VUTA-NKUVUTE
JF-Expert Member
- Nov 25, 2010
- 6,140
- 18,004
Nilipowasili tu jana usiku kutoka Arusha-kwa-Lema nikatamani kujua yaliyoendelea Kisiwandui, Zanzibar. Huko kulifanyika kikao cha Kamati Kuu ya CCM kilichofanya tathmini ya mambo kadha wa kadha yahusuyo chama.
Iliripotiwa kuwa ajenda ya wagombea urais ilikuwa moto na kumeafikiwa mambo magumu na mazito juu ya baadhi yao au wote. Nikataka kujua ukweli. Nikawasiliana na Mjumbe mmoja wa CC aliyekuwepo Kisiwandui.
Alichosema ni kuwa hakukuwa na jipya. Yamejadiliwa mambo ya kawaida sana ya kichama. Hata Ripoti ya Kamati ya Komredi Mangula iliwafagilia wagombea watarajiwa kwa kusema wamerekebishika na sasa wako safi.
Uchaguzi wa Serikali za Mitaa na maandalizi ya uchaguzi ujao yaliteka sana kikao husika. Wakati wa kuwajadili wagombea mbalimbali chamani,wajumbe waligawanyika na kila mchangiaji alimfagilia wa kwake.
"Hakukuwa na jipya ndugu yangu. Nikirudi tutaongea vizuri"nikaambiwa na kuahidiwa na mjumbe huyo wa CC.
Mambo yanakaribia patamu!
Mzee Tupatupa wa Lumumba,Dar es Salaam
Iliripotiwa kuwa ajenda ya wagombea urais ilikuwa moto na kumeafikiwa mambo magumu na mazito juu ya baadhi yao au wote. Nikataka kujua ukweli. Nikawasiliana na Mjumbe mmoja wa CC aliyekuwepo Kisiwandui.
Alichosema ni kuwa hakukuwa na jipya. Yamejadiliwa mambo ya kawaida sana ya kichama. Hata Ripoti ya Kamati ya Komredi Mangula iliwafagilia wagombea watarajiwa kwa kusema wamerekebishika na sasa wako safi.
Uchaguzi wa Serikali za Mitaa na maandalizi ya uchaguzi ujao yaliteka sana kikao husika. Wakati wa kuwajadili wagombea mbalimbali chamani,wajumbe waligawanyika na kila mchangiaji alimfagilia wa kwake.
"Hakukuwa na jipya ndugu yangu. Nikirudi tutaongea vizuri"nikaambiwa na kuahidiwa na mjumbe huyo wa CC.
Mambo yanakaribia patamu!
Mzee Tupatupa wa Lumumba,Dar es Salaam