka kutumia maguvu ya serikali hata pale isipofaa. Lakini kwa mwenendo wa CCM wa sasa hatuhitaji kuandikia mate hali wino upo. 2015 itawashangaza sana. Kwa nini hawajajifunza 2010? Tarehe 5 Februari wote tuliangalia pale Dodoma na uwanja wa Jamhuri ulikuwa mtupu! Wewe bado unaamini katika historia......
 
Mi naona ukimya wao unasababishwa na hoja nzito za CDM, ambazo nyingi majibu yake hayajibiki kirahisi. Sisiem kumebaki walalamikaji tu, wakiongozwa na mwenyekiti wao.
huyu mwenyekiti sijawahi kumwelewa, na hii ngwe yake ya pili ndo nazidi kumdelete kabisa miongoni mwa watu niliowahi hata kusikia majina yao
 
Back
Top Bottom