Hiki ndicho chama kikongwe barani afrika kinachosimamia haki na utu wa mwafrika.vyama vingi barani afrika vimefata misingi bora ya CCM...wanachama wake wanafata misingi ya kuheshimiana na kupendana...hawajui matusi...hawajui ugomvi....wao wamefundishwa maadili.mara nyingi CCM wanazomewa na vijana wa vyama vya kipinzani kutokana na vyama hivyo kutojengwa ktk misingi ya haki na kuheshimiana....sijawahi kuona chama kinachozomea wanachama wa chama kingine kikadumu ktk duru ya kisiasa.mara nyingi vyama hivyo vimekuwa vikihubiri chuki miongoni mwa wananchi,hivyo wanachama hao kuchukiana na hata kufikia kuuwana.hii si afrika tunayoitaka....hii si afrika ya wastaatabu bali ni afrika ya tabu na mateso yanayosababishwa na viongozi wenye uroho na madaraka huku wakiwatumia vijana kama daraja la wao kufikia malengo yao....waafrika wameingia ktk migogoro ya wao kwa wao....waafrika wanauwana kwa kufadhiriwa na wazungu....wazungu wanahitaji hizi malighafi zetu kwa namna yoyote ile....mfano sudan...utajiri mkubwa wa mafuta...nigeria...libya...algeria....equeterial ...pia wanataka kutugombanisha Tanzania kwa sababu ya Gesi....ndugu wananchi naomba tufanye chaguzi kwa amani na tulinde nchi yetu nzuri.