Herbalist Dr MziziMkavu
JF-Expert Member
- Feb 3, 2009
- 42,318
- 33,125
MAKAMU Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Pius Msekwa amesema chama hicho hakiwezi kushindwa katika uchaguzi mkuu ujao kwa kuwa ni sawa na mto Rufiji ambao hauwezi kukauka.
Alifafanua mto Rufiji, hauwezi kukauka kutokana na mtu au watu wachache kuchota maji yake kwa lengo la kuukausha.
Msekwa alitoa kauli hiyo, kutokana na kuwepo taarifa za baadhi ya wabunge wachache wanaotishia kukihama chama hicho baada ya bunge kuvunjwa.
Msekwa alisema hayo jana akijibu swali aliloulizwa na waandishi wa habari katika mkutano wake na waandishi uliofanyika ofisi ndogo za chama hicho kwa lengo la kutangaza rasmi tarehe ya kuchukua fomu kwa wanachama wa chama hicho wanaotaka kugombea kuteuliwa katika nafasi ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Rais wa Zanzibar na kwamba shughuli hiyo, inatarajiwa kufanyika Juni 21 hadi Julai 1 mwaka huu.
Msekwa alisema chama hicho, hakihofii vitisho hivyo na mbunge yeyote mwenye nia ya kukikimbia chama hicho baada ya bunge kuvunjwa hawezi kusababisha madhara yoyote kwa sababu CCM ina wanachama wa kutosha kukipa ushindi katika chaguzi ujao.
Chama chetu hakitetereki, kama kuna hayo mliyouliza ya kukimbiwa na viongozi wetu, hii ni kwa sababu mwaka 2005 waliondoka watu muhimu kama Njelu Kasaka, lakini hatukutetereka na alirudi kundini na chama kinaendelea kama kawaida, alifafanua Msekwa.
Alisema watu wengi maarufu waliondoka katika chama hicho akiwemo aliyekuwa Naibu Waziri Mkuu, Agustino Mrema na kujipatia maarufu na wanachama wengi, lakini chama hicho hakikuyumba.
Akizungumzia kuhusu wagombea wa nafasi hiyo, Msekwa aliwataka kuwa na busara ya kujichunguza wenyewe kama wanakubalika ndipo waende kuchukua fomu za kugombea kuteuliwa nafasi hizo.
Alisema gharama za fomu hizo ni Sh 1milioni kwa nafasi ya Rais wa Jamhuri ya Muungano na kwamba zitatolewa na kurudishwa kwa katibu mkuu wa chama hicho makao makuu ya chama yaliyopo Dodoma na wale watakaochukua fomu kwa ajili ya nafasi ya Rais kwa Zanzibar wanatakiwa kuchukua na kuzirejesha fomu hizo kwa Naibu Katibu Mkuu, ofisi ya chama hicho zilizopo Kisiwa Ndui Zanzibar.
Alisema baada ya kukamilika kwa kurejeshwa fomu hizo kuanzia Julai 2 hadi 8, mwaka huu, wagombea wa nafasi hiyo, wataanza kazi ya kutafuta wadhamini na upande wa muungano anatakiwa kuwa na wadhamini katika mikoa isiyopungua 10 na miwili kati ya hiyo inatakiwa iwe kutoka Unguja na mwingine Pemba.
Msekwa alisema kwa mgombea wa Zanzibar atatakiwa kuwa na wadhamini katika mikoa isiyopungua mitatu, angalau mkoa mmoja kutoka Pemba, lakini hakuna kizuizi kwa wagombea hao, Bara na Visiwani katika kutafuta wagombea katika mikoa yote 26 ya Tanzania.
Msekwa alisema shughuli hiyo ya kuteua jina la kukiwakilisha chama hicho kwa nafasi ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania itafanyika Julai 10 katika mkutano mkuu wa chama hicho na kwa upande wa Rais wa Zanzibar itatangazwa Julai 9, mwaka huu na Halmashauri Kuu yaTaifa.
Alisema watakaogombea udiwani katika kata mpya zaidi ya 700 watachukua fomu kwa makatibu wakuu wa kata za zamani.
CCM haiwezi kuanguka katika uchaguzi mkuu
Alifafanua mto Rufiji, hauwezi kukauka kutokana na mtu au watu wachache kuchota maji yake kwa lengo la kuukausha.
Msekwa alitoa kauli hiyo, kutokana na kuwepo taarifa za baadhi ya wabunge wachache wanaotishia kukihama chama hicho baada ya bunge kuvunjwa.
Msekwa alisema hayo jana akijibu swali aliloulizwa na waandishi wa habari katika mkutano wake na waandishi uliofanyika ofisi ndogo za chama hicho kwa lengo la kutangaza rasmi tarehe ya kuchukua fomu kwa wanachama wa chama hicho wanaotaka kugombea kuteuliwa katika nafasi ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Rais wa Zanzibar na kwamba shughuli hiyo, inatarajiwa kufanyika Juni 21 hadi Julai 1 mwaka huu.
Msekwa alisema chama hicho, hakihofii vitisho hivyo na mbunge yeyote mwenye nia ya kukikimbia chama hicho baada ya bunge kuvunjwa hawezi kusababisha madhara yoyote kwa sababu CCM ina wanachama wa kutosha kukipa ushindi katika chaguzi ujao.
Chama chetu hakitetereki, kama kuna hayo mliyouliza ya kukimbiwa na viongozi wetu, hii ni kwa sababu mwaka 2005 waliondoka watu muhimu kama Njelu Kasaka, lakini hatukutetereka na alirudi kundini na chama kinaendelea kama kawaida, alifafanua Msekwa.
Alisema watu wengi maarufu waliondoka katika chama hicho akiwemo aliyekuwa Naibu Waziri Mkuu, Agustino Mrema na kujipatia maarufu na wanachama wengi, lakini chama hicho hakikuyumba.
Akizungumzia kuhusu wagombea wa nafasi hiyo, Msekwa aliwataka kuwa na busara ya kujichunguza wenyewe kama wanakubalika ndipo waende kuchukua fomu za kugombea kuteuliwa nafasi hizo.
Alisema gharama za fomu hizo ni Sh 1milioni kwa nafasi ya Rais wa Jamhuri ya Muungano na kwamba zitatolewa na kurudishwa kwa katibu mkuu wa chama hicho makao makuu ya chama yaliyopo Dodoma na wale watakaochukua fomu kwa ajili ya nafasi ya Rais kwa Zanzibar wanatakiwa kuchukua na kuzirejesha fomu hizo kwa Naibu Katibu Mkuu, ofisi ya chama hicho zilizopo Kisiwa Ndui Zanzibar.
Alisema baada ya kukamilika kwa kurejeshwa fomu hizo kuanzia Julai 2 hadi 8, mwaka huu, wagombea wa nafasi hiyo, wataanza kazi ya kutafuta wadhamini na upande wa muungano anatakiwa kuwa na wadhamini katika mikoa isiyopungua 10 na miwili kati ya hiyo inatakiwa iwe kutoka Unguja na mwingine Pemba.
Msekwa alisema kwa mgombea wa Zanzibar atatakiwa kuwa na wadhamini katika mikoa isiyopungua mitatu, angalau mkoa mmoja kutoka Pemba, lakini hakuna kizuizi kwa wagombea hao, Bara na Visiwani katika kutafuta wagombea katika mikoa yote 26 ya Tanzania.
Msekwa alisema shughuli hiyo ya kuteua jina la kukiwakilisha chama hicho kwa nafasi ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania itafanyika Julai 10 katika mkutano mkuu wa chama hicho na kwa upande wa Rais wa Zanzibar itatangazwa Julai 9, mwaka huu na Halmashauri Kuu yaTaifa.
Alisema watakaogombea udiwani katika kata mpya zaidi ya 700 watachukua fomu kwa makatibu wakuu wa kata za zamani.
CCM haiwezi kuanguka katika uchaguzi mkuu