CCM Hali mbaya, Janja yake Yabainika !

CCM Hali mbaya, Janja yake Yabainika !

Goodrich

JF-Expert Member
Joined
Jan 29, 2012
Posts
2,091
Reaction score
1,179
Hali ni mbaya upande wa ccm baada ya hila zake za kuchakachua rasimu ya katiba iliyowasiliswa na Tume ya Jaji Joseph Warioba kubainika.

Kazi ya BMK ilikuwa ni kujadili namna ya kutekeleza maoni ya wananchi na sio kuyakataa na kuja na rasimu mpya.

Imebainika kwamba kwa mujibu wa sheria ya mabadiliko ya katiba, 2012, waliojitoa kwenye bunge maalumu la katiba ni ccm kutokana na uamuzi wao wa kuachana na rasimu iliyowasilishwa na Tume na kuamua kujadili rasimu iliyowasilishwa na kikundi fulani cha ccm kinyume cha sheria ya mabadiliko ya katiba.

Aidha kauli za baadhi ya makada wa ccm ambao wameonyesha kukerwa na hila hizi na kuweka wazi kuwa itakuwa ngumu katiba kupatikana bila UKAWA, kauli ya msajili kuwataka ccm warejee kwenye rasimu ya warioba, na ukimya wa walioandaa rasimu ya ccm vinaashiria hali ni mbaya ndani ya ccm.

Hivi sasa kuna mnyukano ndani ya ccm ambapo wakongwe wanadai hakukuwa na haja ya kuigharimu nchi kwa kuanzisha mchakato wa katiba na mwisho wa siku kuyakataa maoni ya wananchi.

Wengine wamehoji itakuwaje Rais wa Muungano akiwa Mzanzibari, maana Zanzibar itakuwa na Marais wawili, na Tanganyika itakuwa haina Rais hasa ikizingatiwa kuwa nafasi za umakamu hazina nguvu yoyote kikatiba wala kisheria.


NB
Tujadili bila kuweka ushabiki wala itikadi.
Hili ni suala la kitaifa.
 
Kuna vitu viwili ambavyo ni sahihi na ccm wanaviogopa sana ; Serikali moja na serikali tatu
1. Serikali moja - ilikuwa muafaka sana. Ila wanaiogopa Zanzibar.
2. Serikali tatu - wanaogopa kuondoa dhana ya chama kushika hatamu.

Hali hiyo imewafanya wapiganie serikali mbili ambazo sio sahihi kwa kuwa Tanganyika inapoteza utaifa wake
 
Katiba mpya haukuwa mpango wa ccm bali ni dhamira binafsi ya rais kikwete, na amekwama baada ya kushinikizwa na makada wenzake ndani ya ccm, kwa kupenyeza rasimu ya chama badala ya ile iliyopendekezwa na tume kwa niaba ya wananchi!
 
Kuna hatari ya taifa kugawanyika vipande vikuu viwili.Tayari taasisi za kidini hasa Roman catholic wamebaini makosa yao ya awali. wiki jana tumeshuhudia U-TURN kali kutoka TEC baada ya kutoka sauti ya individual bishops wakilaumu ukawa bila kujua kuwa ukawa ni wananchi.
 
Rudini bungeni mkajadili rasimu ya pili ambayo ndiyo maoni ya watanzania.
Nimemnukuu askofu niwemugizi.
 
umeandika ukweli mtupu ! Ccm imejinasisha yenyewe ! Lakini tuliwajulisha mapema sana kuhusu hili .
 
umeandika ukweli mtupu ! Ccm imejinasisha yenyewe ! Lakini tuliwajulisha mapema sana kuhusu hili .

MKUU REjEA KAULI YA ASKOFU ZACKARIA KAKOBE.
"WATARUMBANA WAO KWA WAO NA HAWATAFIKIA MWAFAKA,WATAGAWANYIKA MAKUNDI KWA MAKUNDI NA MWISHO WATASAMBARATIKA"
 
Hali ni mbaya upande wa ccm baada ya hila zake za kuchakachua rasimu ya katiba iliyowasiliswa na Tume ya Jaji Joseph Warioba kubainika.

Imebainika kwamba kwa mujibu wa sheria ya mabadiliko ya katiba, 2012, waliojitoa kwenye bunge maalumu la katiba ni ccm.

Kujitoa kwa ccm kisheria kunatokana na uamuzi wao wa kuachana na rasimu iliyowasilishwa na Tume na kuamua kujadili rasimu iliyowasilishwa na kikundi fulani cha ccm kinyume cha sheria ya mabadiliko ya katiba.

Aidha kauli za baadhi ya makada wa ccm ambao wameonyesha kukerwa na hila hizi na kuweka wazi kuwa itakuwa ngumu katiba kupatikana bila UKAWA, kauli ya msajili kuwataka ccm warejee kwenye rasimu ya warioba, na ukimya wa walioandaa rasimu ya ccm vinaashiria hali ni mbaya ndani ya ccm.

Hivi sasa kuna mnyukano ndani ya ccm ambapo wakongwe wanadai hakukuwa na haja ya kuigharimu nchi kwa kuanzisha mchakato wa katiba na mwisho wa siku kuyakataa maoni ya wananchi.


NB
Tujadili bila kuweka ushabiki wala itikadi.
Hili ni suala la kitaifa.
Tatizo letu ni kujifanya kutokuona chanzo cha KUJIKWAA na kubaki kulaumu pale TUANGUKIAPO.
 
Warudi njia kuu haraka iwezekanavyo,walifanya kampeni kubwa nazagharama kuhubiri kuwa ukawa wameharibu mchakato wa katiba bila kujua kuwa uongo hupanda kwa rift na ukweli hupanda kwa ngazi

40 za ccm zimetimia,mabaya yao yameonekana hadharani na mkosaji mkubwa kishajulikana,yu wapi bulembo na paulo?
 
Tatizo letu ni kujifanya kutokuona chanzo cha KUJIKWAA na kubaki kulaumu pale TUANGUKIAPO.


mkuu weka mawazo yako bayana yatunufaishe, ulitaka kusema nini au unamaanisha nini.
 
Kuna hatari ya taifa kugawanyika vipande vikuu viwili.Tayari taasisi za kidini hasa Roman catholic wamebaini makosa yao ya awali. wiki jana tumeshuhudia U-TURN kali kutoka TEC baada ya kutoka sauti ya individual bishops wakilaumu ukawa bila kujua kuwa ukawa ni wananchi.
Mkuu, TEC inajua fika kuwa UKAWA ni WANANCHI ila sijui kuna nini kinachofanya kila mtu awaseme UKAWA kana kwamba ndio CHANZO cha BMK kukwama. Wengi hawasemi na kuilaumu CCM kwa kusababisha hali hii kwanza kwa kutoijadili Rasimu ya katiba iliyowasilishwa na tume na pili lugha chafu waliyokuwa wakiitumia wabunge/jumbe wake mpaka kupelekea UKAWA kususia vikao. Kwanza aliyeanzisha UKAWA ni hao hao CCM.
 
Kuna vitu viwili ambavyo ni sahihi na ccm wanaviogopa sana ; Serikali moja na serikali tatu
1. Serikali moja - ilikuwa muafaka sana. Ila wanaiogopa Zanzibar.
2. Serikali tatu - wanaogopa kuondoa dhana ya chama kushika hatamu.

Hali hiyo imewafanya wapiganie serikali mbili ambazo sio sahihi kwa kuwa Tanganyika inapoteza utaifa wake

na mtanganyika yeyote anayependa serikal mbili ni mjing a
 
Back
Top Bottom