CCM ijiandae kisaikolojia hakuna namna!

CCM ijiandae kisaikolojia hakuna namna!

MAHANJU

JF-Expert Member
Joined
Aug 26, 2014
Posts
5,255
Reaction score
8,027
Hili limejidhihirisha leo kwenye viwanja vya Jangwani jijini Dar! Sikuamini kama watanzania leo wameamua kwa yakini kabisa kwamba hawaitaki CCM!Sio kuhudhuria kwenye mkutano tu bali ni pamoja na mwotikio wao wa salamu kwa viongozi waliokuwepo jukwaani.
Nduguzanguni hata wale mlioko CCM mkubali tu kwamba haya ni mabadiliko ya wazi na hayana mpinzani, mkubali kubadili fikra zenu maana ukweli ndio huo na kuendelea kuing'ang'ania ccm ni kupoteza muda
 
Mkuu kwa hali ilivyo sasa hivi nchini Tanzania kisiasa nilazima ccm wajiandae kisaikolojia kabisa kukabidhi madaraka kwa amani,maana hata kama watu waliokuwepo leo jangwani wakiamua kuipigia ukawa kura basi ccm ni chaaliiii
 
Hili limejidhihirisha leo kwenye viwanja vya Jangwani jijini Dar! Sikuamini kama watanzania leo wameamua kwa yakini kabisa kwamba hawaitaki CCM!Sio kuhudhuria kwenye mkutano tu bali ni pamoja na mwotikio wao wa salamu kwa viongozi waliokuwepo jukwaani.
Nduguzanguni hata wale mlioko CCM mkubali tu kwamba haya ni mabadiliko ya wazi na hayana mpinzani, mkubali kubadili fikra zenu maana ukweli ndio huo na kuendelea kuing'ang'ania ccm ni kupoteza muda
Tatizo ni huyu mtu tuanaetaka kumkabidhi mabadiliko, anaacha maswali mengi kuliko majibu.!
 
Nchi haichukuliwi kwa hotuba ya dakika kumi mwambie akagombee ujumbe wa shina
 
CCM haitakiwi kabisa ni panya hawa. Maana wameitafuna nchi hii
 
Nchi haichukuliwi kwa hotuba ya dakika kumi mwambie akagombee ujumbe wa shina

Nchi haiendelei kwa Usanii na vijembe, na story za vijiweni. Mabadiliko yanaanza kwenye hotuba na watu wakiingia ikulu ni kazi tuu, Tumechoka hotuba za masaa 4 zilizokua haziktekelezeki.
 
Wengine ni mafundi sana wa kusema midomoni lakini ni wazembe sana wakati wa utendaji; na wengine wamejaliwa sana utendaji na usimamizi wa mambo ya msingi lakini maneno yao ni machache sana kama Lowasa! Namchagua Lowasa!
 
Bora mama lowassa kuliko lowassa!

Mzee kajiandaa miaka 20 anataka kumtoa babu seya ndo Sera?
 
Nchi haichukuliwi kwa hotuba ya dakika kumi mwambie akagombee ujumbe wa shina

Ila inachukuliwa na kwa dk 56 za kushangaa polisi wanavamiwa, kwa kushangaa hospitali kukosa dawa huku pharmacy zikiwa na dawa, kwa kushangaa watanzania ni masikini, kushangaa kushangaa tu
 
Hili limejidhihirisha leo kwenye viwanja vya Jangwani jijini Dar! Sikuamini kama watanzania leo wameamua kwa yakini kabisa kwamba hawaitaki CCM!Sio kuhudhuria kwenye mkutano tu bali ni pamoja na mwotikio wao wa salamu kwa viongozi waliokuwepo jukwaani.
Nduguzanguni hata wale mlioko CCM mkubali tu kwamba haya ni mabadiliko ya wazi na hayana mpinzani, mkubali kubadili fikra zenu maana ukweli ndio huo na kuendelea kuing'ang'ania ccm ni kupoteza muda

Ukiwa na akili nyepesi utasumbuliwa sana na matukio. Ni kama desi tu. Wewe unaweza kuangamiza hata vizazi vyako kwa kukosa kuelewa mambo kwa picha pana.
 
huu ndio mwaka wa kuonyesha hasira zetu malofa. Ccm kwanza wasepe tumechoka, tumewachokaaa. Then tutaweka mifumo mipya ya kuiongoza tz mpya. Tatizo sio magufuli, tatizo ni ccm. Hatuna namna. Asanteni kwa uhuru, imetosha.
 
Unaweza kutusaidia hayo maswali ili wenye fursa ya karibu zaidi ya kuuliza wafanye hivyo?
 
Back
Top Bottom