Acheni wivu wa kike na kunung'unika kama mmevunja ungo juzi, Lowassa ni Mkristo, ushiriki wake kanisani unawauma wapi? Oilcom anavyowajengea misikiti yake ile asiyoruhusu wanawake kuingia, kuna mtu amehoji kwa nini? Haya.......
Waziri Mkuu Mstaafu na Mbunge wa jimbo la Monduli, Mh. Edward Lowassa akikabidhi msaada wa
Tshs milioni 5 kwa Katibu Mkuu wa Baraza la Misikiti Tanzania (BAMITA) SHeikh Salum Sung'he kwa
ajili ya kuendeleza mipango kazi ya BAMITA.
(Unaona Sheikh alivyoinama kwa adabu?)
Katibu Mkuu wa BAMITA akizungumza na waandishi wa habari akimshukuru Mh. Lowassa
(Bila shaka kamsifia pia)
Lowassa huyu ndio unayemzungumzia?
Lowassa ndani ya RED CARPET, nafikiri unaona aina ya watu waliopanga mistari ili tu kupata fursa ya kushikana mkono na Mheshimiwa Noti. Wengine wanaandaa simu zao wapate picha ya mheshimiwa. Wake upande huu, waume zao upande huu. Watoto watakuwa nje.....mbona raha!
Huyu ni Askofu?
Wahasibu wetu hao......tunawaamini.
Hata Redio yetu, Radio Imaan....nayo imechangiwa!
Mheshimiwa huwa hagawi tende jamani hizo ni
ANKRA
Edward
'Maestro' Lowassa....cheka naye maisha yabadilike.
Akwiiiii! Muru ingine nasaniaga masai hafui kandambuga.....haba ago peku nafanya ibada
Wanaosema wewe sio ndugu yetu wana lao jambo.
NOTE: Tuache wivu wa kike, majungu na roho za manung'uniko. Hata Kinana anagawa fedha kila anapopita, tofauti ni kwamba Lowassa anataka mumrudie Allah na Jehova ilhali Kinana anawapeni mkanywe pombe.
Ni dhahiri kwamba, Lowassa anatoa fedha penye miradi ya maendeleo na si kwamba anazigawa tu watu wakanywe viroba. Kasi yenu ya shughuli za maendeleo ndio ita-determine kiasi gani mtapata kutoka kwa Mheshimiwa.
Lowassa Hoyeeeeee!
Edwars Ngoyai 'Maestro' Lowassa
kamua baba misikiti ing'ae