Keynez
JF-Expert Member
- Feb 12, 2007
- 2,397
- 3,884
Wakuu, nimekuwa nafuatilia mijadala inayoendelea huko Bungeni. Ukisikiliza kwa makini utagundua ni mijadala ambayo ingetakiwa kufanyika ndani ya Chama. Bungeni ni sehemu ya kuongelea mambo yaliyo ya maslahi mapana ya taifa hususani utungaji wa sheria, kurekebisha sheria mbalimbali na kuisimamia serikali.
Najua kuna moto unafukuta huko chini kwa chini kati ya kambi mbili na wanajaribu kuuzima kabla hawajafika katika vikao vya chama ila mimi nasema kutumia rasilimali za nchi hususani taasisi kubwa kama BUNGE kuongelea na kujaribu kutatua tofauti zao siyo jambo sahihi kabisa. Wananchi wengi tu hawana maslahi wala ushabiki na Chama Cha Mapinduzi na wengi tu hawajali hata hiko chama kingejifia leo hii.
Hili linaloendelea halikubaliki!
Najua kuna moto unafukuta huko chini kwa chini kati ya kambi mbili na wanajaribu kuuzima kabla hawajafika katika vikao vya chama ila mimi nasema kutumia rasilimali za nchi hususani taasisi kubwa kama BUNGE kuongelea na kujaribu kutatua tofauti zao siyo jambo sahihi kabisa. Wananchi wengi tu hawana maslahi wala ushabiki na Chama Cha Mapinduzi na wengi tu hawajali hata hiko chama kingejifia leo hii.
Hili linaloendelea halikubaliki!