Bishop Zachary Kakobe: Mimi si CCM wala CHADEMA, sina kati ya chama cha Siasa hata Kimoja

JPN

Senior Member
Jul 28, 2013
119
42
Anazungumzia juu ya kwanini anaenda kwenye Mialiko ya Kiserekali.. Ameaanza kuzungumza kwamba kanisa Hili LA FGBF siyo la Chama cha CHADEMA wala CCM wala chama chochote kingine.... Ndiyo anaendelea kuzungumza

juu ya kwanini anaenda kwenye Mialiko... Na kanisa Hili siyo CHADEMA wala CCM wala chama chochote kile....

======

"Sijawahi kuwa mwanachama wa chama cha Chadema wala CCM, na sina kadi ya vyama hivyo"-Kakobe

"Sijawahi kuwasiliana na kiongozi yoyote wa Chadema wala kuonana nao ana kwa ana, wala hawajawahi kuja ofisini kwangu, halijawahi kutokea"-Kakobe

"Niliwahi kuitikia mwaliko wa chama cha Chadema mara moja tu miaka michache iliyopita kwenye mkutano uliofanyika eneo la Mlimani City na nilienda kama baba anayeweza kualikwa na watoto"-Kakobe

"Wakati wa vuguvugu la katiba, niliwahi kwenda kwenye mkutano wa Chadema uliokuwa unafanyika katika viwanja vya Jangwani, na nikizungumza na Mbunge John Mnyika kwenye simu kuhusu mkutano huo, na nilikwenda"-Kakobe

"Hata Rais Magufuli akiniteua Leo siwezi kukubali, nitamueleza Nina kazi maalum ya kumtumikia Mungu, siwezi kuwa mbunge alafu nikakaa bungeni miezi mitatu niache kumtumia Mungu"-Kakobe

"Siwezi kuwa Mbunge wala Waziri, na hata siku ikitokea nimeteuliwa na Rais, nitasema asante lakini sitakubali"-Kakobe

"Waumini wangu si mnajua nina pesa, si mnnafahamu nilisema mimi ni tajiri kuliko serikali, si TRA wanajua walikuta fedha nzuri tu Benki, si walikuta akiba nzuri katika akaunti ya kanisa, utaninunua kwa bei gani? Sina bei mimi"-Kakobe

"Wanaosema mbona Askofu Kakobe anatuacha Chadema, " Niliwaacha wapi? Lini niliwahi kuwa na nyie? "-Kakobe

Habari zaidi...

Askofu Mkuu wa Kanisa la Full Gospel Bible (FGBF), Zachary Kakobe amewataka viongozi wa Chadema waliotukana viongozi wa dini watubu hadharani, wasipofanya hivyo, chama chao kitatumbukia kwenye shimo refu zaidi, hawataweza kuinuka tena.

Kiongozi huyo wa FGBF ametoa kauli hiyo leo Jumapili Januari 27, 2019 jijini Dar es Salaam wakati wa ibada kufuatia siku za hivi karibuni kuonekana mara kadhaa kwenye hafla za Rais John Magufuli na kupewa nafasi ya kuomba.

Pia, amesema yeye na kanisa hilo si wanachama wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo( Chadema). Hata hivyo, amesema aliwahi kuhudhuria mkutano mmoja tu wa Chadema uliofanyika Mlimani City na kwamba katika mkutano huo alihudhuria si kama mwanachama bali kama baba ambaye anaweza kualikwa na watoto wengi.

"Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe, sijawahi kuwa na mazungumzo naye; iwe kanisani au nyumbani au mahali popote. Hata katika mkutano ule nilipokelewa na viongozi wengine kabisa," amesema Askofu Kakobe. Amesema hajawahi kuonana wala kuzungumza kwa simu na mbunge wa jimbo la Ubungo (Chadema), Saed Kubenea ambaye anaongoza eneo ambalo kanisa lake lipo.

"Kama hamjui, nimehudhuria mikutano mingi zaidi ya CCM kuliko Chadema. Nakumbuka wakati mmoja niliwahi kuhudhuria mkutano wa wazee kumuaga Rais Benjamin Mkapa, nilialikwa na Yusuph Makamba. Wakati ule nilihudhuria mikutano mingi kwa sababu Makamba ni rafiki yangu sana," amesema.

Askofu Kakobe amesema kuhudhuria kwake mikutano ya Rais Magufuli kumeibua mitazamo tofauti, wengine wakisema ameahidiwa ubunge na wengine wakisema amenunuliwa. Hata hivyo, amekanusha madai hayo.

"Wanasema 'sasa inakuwaje umeanza kuandamana na Rais Magufuli, umeahidiwa ubunge? Nianze kukaa bungeni miezi mitatu, nani atafanya kazi hii. Hata nikiteuliwa, nitasema asante, nimeitwa kwa kazi moja tu."

"Wengine wanasema labda amenunuliwa, mimi? Si mnaelewa nina hela? Si wanafahamu nilisema nina hela kuliko Serikali? Si wanafahamu TRA walikuta fedha nzuri tu kwenye akaunti ya kanisa? Sasa unaninunua kwa bei gani, sina bei," amesema Askofu Kakobe huku waumini wake wakimshangilia.

CHANZO: Gazeti la Mwananchi.


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Anazungumzia juu ya kwanini anaenda kwenye Mialiko ya Kiserekali.. Ameaanza kuzungumza kwamba kanisa Hili LA FGBF siyo la Chama cha CHADEMA wala CCM wala chama chochote kingine.... Ndiyo anaendelea kuzungumza

juu ya kwanini anaenda kwenye Mialiko... Na kanisa Hili siyo CHADEMA wala CCM wala chama chochote kile....

======

"Sijawahi kuwa mwanachama wa chama cha Chadema wala CCM, na sina kadi ya vyama hivyo"-Kakobe

"Sijawahi kuwasiliana na kiongozi yoyote wa Chadema wala kuonana nao ana kwa ana, wala hawajawahi kuja ofisini kwangu, halijawahi kutokea"-Kakobe

"Niliwahi kuitikia mwaliko wa chama cha Chadema mara moja tu miaka michache iliyopita kwenye mkutano uliofanyika eneo la Mlimani City na nilienda kama baba anayeweza kualikwa na watoto"-Kakobe

"Wakati wa vuguvugu la katiba, niliwahi kwenda kwenye mkutano wa Chadema uliokuwa unafanyika katika viwanja vya Jangwani, na nikizungumza na Mbunge John Mnyika kwenye simu kuhusu mkutano huo, na nilikwenda"-Kakobe

"Hata Rais Magufuli akiniteua Leo siwezi kukubali, nitamueleza Nina kazi maalum ya kumtumikia Mungu, siwezi kuwa mbunge alafu nikakaa bungeni miezi mitatu niache kumtumia Mungu"-Kakobe

"Siwezi kuwa Mbunge wala Waziri, na hata siku ikitokea nimeteuliwa na Rais, nitasema asante lakini sitakubali"-Kakobe

"Waumini wangu si mnajua nina pesa, si mnnafahamu nilisema mimi ni tajiri kuliko serikali, si TRA wanajua walikuta fedha nzuri tu Benki, si walikuta akiba nzuri katika akaunti ya kanisa, utaninunua kwa bei gani? Sina bei mimi"-Kakobe

"Wanaosema mbona Askofu Kakobe anatuacha Chadema, " Niliwaacha wapi? Lini niliwahi kuwa na nyie? "-Kakobe


Sent using Jamii Forums mobile app

Mnaomshangaa Kakobe leo hii kubadilika hivi nadhani nanyi mnatakiwa mkapimwe ' akili ' zenu kwani inawezekana vipi Mtu umeshagundulika siyo Raia wa Tanzania huku ukiwa unadaiwa Kodi Kubwa na kama haitoshi hata eneo lako la Kanisa kuna ' Upanuzi ' mkubwa wa Barabara ya Mwendokasi inatakiwa kupitia hapo? Mnadhani Mwenzenu hadi ameamua Kujirudi na Kujipendekeza hivyo ni ' Popoma ' kwamba hajui analolifanya?
 
Mnaomshangaa Kakobe leo hii kubadilika hivi nadhani nanyi mnatakiwa mkapimwe ' akili ' zenu kwani inawezekana vipi Mtu umeshagundulika siyo Raia wa Tanzania huku ukiwa unadaiwa Kodi Kubwa na kama haitoshi hata eneo lako la Kanisa kuna ' Upanuzi ' mkubwa wa Barabara ya Mwendokasi inatakiwa kupitia hapo? Mnadhani Mwenzenu hadi ameamua Kujirudi na Kujipendekeza hivyo ni ' Popoma ' kwamba hajui analolifanya?
Sasa Ndio Asaliti Misimamo Yake Aliyoionesha Kwa Waumini? Nani Atamuamini Tena?
 
Swala si uanachama wa chama fulani
Kakobe unakosa kuusimamia ukweli unaohubiri
Umelidhulumu kanisa
Wengi wa watumishi kama Kakobe hamna hofu na Mungu
Mmekuwa waongo kushinda wakweli
Mnatumia mapungufu ya watu kujinufaisha kiuchumi

Yesu yu mlangoni utajibu ulivyojibu haya
Huu moto utaunguza wengi
Mungu shuka tukuone leta gharika kwa watu wanaojinufaisha kupitia jina lako
 
kakobe anajiingiza kwenye kundi la wahubiri wenye utata juu ya wanachohubiri na kuaminisha watu kumbe wenyewe hawaamini mahubiri yao. iweje anaruka futi mia misimamo yake kama si unafiki? ana tofauti gani na mafarisayo?
 
Kakobe mzee wa Mjini mjini mjanja Muhuni anawatafutia tu Gape CDM awaponyoke kwa vile nae ni binadamu basi tumbo kwanza. Mzee huyu tumemshuhudia akifanya Covert activities leo anajikana sio activitist ama kweli Njaa ni mbaya sana
 
Bado Gwajima Nae Kama Kakobe Tu, Kuna Mzee Wa Upako And Alike So, Hawa Haileweki Wanahubiri Nini? Wajaza Watu Wenye Misongo Ya Mawazo Wakiwaghilibu Kwa Hila Zao. Lini Waliwasaidia Waumini Wao Kuondokana Na Shida Zinazowakabili? Wanaishia Kufanya Syndicate Halafu Wanakuja Kuruka Futi Mia Hawahusiki.
 
Bora Wale Wanaojiita Mitume Na Manabii Na Makuhani Waishie Tu Huko Kwenye Utume Na Unabii Wao Wasije Kwenye Siasa Hawataeleweka. Mabishop Wanaruka Sana Mahubiri Yao Waliyoyachanganya Na Siasa. Wanakabiliwa Na Wanasiasa, Hawana Jinsi Ya Kujinasua Kutoka Kwenye Rangi Ya Kisiasa Waliyoionesha, Ni Kukana Tu Hawakuwa Na Rangi Hizo. Haya Ni Maajabu !
 
Askofu Mkuu wa Kanisa la Full Gospel Bible (FGBF), Zachary Kakobe amewataka viongozi wa Chadema waliotukana viongozi wa dini watubu hadharani, wasipofanya hivyo, chama chao kitatumbukia kwenye shimo refu zaidi, hawataweza kuinuka tena.

Kiongozi huyo wa FGBF ametoa kauli hiyo leo Jumapili Januari 27, 2019 jijini Dar es Salaam wakati wa ibada kufuatia siku za hivi karibuni kuonekana mara kadhaa kwenye hafla za Rais John Magufuli na kupewa nafasi ya kuomba.

Pia, amesema yeye na kanisa hilo si wanachama wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo( Chadema). Hata hivyo, amesema aliwahi kuhudhuria mkutano mmoja tu wa Chadema uliofanyika Mlimani City na kwamba katika mkutano huo alihudhuria si kama mwanachama bali kama baba ambaye anaweza kualikwa na watoto wengi.

"Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe, sijawahi kuwa na mazungumzo naye; iwe kanisani au nyumbani au mahali popote. Hata katika mkutano ule nilipokelewa na viongozi wengine kabisa," amesema Askofu Kakobe. Amesema hajawahi kuonana wala kuzungumza kwa simu na mbunge wa jimbo la Ubungo (Chadema), Saed Kubenea ambaye anaongoza eneo ambalo kanisa lake lipo.

"Kama hamjui, nimehudhuria mikutano mingi zaidi ya CCM kuliko Chadema. Nakumbuka wakati mmoja niliwahi kuhudhuria mkutano wa wazee kumuaga Rais Benjamin Mkapa, nilialikwa na Yusuph Makamba. Wakati ule nilihudhuria mikutano mingi kwa sababu Makamba ni rafiki yangu sana," amesema.

Askofu Kakobe amesema kuhudhuria kwake mikutano ya Rais Magufuli kumeibua mitazamo tofauti, wengine wakisema ameahidiwa ubunge na wengine wakisema amenunuliwa. Hata hivyo, amekanusha madai hayo.

"Wanasema 'sasa inakuwaje umeanza kuandamana na Rais Magufuli, umeahidiwa ubunge? Nianze kukaa bungeni miezi mitatu, nani atafanya kazi hii. Hata nikiteuliwa, nitasema asante, nimeitwa kwa kazi moja tu."

"Wengine wanasema labda amenunuliwa, mimi? Si mnaelewa nina hela? Si wanafahamu nilisema nina hela kuliko Serikali? Si wanafahamu TRA walikuta fedha nzuri tu kwenye akaunti ya kanisa? Sasa unaninunua kwa bei gani, sina bei," amesema Askofu Kakobe huku waumini wake wakimshangilia.

CHANZO: Gazeti la Mwananchi.
 
Kakobe ni mtu mdogo kama wahubiri matapeli wengine! Early 80s shemeji yangu alikwenda kusali akiamini akitoka huko mali itatelemka, akatoa pete za ndoa yake -dhababu , akiamini anampa Mungu. Mpaka leo analia kwanini alifanya hivyo!
Watu wangu wanaangamia kwa Kukosa Maarifa,unatoa sadaka 10,000 alafu nyumbani unakula Tembele alafu unasema ipo siku utakula vizuri..
 
Kakobe ni mtu mdogo kama wahubiri matapeli wengine! Early 80s shemeji yangu alikwenda kusali akiamini akitoka huko mali itatelemka, akatoa pete za ndoa yake -dhababu , akiamini anampa Mungu. Mpaka leo analia kwanini alifanya hivyo!
Alienda kanisani kumwabudu kakobe? Na hizo pete alimtolea Mungu au kakobe?
Ndugu,Mungu hadhihakiwi ndo maana shem wako alifirisika,Usitoe sadaka ili utajirike hapo ni lazima uharibikiwe,anamlaumu kakobe,kakobe ndo anayebariki watu?
Alienda kanisani kama vile anaenda kwa mganga wa kienyeji,eti alitoa pete za dhahabu ili atajirike,hahahahahah....mpe pole,

Sent using Jamii Forums mobile app
 
"Halima James Mdee Retweeted Boniface Jacob
Tuna MANABII wengi WA UONGO !! Na WACHACHE sana ni WA UKWELI... Waumini tuna wajibu wa KUWATAMBUA MANABII wa UKWELI na KUJUMUIKA NAO!! Hawa wanafiki/wafanyabiashara wa kiroho wakiachwa peke yao na NYUMBA zao za IBADA AKILI ITAWARUDIA."
 
Kama kuna baadhi ya viongozi wa chadema wamekukosea.kwa nini ukihukumu chama chote na kukitabiria mabaya?.Huyu mzee mhuni eeeeeh?.Mangapi aliyatabiri na bado hayakutimia?Mrema alikuwa raisi kama alivyotabiri?.Lowasa jee?Kwani Jiwe tayari ashatubu?.Au yeye ndio kwanza anatubu?.Huyo Yesu wake anayesema yuko pale kwake,kamuambia ahukumu?.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom