vyuku
JF-Expert Member
- Mar 30, 2012
- 503
- 87
Mbunge wa viti maalum mkoa wa Arusha mh Catherine Magige ameendelea na ziara yake ya kikazi leo wilayani Monduli. Akiwa kata ya mto wa mbu mbunge alikutana na baraza kuu la UWT wilaya monduli pamoja na wataalam(wakuu wa idara). Mh mbunge alifuatana na katibu wa UWT mkoa wa Arusha Irimina Mushongi pamoja na mjumbe wa baraza kuu la UWT Taifa anawakilisha mkoa wa Arusha ndg Agness Martin. Kama kawaida yake mh mbunge alisikiliza kero na changamoto mbali mbali kutoka kata mbali mbali za wilaya monduli. Mh mbunge aliwaomba wataalam kujibu kero hizo na yeye kuzichukua zingine ili zifanyiwe kazi na mamlaka husika. Mh mbunge pia aliwasihi wanawake kushiriki na kugombea nafasi mbali mbali ktk uchaguzi ujao wa serikali za mitaa mwaka huu. Mh mbunge pia alichangia miradi ya UWT wilaya monduli kwa kutoa mashine ya kusaga na kukoboa yenye thamani ya 3,500,000/- pamoja na viti 100 vyenye thamani Tsh 1,600,000/-
Na kila mjumbe kumpatia sh elfu 20.
Mh Catherine pia aliwapatia wanawake hao vitenge kama sare ya CCM. Kesho ziara hiyo itaendelea wilayani karatu. Hapa kazi tu.
Na kila mjumbe kumpatia sh elfu 20.
Mh Catherine pia aliwapatia wanawake hao vitenge kama sare ya CCM. Kesho ziara hiyo itaendelea wilayani karatu. Hapa kazi tu.