CCJ Kulikoni!?


Mzee mwanakijiji,

Hamkujifunza hata vyama vingine vinafanyeje wakati wa kuhakiki majina? Inaelekea mmeenda kichwa kichwa labda mliona mnajua zaidi.

Inabidi mjifunze makosa na mafanikio ya walio watangulieni.

Hapa si ajabu mmefungwa goli na factors mbalimbali zikiwemo za CCM, CUF, CHADEMA, Msajili na wengine.

Mmejianika uchi barabarani na hata waliotaka kujiunga nanyi wanaweza kuficha sura zao.
 

CCJ ilishafanya uhakiki wake na nililiweka hapa.. ndio sababu ya kupeleka yale majina na fomu kwa msajili..

Kuhusu matamshi ya Kyabo.. hata mimi sijafurahishwa na nimewapa ujumbe juu ya hilo.. lakini well.. hisia ni sehemu ya uanadamu na watu wanaruhusiwa kuonesha hisia hili wala sina tatizo nalo kubwa sana. Kwani wanadamu siyo maroboti.
 

kwa kweli watu wanaosubiri pembeni ili mambo mazuri ndio wajiunge hawatufai..
 
kwa kweli watu wanaosubiri pembeni ili mambo mazuri ndio wajiunge hawatufai..

Mzee Mwanakijiji,

Bahati mbaya ukweli ndio huo dunia nzima kwamba watu wengi wanapenda ku support mshindi na sio mshindwa.

Kwanini nipate ugonjwa wa moyo kuunga mkono timu inayofungwa kila siku?

Watu walivyodhani Mrema anaweza kuwa mshindi mwaka 1995 walimwunga mkono kwa wingi. Sasa wote wamekimbia maana wanaona ni looser tu.

CCJ mmefulia kwa hili kama mlivyofulia mlivyoenda kulia kwenye kaburi la baba wa taifa.
 

Pole sana kaka Mwanakijiji, ndio siasa, kaza buti maana hata Mandela alikaza buti miaka mingi sana.
 

Zitto;
Siku zote nilipokuwa nikisoma watu wanakushambulia nilikuwa najua kuwa ni watu wasiotakia mema nchi yetu. Il leo nimeamini kuwa wewe ni Hoax, yaani si mpinzani wa kweli. Mifano yako yoote inaonesha umeishawekwa sawa na CCM. Haiingii akilini hata kidogo kusema TEMEKE na TUNDURU ni ngome za CUF wakati sehemu hizo zilichagua wabunge kutoka CCM. Kwa nini usiseme CCJ waliingizwa kwenye mtego na wana-CCM ambao ndicho chama pekee mpaka saa ambacho viongozi wake wamesema hadharani kuwa CCJ haitashiriki uchaguzi mwaka huu?. Je Tendwa yupo CUF?, Philip Marmo yupo CUF?, Pius Msekwa yupo CUF?. Ninachokiona hapa bwana Zitto ni kwamba umekubali kuingia katika ngoma ambayo inapigwa na CCM ya kuwagawa wapinzani ili wao wawatawale. Zitto umeahidiwa kuwa CCM hawata kuhujumu uchaguzi jimboni kwako ili usiwaguse wakati wao wanawashughulikia wengine?.

Sijakuelewa kabisa mbunge kwenye hili na umenikatisha tamaa kabisa, CCJ, CUF si adui wa vyama vya upinzani vyenzake bali ni adui wa chama tawala kama ilivyo CHADEMA. Wivu huu wa vyama pinzani kwa CCJ na kwa vyenyewe kwa vyenyewe ndiyo utafanya wananchi kama sisi ambao hatuangalii chama bali maslahi ya Taifa na maendeleo kukata tamaa kabisa na ninyi na kuona ni bora tuangalie katika kuifanya CCM iwe safi na kuendelea kutawala mpaka Massiah atakaporudi. There's no point ya kuwa na watu kama Zitto ambao slowly wanakuwa erroded na corrupt system na kujisahau kuwa Umoja ni nguvu, unganeni mtupe hope watanzania. It's a sad day for me to read a post with CCM leaning strategy from Someone like you.
 
CCJ ilishafanya uhakiki wake na nililiweka hapa.. ndio sababu ya kupeleka yale majina na fomu kwa msajili..

......


You know what, i wish ungeona kwa macho yaliyokuwa yanatokea. Hata ingekuwa wewe msajili wa vyama usingekubaliana nao.


Okay, walishafanya uhakiki. Je walitumia similar method na anayotumia msajili wa vyama?

Pili, kuanza kulialia na hujuma toka CCM bila kutoa ushahidi/vielelezo ni dalili kubwa sana ya kutojiamini, kutokuwa na uhakika, kutokuelewa nini kinatokea na kinaendelea. Kwa nini hawakuzuia hiyo hali isitokee kama walijua hujuma na hila zingetokea? Hii yote ni kukosa umakini na ujuzi pamoja na uzoefu.
 

Mbona umekasirika hivyo Mkuu?na je nyie wenyewe CCJ mliuliza kwamba Msajili kapata wapi pesa?nakumbuka mimi niliuliza swali hili kwamba amekopa wapi?mbona mlikubali haraka kahikiwa wakati malikuwa hajajipanga vya kutosha?usilie ndio siasa za tz na wenzako tukiwa tunasema hali ni ngumu kwa upinzani kupenya yaani ni rahisi kwa ngamia kupenya kwenye tundu la sindano kuliko upinzani kupata ushindani sawa wa kisiasa wewe ulikuwa unaona kama vyama vingine voye vimelala havijafanya kazi,nadhani unaanza kuuona utamu wa ngoma,na bado huu ni mwanzo tu.mizengwe kila kona!siasa tz ni ngumu ni heri hata kulima...
 


Msianze kuingiza siasa zenu hata kwenye scientific truth. Anayoyasema Zitto ni ukweli na ukweli mtupu. Utaona Zitto ni hoax kwenye hili kwa vile unataka afinyange ukweli na kuimba pambio la kuisifu CCJ hata kama imechemsha, eti kwa vile tu naye ni mpinzani wa CCM.

Hofst, hatuendi hivyo siku hizi.
 

Hofstede,

Mbona Zitto kaandika ukweli mtupu?

Unataka kwasababu Zitto yuko CHADEMA basi hata pale penye ukweli, yeye awe ana SPIN tu?

Hofstede nilifikiri ni real kumbe na wewe bomu. Unamtolea Zitto mimacho kwasababu tu hajawatukana CCM? Kazi ipo kweli TZ!
 

Brother, ama upo misinformed au deadly wrong. Here CCJ is the problem. They must be smarter and smarter.

Hebu niambie kwa nini Kiyabo hakuwa na kadi yake? Kweli hakuweza hata kupata ushauri kwa wazoefu pale Ufipa street CHADEMA? Ofisi za CCJ na CHADEMA zipo karibu kabisa. Ofisi za CCJ na UDP zipo karibu kabisa, wangeuliza hata.

Tatizo ni CCJ. with media coverage, with support ya watu kama MwanaKijiji walijiona wao ndio upinzani na upinzani ndio wao. Hata kama watu wanadhani upinzani wa sasa ulikosea mahala fulani, lakini historia ni funzo nzuri sana. Kuna watu walisajili vyama wakati ambao CCM ilikuwa na nguvu kweli kweli na wakavuka viunzi. CCJ wajifunze kwao.

Nilisoma Katiba ya CCJ, inaeleza imani yangu ya kisiasa kabisa ie Social democracy. Nilikutana mara kwa mara na Mwenyekiti wa CCJ. Nilizungumza na Mpendazoe.

CCJ ndio tatizo. Wajirekebishe
 

You are right kama wewe ni msemaji wa Muheshimiwa Zitto. Ukweli utabaki palepale huyu jamaa ni Hoax, nimegundua leo kutokana na post yake. Na sitashangaa ama akahamia CCM au akapewa cheo cha ahsante serikalini baada ya uchaguzi.
 

Hujanielewa na kwa kuwa umeshahukumu wala siakusaidia kuelewa. Hapa nimeonesha jinsi vyama makini kama CUF vinavyolinda ngome zao. Niseme tu kuwa, to me CCJ was a threat to CHADEMA and other opposition parties. I better get rid of it. We dont need an emerging party every new election. We need existing parties to consolidate. To me i go for CHADEMA, CUF and NCCR-M and the civil society. New parties? i dont have that luxury
 
You are right kama wewe ni msemaji wa Muheshimiwa Zitto. Ukweli utabaki palepale huyu jamaa ni Hoax, nimegundua leo kutokana na post yake. Na sitashangaa ama akahamia CCM au akapewa cheo cha ahsante serikalini baada ya uchaguzi.

Expected this as you are a hero you BASH Zitto on JF!

For your information i was to be a Minister in February 2008. I have always strived for change and not positions. Wewe endelea kuota na time will tell
 

Utakuwa unalako jambo tu,si bure huwezi kuandika kwa jazba kiasi hiki..Kila mtu ana maoni yake humu sio lazima wote tufanane misimamo,tambua hilo!
 
Expected this as you are a hero you BASH Zitto on JF!

For your information i was to be a Minister in February 2008. I have always strived for change and not positions. Wewe endelea kuota na time will tell

Zitto wala usihangaike naye huyo,ana lake jambo unapoteza muda na nguvu yako bure,utakasirika bure,,Mpotezee!
 
Inawezekana kabisa ipo mikono ya CUF, CCM ............ Lakini jambo la msingi ni ukweli ulio bayana kwamba hata hao viongozi wa CCJ ni wababaishaji wakubwa.

Tanzania ina vyama karibu ishirini vilivyosajiliwa. Hivi hao viongozi wa CCJ walishindwa kujua mahitaji halisi ya uhakiki toka kwa msajili? Viongozi wa chama wameshindwaje kuwa na hata leja ya wanachama wao, kama wanasema alichokuwa nacho msajili sio sahihi?

Badala ya kuandaa wanachama wao kwa ajili ya uhakiki, waliishia kutumia muda mwingi kuongea na waandashi wa habari, matokeo yake kadi ya Asha Bakari anakuja nayo Hamisi Athmani! Taarifa zinaonyesha kwamba hiyo jana walikuwa wanaendelea kuuza kadi na kutaka nao wahakikiwe hapo hapo!

Jamani, tumaomba mtu mwenye CV za hawa wababaishaji atuwekee hapa. Huwezi kuendesha chama kama kikundi cha ngoma ya mdumange.
 
Mkuu Zitto hapa mie ndio wapinzani wanaponishangaza,kama mnajua jimbo fulani kuna chama cha upinzani tayari kina nguvu kwanini msiki support hicho chama badala yake na nyie au vyama vingine vya upinzani navyo vinaenda kusimamisha mgombea? inama hakuna anayejua kwamba atakae faidika ni ccm siku ya uchaguzi?
 
Ni Kweli kaka nasikia hata Mwenyekiti wao naye alipewa 20,000,000 asijipe kadi na Katibu Mkuu akapewa donge nono na ahadi kemkem asijiorodheshe kwenye fomu za Wanachama

sasa hapo wanamkomoa nani?


ukweli halisi hakuna chama cha upinzani chenye nia ya kuigomboa nchi yetu kutoka mikononi mwa CCM,wote wapo kwa maslahi yao binafsi na ndio maana imekuwa vigumu sana wapinzani kuungana japo kuwa lengolilitakiwa liwe moja.
 
Expected this as you are a hero you BASH Zitto on JF!

For your information i was to be a Minister in February 2008. I have always strived for change and not positions. Wewe endelea kuota na time will tell

Hon. Zitto, respect!
I am not as simple minded as you think, bashing Zitto so what?. I will always be on the side of serious positive minded people who are pro bono regardless of whether they are in Chadema, CCM, CCJ, CUF et al. But when it comes into a person of your caliber trying to torpido the smear to a party which does not have any power to register a political party, without any substantive evidence; it simply doesn't make sense and a heartbreaking. Circumstantial evidence via their statements shows that, this is a deliberate attempt by CCM to block CCJ from particiapting in GE. How will CUF benefit by the refusal of CCJ being permanently registered?. This is unfortunate, but if CCM invited you to join their gov in 2008 and refused, I hope you will also refuse to help them knowingly or unknowingly blocking the CCJ participation into GE.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…