Pascal Mayalla
Platinum Member
- Sep 22, 2008
- 50,279
- 113,076
Kuna kitu nilikisema hapa kumhusu Fred Mpendazoe leo nimekishuhudia kikitimiaMzee Mwanakijiji, this is my thinking aloud, CCJ ni spare tairi tuu, baada ya kile kitisho cha kumuengua Sitta, ili akienguliwa tuu, yeye na makamanda wake wote na wabunge wengine zaidi ya 100 wangetimka CCM na kuleta upinzani wa kweli.
Taarifa zilifika kwa mkulu, akaamua kukinusuru chama, akamuweka chini Sitta, waka compromise, sasa hakuna tena kitisho cha kumuengua Sitta. Mkulu kakubali kumtosa sahiba wake RA, Sitta akakubali kutoendelea kuisulubu serikali bungeni, ndio maana issue zote hot, akazimaliza kiaina.
Masikini Mpendazoe, hakuijua hiyo compromise na hakuona mbali, akajitoa muhanga ili aonekane shujaa, akatimka mbio kutimkia CCJ, akijiaminisha ndio amefungua njia, kumbe ndio kwanza amekwenda kulitoboa hilo spare tairi na kulitia pancha!. Kama tayari spare tairi inapancha kabla hata ya kuanza kwa safari, hiyo safari itakuwaje?.