CCM Huu ni UDINI wa aina yake

CCM Huu ni UDINI wa aina yake

Mheshimiwa Edward Lowassa, watu wanakutaja sana kuwa una nia ya kugombea urais.

Wakati huo huo unasikika ukihaha kila kona ya Tanzania ukitembelea makanisa mbalimbali na kutoa misaada mikubwa mikubwa kwa mahitaji mbali mbali ya makanisa hayo kama ambavyo umeripotiwa na vyombo vya habari hapa chini:

Kanisa lamuandalia tuzo Lowassa

Filikunjombe, Ligola wajitosa kambi ya Lowassa, wamnadi kanisani Iringa. | Dullonet Tanzania

Mzee wa Mshitu: Lowassa ashiriki harambee ya kanisa Akyeri Meru

Mbeya Yetu: LOWASSA ACHANGIA MILIONI 10 KANISA LA EAGT TUNDUMA MBEYA

Lowassa ajiweka mbali na kampeni Arumeru,ajikita kanisani..


Msamaa.

LOWASSA AMWAGIA FEDHA KANISANI ~ Mwanafasihi Mahiri

Lowassa kuongoza Harambee ya Kanisa Nyakato Mwanza | Fikra Pevu | Kisima cha busara!

MH. LOWASSA AONGOZA HARAMBEE YA KUNUNUA BASI LA KWAYA LA KANISA LA KKKT,MSASANI JIJINI DAR ~ Father Kidevu

WAZIRI MKUU AWAMU YA NNE ACHANGISHA SH100 KANISANI DAR ES SALAAM. ~ JUMA MTANDA

habarimpya.com - Kanisa lazidi kumtumia Lowassa katika harambee

Lowassa aendesha harambee Kanisa la Moravian Mbezi Beach Dar | Blog ya habari Tanzania | Online Newspaper | Thehabari.com

Kutokana na haya ninapata maswali yafuatayo:

1. Je Mh. Lowassa, unatarajia kulipwa kura na WAKRISTO hao ambao unawasaidia kwa vihela hivyo?

2. Je huu si udini kwa kiongozi anayetarajia kugombea urais kutumia nyumba za ibada kupata umaarufu wa kisiasa?

3. Je haya yangefanywa na mwanasiasa asiye wa chama tawala ingezua mjadala gani?

Let us call a spade a spade. Kama ni UDINI tuuite UDINI bila kujali mtu huyo ni wa chama gani.

Hivi hakuna msikiti aliyochangia kweli? tukumbushane
 
Tatizo ni kutoa sadaka na kupiga kampeni. Sasa akialikwa kwenye harambee asitoe? Mbona misikitini nako anatoa? Kama ametoa mara moja tu basi endeleeni kumwalike ili amwage mapesa. Siri ya alivyozipata hizo pesa ni yake na Mungu wake, kwakuwa wapiga kura huwa na umri wa zaidi ya 18 watajua cha kufanya maana kura ni siri
Hayo maneno mekundu hapo chini yana maana gani?by JOHN BUKUKU on APRIL 21, 2013 in JAMII with NO COMMENTS

Picha .Askofu wa kituo cha maombezi na uponaji cha Overcomers Power Center (OPC) Dkt Boaz Sollo (kushoto) akimakabidhi tuzo ya heshima mfano wa ramani ya Tanzania waziri mkuu wa zamani Edward Lowassa leokatika hafla ya kuchangia ujenzi wa kanisa na kuendeleza kituo cha radio Overcomers Fm ,katika harambee hiyo Lowassa aliahidi kuachangia milioni 15 na kufanikisha kupata Tsh zaidi ya milioni 75 zikiwemo fedha taslimu na ahadi (picha na Francis Godwin)
Na Francis Godwin
WAZIRI mkuu mstaafu Edward Lowassa amesema kuwa mbali ya kuwa yeye si tajiri ila bado ataendelea kufanya kazi yake kwa ukaribu zaidi na jamii ikiwa ni pamoja na kushirikiana na marafiki zake kusaidia na kuwataka wale wote wenye kusema dhidi yake kuendelea kusema ila hatarudi nyuma katika kutoa misaada kama njia ya kutafuta baraka za Mungu.
Lowassa ambae pia alikabidhiwa tuzo ya heshima kwa ajili ya kuendeleza kulipigania Taifa la Tanzania ,huku mwenyewe akichangia kiasi cha Tsh milioni 15 na mbunge wa jimbo la Ludewa Deo Filikunjombe akichangia milioni 9 kati ya fedha zote zaidi ya Tsh milioni 75 zilizochangwa kwa ajili ya kuendeleza ujenzi wa kanisa la OPC mkoani Iringa kama njia ya kuhamasisha amani katika Taifa ametaka watanzania kuwapuuza wale wote wanaoeneza siasa za uchochezi .
“Nataka kuwaomba leo wachukieni wachochezi na pia niwaelezeni kuwa mimi si tajiri ila nina utajiri wa watu na ushawishi na ninafanya mambo haya ili kumbukumbu yangu iweze kuandikwa Mbinguni na nimekuwa nikialika watu wengi na nimekuwa nikifika wacha wenye kusema waseme watasema ila usiku watalala wenyewe ….sitaacha kusaidia kwa kuogopa kusemwa”
Akizungumza katika hafla hiyo iliyoandaliwa na kituo cha maombezi na uponyaji mkoani Iringa Overcomers Power Center (OPC) na kufanyika katika ukumbi wa St Dominic mjini Iringa leo Lowassa alisema kuwa yeye si tajiri kama ambavyo watu wanavyofikiri ila amekuwa akipewa nguvu na rafiki zake ambao wamekuwa wakimuunga mkono pindi anapoalikwa katika hafla mbali mbali.
“Nataka kwanza kuwashukuru ndugu zangu wa mkoa wa Iringa na napenda kumshukuru zaidi Askofu Dkt Boaz Sollo kwa kunialika mkoani Iringa …..ila napenda kuwaeleza kuwa si kwamba nachangia michango mbali mbali katika jamii kama mimi ni tajiri ila mimi ni mtumishi nisiye na faida na nayaweza yote katika yeye anitiaye nguvu Pia nawashukuru sana wabunge wenzangu ambao wamepata kushiriki name leo katika ziara hiyo akiwemo mbunge machachari bungeni Deo Filikunjombe , Kagi Lugola na dada yangu Ritta Kabati bila kumsahau mbunge Mendradi Kigola kwa kuungana nami leo naamini nao wamepanda mbegu bora”.
Lowassa alisema kuwa anatambua bado ana mialiko migi sana na lazima anaifanyia kazi mialiko yote kama ambavyo jamii imepata kumwalika na kuwa hata hatua ya mkoa wa Iringa kumpa tuzo hainamanishi kuwa ni mwisho wa yeye kualikwa.
Hata hivyo Lowassa alisema kuwa kwa upande wake anapongeza jitihada za askofu Dkt Sollo kwa kuwa na mipango na mitazamo ya kulisaidia Taifa kwa kuanzisha ujenzi wa kanisa kwa ajili ya kudumisha amani na kwenda mbali zaidi kwa kuanzisha kituo cha radio Overcomers Fm chambo ambacho kitatumika kudumisha amani ya mkoa wa Iringa na Taifa pia
Kuhusu amani ya Taifa la Tanzania LOwassa alisema kuwa alikuwa ni miongoni mwa watu walioalikwa Kenya katika sherehe ya kuapishwa Rais mpya wa Kenya Uhuru Kenyatta ila sehemu kubwa ya wote waliotoa salam zao walitumia muda mwingi kupongeza vyombo vya habari kwa kulinda amani na hivyo kuvitaka vyombo vya habari za Tanzania na wanahabari kuendelea kuandika habari bila kuhatarisha amani ya Taifa
“Tusiruhusi amani ya nchi yetu iyumbishwe na mtu awaye yeyote na kila mtanzania anapaswa kulinda amani hii kwa nguvu zote ….Nawaombeni wanahabari tunzeni amani yetu…wapuuzeni wale wote wanaoch0chea machafuko katika Taifa hili ….tuachane na udini wala ukabila katika taifa letu ila “
Katika hatua nyingine Lowassa aliwapongeza wabunge wa CCM ambao wameendelea kupigania wanyonge bungeni akiwemo Deo Filikunjombe mbunge wa Ludewa na mbunge wa jimbo la Mwibara Kagi Lugola kuwa ni miongoni mwa wabunge ambao amekuwa akiwapenda kutokana na kusema kweli bungeni.
Kwa upande wake mbunge Filikunjombe alisema kuwa mbali ya kutoa ahadi ya kuchangia kiasi cha Tsh milioni 9 ila bado atamwalika Lowassa jimboni kwake Ludewa na kuwa kanisa hilo la OPC halijakosea kumpa tuzo ambayo ni ramani ya Tanzania kutokana na Lowassa kuwa ni mtu wa watu mpendwa na watu na kuwa tuzo hiyo ina maana kubwa na hawajakupa ramani ya jimboni kwako Monduli
Filikunjombe alimtaka Lowassa kuendelea kuchapa kazi na kuwa hajakosea kuwaalika wao kwani bungeni kuna wabunge zaidi ya 300 ina amewachagua wao pekee ni jambo la kumshukuru na kumfananisha L0wassa na mti unaopigwa mawe kuwa ni mti wenye matunda
“Nakuomba Lowassa simama Imara sisi wana Iringa tupo nyuma yako na niseme tuna kazi kubwa ya kuifanya katika Taifa hili kubwa ni kumwomba Mungu na makanisa na dini zote kuungana katika maombi zaidi kwani vita ni kubwa mbele “
Kwa upande askofu Dkt Sollo mbali ya kumpongeza Lowassa bado alisema kuwa wao kama kanisa wataendelea kumwombea afya njema na kuona kuwa mambo yake yanafanikiwa na ndio maana ya kumpa tuzo hiyo ya heshima.
Sollo alisema kuwa mchango wa TSh milioni 15 ulioahidiwa na Lowassa na ule wa milioni 9 ulioahidiwa na mbunge wa jimbo la Ludewa Deo Filikunjombe ni mchango ambao wao wanaupongeza na kuwapongeza wabunge wengine akiwemo Ritta Kabati aliyeahidi Tsh milioni 2 ,Benki ya wananchi Mufindi milioni 2 , mwenyekiti wa CCM mkoa wa Iringa Jesca Msambatavangu milioni 2 mfanyabiashara Salim Abri milioni 1 na wengine wengi ambao wamepelekea kupata zaidi ya Tsh milioni zaidi ya 75 pesa taslim na ahadi .
 
Tatizo ni kutoa sadaka na kupiga kampeni. Sasa akialikwa kwenye harambee asitoe? Mbona misikitini nako anatoa? Kama ametoa mara moja tu basi endeleeni kumwalike ili amwage mapesa. Siri ya alivyozipata hizo pesa ni yake na Mungu wake, kwakuwa wapiga kura huwa na umri wa zaidi ya 18 watajua cha kufanya maana kura ni siri
Hayo maneno mekundu hapo chini yana maana gani?

by
JOHN BUKUKU on APRIL 21, 2013 in JAMII with NO COMMENTS


Picha .Askofu wa kituo cha maombezi na uponaji cha Overcomers Power Center (OPC) Dkt Boaz Sollo (kushoto) akimakabidhi tuzo ya heshima mfano wa ramani ya Tanzania waziri mkuu wa zamani Edward Lowassa leokatika hafla ya kuchangia ujenzi wa kanisa na kuendeleza kituo cha radio Overcomers Fm ,katika harambee hiyo Lowassa aliahidi kuachangia milioni 15 na kufanikisha kupata Tsh zaidi ya milioni 75 zikiwemo fedha taslimu na ahadi (picha na Francis Godwin)
Na Francis Godwin
WAZIRI mkuu mstaafu Edward Lowassa amesema kuwa mbali ya kuwa yeye si tajiri ila bado ataendelea kufanya kazi yake kwa ukaribu zaidi na jamii ikiwa ni pamoja na kushirikiana na marafiki zake kusaidia na kuwataka wale wote wenye kusema dhidi yake kuendelea kusema ila hatarudi nyuma katika kutoa misaada kama njia ya kutafuta baraka za Mungu.
Lowassa ambae pia alikabidhiwa tuzo ya heshima kwa ajili ya kuendeleza kulipigania Taifa la Tanzania ,huku mwenyewe akichangia kiasi cha Tsh milioni 15 na mbunge wa jimbo la Ludewa Deo Filikunjombe akichangia milioni 9 kati ya fedha zote zaidi ya Tsh milioni 75 zilizochangwa kwa ajili ya kuendeleza ujenzi wa kanisa la OPC mkoani Iringa kama njia ya kuhamasisha amani katika Taifa ametaka watanzania kuwapuuza wale wote wanaoeneza siasa za uchochezi .
"Nataka kuwaomba leo wachukieni wachochezi na pia niwaelezeni kuwa mimi si tajiri ila nina utajiri wa watu na ushawishi na ninafanya mambo haya ili kumbukumbu yangu iweze kuandikwa Mbinguni na nimekuwa nikialika watu wengi na nimekuwa nikifika wacha wenye kusema waseme watasema ila usiku watalala wenyewe ….sitaacha kusaidia kwa kuogopa kusemwa"
Akizungumza katika hafla hiyo iliyoandaliwa na kituo cha maombezi na uponyaji mkoani Iringa Overcomers Power Center (OPC) na kufanyika katika ukumbi wa St Dominic mjini Iringa leo Lowassa alisema kuwa yeye si tajiri kama ambavyo watu wanavyofikiri ila amekuwa akipewa nguvu na rafiki zake ambao wamekuwa wakimuunga mkono pindi anapoalikwa katika hafla mbali mbali.
"Nataka kwanza kuwashukuru ndugu zangu wa mkoa wa Iringa na napenda kumshukuru zaidi Askofu Dkt Boaz Sollo kwa kunialika mkoani Iringa …..ila napenda kuwaeleza kuwa si kwamba nachangia michango mbali mbali katika jamii kama mimi ni tajiri ila mimi ni mtumishi nisiye na faida na nayaweza yote katika yeye anitiaye nguvu Pia nawashukuru sana wabunge wenzangu ambao wamepata kushiriki name leo katika ziara hiyo akiwemo mbunge machachari bungeni Deo Filikunjombe , Kagi Lugola na dada yangu Ritta Kabati bila kumsahau mbunge Mendradi Kigola kwa kuungana nami leo naamini nao wamepanda mbegu bora".
Lowassa alisema kuwa anatambua bado ana mialiko migi sana na lazima anaifanyia kazi mialiko yote kama ambavyo jamii imepata kumwalika na kuwa hata hatua ya mkoa wa Iringa kumpa tuzo hainamanishi kuwa ni mwisho wa yeye kualikwa.
Hata hivyo Lowassa alisema kuwa kwa upande wake anapongeza jitihada za askofu Dkt Sollo kwa kuwa na mipango na mitazamo ya kulisaidia Taifa kwa kuanzisha ujenzi wa kanisa kwa ajili ya kudumisha amani na kwenda mbali zaidi kwa kuanzisha kituo cha radio Overcomers Fm chambo ambacho kitatumika kudumisha amani ya mkoa wa Iringa na Taifa pia
Kuhusu amani ya Taifa la Tanzania LOwassa alisema kuwa alikuwa ni miongoni mwa watu walioalikwa Kenya katika sherehe ya kuapishwa Rais mpya wa Kenya Uhuru Kenyatta ila sehemu kubwa ya wote waliotoa salam zao walitumia muda mwingi kupongeza vyombo vya habari kwa kulinda amani na hivyo kuvitaka vyombo vya habari za Tanzania na wanahabari kuendelea kuandika habari bila kuhatarisha amani ya Taifa
"Tusiruhusi amani ya nchi yetu iyumbishwe na mtu awaye yeyote na kila mtanzania anapaswa kulinda amani hii kwa nguvu zote ….Nawaombeni wanahabari tunzeni amani yetu…wapuuzeni wale wote wanaoch0chea machafuko katika Taifa hili ….tuachane na udini wala ukabila katika taifa letu ila "
Katika hatua nyingine Lowassa aliwapongeza wabunge wa CCM ambao wameendelea kupigania wanyonge bungeni akiwemo Deo Filikunjombe mbunge wa Ludewa na mbunge wa jimbo la Mwibara Kagi Lugola kuwa ni miongoni mwa wabunge ambao amekuwa akiwapenda kutokana na kusema kweli bungeni.
Kwa upande wake mbunge Filikunjombe alisema kuwa mbali ya kutoa ahadi ya kuchangia kiasi cha Tsh milioni 9 ila bado atamwalika Lowassa jimboni kwake Ludewa na kuwa kanisa hilo la OPC halijakosea kumpa tuzo ambayo ni ramani ya Tanzania kutokana na Lowassa kuwa ni mtu wa watu mpendwa na watu na kuwa tuzo hiyo ina maana kubwa na hawajakupa ramani ya jimboni kwako Monduli
Filikunjombe alimtaka Lowassa kuendelea kuchapa kazi na kuwa hajakosea kuwaalika wao kwani bungeni kuna wabunge zaidi ya 300 ina amewachagua wao pekee ni jambo la kumshukuru na kumfananisha L0wassa na mti unaopigwa mawe kuwa ni mti wenye matunda
"Nakuomba Lowassa simama Imara sisi wana Iringa tupo nyuma yako na niseme tuna kazi kubwa ya kuifanya katika Taifa hili kubwa ni kumwomba Mungu na makanisa na dini zote kuungana katika maombi zaidi kwani vita ni kubwa mbele "
Kwa upande askofu Dkt Sollo mbali ya kumpongeza Lowassa bado alisema kuwa wao kama kanisa wataendelea kumwombea afya njema na kuona kuwa mambo yake yanafanikiwa na ndio maana ya kumpa tuzo hiyo ya heshima.
Sollo alisema kuwa mchango wa TSh milioni 15 ulioahidiwa na Lowassa na ule wa milioni 9 ulioahidiwa na mbunge wa jimbo la Ludewa Deo Filikunjombe ni mchango ambao wao wanaupongeza na kuwapongeza wabunge wengine akiwemo Ritta Kabati aliyeahidi Tsh milioni 2 ,Benki ya wananchi Mufindi milioni 2 , mwenyekiti wa CCM mkoa wa Iringa Jesca Msambatavangu milioni 2 mfanyabiashara Salim Abri milioni 1 na wengine wengi ambao wamepelekea kupata zaidi ya Tsh milioni zaidi ya 75 pesa taslim na ahadi .
 
Mwacheni arejeshe pesa alizoibia watanzania vipi nyinyi!!

Sidhani kama waumini wa Misikiti huwa wanachangia kihivyo wakichangishwa zaidi watachangia coin za kufa mtu
 
Hivi hakuna msikiti aliyochangia kweli? tukumbushane
Ameshachangia. Lakini swali kwako, kama kiongozi wa Chadema au Cuf au NCCR akifanya afanyayo huyu huyu, nyuzi ngapi zitaanzishwa hapa JF kwa hoja ya UDINI?
 
kule mwanza alichangisha ml 500 wao walijua wangepata ml 300!
 
Majuzi amekuja hapa Mwanza na amechangia redio ya kiislamu IQRA FM zaidi ya millioni mia tano. Hilo halisemwi. Mwacheni Rais Mtarajiwa anayeweza akatumia pesa zake kusaidia wengine......
 
Hapo ndipo CCM baba RITZ 1 woote mtandaoni wataigeuka CCM na kumuunga mkono SULTANI
 
Ameshachangia. Lakini swali kwako, kama kiongozi wa Chadema au Cuf au NCCR akifanya afanyayo huyu huyu, nyuzi ngapi zitaanzishwa hapa JF kwa hoja ya UDINI?
Mtu wa Shamba, mimi nakuunga mkono.. Hata hao wanaounga mkono CCM hivi leo kwa sababu ya dini... Akipitishwa LOWASA watamwachia CHAMA.
 
Ameshachangia. Lakini swali kwako, kama kiongozi wa Chadema au Cuf au NCCR akifanya afanyayo huyu huyu, nyuzi ngapi zitaanzishwa hapa JF kwa hoja ya UDINI?
mbona haujaweka link hapo juu. au ndo walewale mnaotaka kuendeleza mipasuko ya kidini?
nikisoma bandiko lako na comment zako naiona kitu kama ajenda ya siri.
 
mbona haujaweka link hapo juu. au ndo walewale mnaotaka kuendeleza mipasuko ya kidini?
nikisoma bandiko lako na comment zako naiona kitu kama ajenda ya siri.
Umejiuliza kwa nini pesa zake hazimwagi kwa vikundi vya vijana, au wakina mama wajasiriamali, au kwenye nyumba za kutunza wasiojiweza? Hao si wahitaji? Kwa nini kwenye vikundi vya dini (wakristo kwa waislamu)?

Think big!
 
Wewe unaishi wapi ? hapa Tanzania ..ukitoa Msikitini ndio inaitwa udini lakini ...ukitoa Kanisani inaitwa Harambee au sadaka...
 
Mliwah kumwalika misikitin hakuwachangial?© hebu toa umalayw wako hapa
 
ingekuwa ni mwanasiasa muislam anafanya hayo misikitini, hakika angesha kufa kisiasa. Wangemmaliza kwa kila aina ya hilo.

Acheni wivu wa kike na kunung'unika kama mmevunja ungo juzi, Lowassa ni Mkristo, ushiriki wake kanisani unawauma wapi? Oilcom anavyowajengea misikiti yake ile asiyoruhusu wanawake kuingia, kuna mtu amehoji kwa nini? Haya.......

7.jpg


Waziri Mkuu Mstaafu na Mbunge wa jimbo la Monduli, Mh. Edward Lowassa akikabidhi msaada wa
Tshs milioni 5 kwa Katibu Mkuu wa Baraza la Misikiti Tanzania (BAMITA) SHeikh Salum Sung'he kwa
ajili ya kuendeleza mipango kazi ya BAMITA.

(Unaona Sheikh alivyoinama kwa adabu?)


4.jpg


Katibu Mkuu wa BAMITA akizungumza na waandishi wa habari akimshukuru Mh. Lowassa

(Bila shaka kamsifia pia)

LOWASSA1.jpg


Lowassa huyu ndio unayemzungumzia?

LOWASSA5.jpg



Lowassa ndani ya RED CARPET, nafikiri unaona aina ya watu waliopanga mistari ili tu kupata fursa ya kushikana mkono na Mheshimiwa Noti. Wengine wanaandaa simu zao wapate picha ya mheshimiwa. Wake upande huu, waume zao upande huu. Watoto watakuwa nje.....mbona raha!

LOWASSA2.jpg


Huyu ni Askofu?


LOWASSA3.jpg


Wahasibu wetu hao......tunawaamini.

LOWASSA7.jpg


Hata Redio yetu, Radio Imaan....nayo imechangiwa!

Lowasa+mufti.JPG


Mheshimiwa huwa hagawi tende jamani hizo ni ANKRA

IMG_5817.JPG


Edward 'Maestro' Lowassa....cheka naye maisha yabadilike.

maulid5.jpg


Akwiiiii! Muru ingine nasaniaga masai hafui kandambuga.....haba ago peku nafanya ibada

3.jpg


Wanaosema wewe sio ndugu yetu wana lao jambo.


NOTE: Tuache wivu wa kike, majungu na roho za manung'uniko. Hata Kinana anagawa fedha kila anapopita, tofauti ni kwamba Lowassa anataka mumrudie Allah na Jehova ilhali Kinana anawapeni mkanywe pombe.

Ni dhahiri kwamba, Lowassa anatoa fedha penye miradi ya maendeleo na si kwamba anazigawa tu watu wakanywe viroba. Kasi yenu ya shughuli za maendeleo ndio ita-determine kiasi gani mtapata kutoka kwa Mheshimiwa.

Lowassa Hoyeeeeee!


Lowassa.jpg


Edwars Ngoyai 'Maestro' Lowassa

kamua baba misikiti ing'ae
 
unaelewa maana ya udini????udini ni neno pana ambalo kimsingi lina mazingira mengi nje ya nyumba za ibada so "watchout"
Umejiuliza kwa nini pesa zake hazimwagi kwa vikundi vya vijana, au wakina mama wajasiriamali, au kwenye nyumba za kutunza wasiojiweza? Hao si wahitaji? Kwa nini kwenye vikundi vya dini (wakristo kwa waislamu)?
 
Umejiuliza kwa nini pesa zake hazimwagi kwa vikundi vya vijana, au wakina mama wajasiriamali, au kwenye nyumba za kutunza wasiojiweza? Hao si wahitaji? Kwa nini kwenye vikundi vya dini (wakristo kwa waislamu)?
Acheni wivu wa kike na kunung'unika kama mmevunja ungo juzi, Lowassa ni Mkristo, ushiriki wake kanisani unawauma wapi? Oilcom anavyowajengea misikiti yake ile asiyoruhusu wanawake kuingia, kuna mtu amehoji kwa nini? Haya.......

7.jpg


Waziri Mkuu Mstaafu na Mbunge wa jimbo la Monduli, Mh. Edward Lowassa akikabidhi msaada wa
Tshs milioni 5 kwa Katibu Mkuu wa Baraza la Misikiti Tanzania (BAMITA) SHeikh Salum Sung'he kwa
ajili ya kuendeleza mipango kazi ya BAMITA.

(Unaona Sheikh alivyoinama kwa adabu?)


4.jpg


Katibu Mkuu wa BAMITA akizungumza na waandishi wa habari akimshukuru Mh. Lowassa

(Bila shaka kamsifia pia)

LOWASSA1.jpg


Lowassa huyu ndio unayemzungumzia?

LOWASSA5.jpg



Lowassa ndani ya RED CARPET, nafikiri unaona aina ya watu waliopanga mistari ili tu kupata fursa ya kushikana mkono na Mheshimiwa Noti. Wengine wanaandaa simu zao wapate picha ya mheshimiwa. Wake upande huu, waume zao upande huu. Watoto watakuwa nje.....mbona raha!

LOWASSA2.jpg


Huyu ni Askofu?


LOWASSA3.jpg


Wahasibu wetu hao......tunawaamini.

LOWASSA7.jpg


Hata Redio yetu, Radio Imaan....nayo imechangiwa!

Lowasa+mufti.JPG


Mheshimiwa huwa hagawi tende jamani hizo ni ANKRA

IMG_5817.JPG


Edward 'Maestro' Lowassa....cheka naye maisha yabadilike.

maulid5.jpg


Akwiiiii! Muru ingine nasaniaga masai hafui kandambuga.....haba ago peku nafanya ibada

3.jpg


Wanaosema wewe sio ndugu yetu wana lao jambo.


NOTE: Tuache wivu wa kike, majungu na roho za manung'uniko. Hata Kinana anagawa fedha kila anapopita, tofauti ni kwamba Lowassa anataka mumrudie Allah na Jehova ilhali Kinana anawapeni mkanywe pombe.

Ni dhahiri kwamba, Lowassa anatoa fedha penye miradi ya maendeleo na si kwamba anazigawa tu watu wakanywe viroba. Kasi yenu ya shughuli za maendeleo ndio ita-determine kiasi gani mtapata kutoka kwa Mheshimiwa.

Lowassa Hoyeeeeee!


Lowassa.jpg


Edwars Ngoyai 'Maestro' Lowassa

kamua baba misikiti ing'ae
 
Wewe unaishi wapi ? hapa Tanzania ..ukitoa Msikitini ndio inaitwa udini lakini ...ukitoa Kanisani inaitwa Harambee au sadaka...

Kweli basi Lowassa ni mdini, manake kaichangia misikiti mingi tu. Angalia post yangu nyingine
 
Back
Top Bottom