CAG mstaafu ashangaa kesi ya Idd Simba ya fedha za UDA kufutwa

CAG mstaafu ashangaa kesi ya Idd Simba ya fedha za UDA kufutwa

Hivi tuna uwezo wa kulirudisha kwa u moja wetu ?
Ni changamoto, ila tukinyamaza bila kulisemea jamaa wanalikwapua. Lipo kimtegomtego kwa hawa wajanja hivi wanawasikilizia mkikaa kimya wanalikwapua, ni vema ikawekwa wazi mchakato mzima uliofanyika katika kulikwapua kiujanjajanza. Nikisema kiujanja ni maana taratibi zilizotumika zinatia mashaka sana, na si ajabu mwisho wa siku ikaonekana bado lipo serikalini.
 
Taffman said:
Kuna watu humu ndani kz yao ni kumtukana tu jk,hv kiukweli kbs,yaani kiroho safi jk hana mazuri completely ktk jamhuri hii ya muungano wa Tz?
mie ninaamini jk kafanya makubwa ya maana kuliko rais yyt yule ktk nchi hii ktk sekta zote za uchumi,jamii,kisiasa etc
Ikumbukwe pia jk ni binadamu km tulivyo sisi,kila mmoja ana mapungufu yk km binadamu,no body is perfect,tusilaumu tu na kutukana,tuangalie pia ufisadi na wizi ulikuwa kwa kikwete tu?wizi ulianza sk nyingi sana,watu wamekwiba vya kutosha,si ccm wala cdm wengi wetu ni wezi,wengi hatuna uzalendo na wala hakuna msafi nchi hii,yyt yule ktk sisi hata ikitokea amepata nafasi ktk nchi hii atajiangalia yy kwanza na familia yk,ndivyo tulivyo na huo ndo ukweli
Wewe mzima kweli kichwani? Mtu aliyepewa dhamana anageuka kuwa jizi badala ya kakasirika unaleta ngojea, angalia Ufaransa na hata Israel marais wastaafu wamepelekwa mahakamani kwa makosa mbali mbali yanayohusu rushwa na matumizi mabaya ya madaraka.

Unawaingiza CDM kuwa nao wezi ni lini walipewa nafasi ya kuongoza nchi? Juha wahed
 
Ngoja Meya wa Jiji (UKAWA) amalize kuyapitia mafaili ya UDA. Naona kuna agenda ya kuwa.outsmart UKAWA kwa kumpa jukumu hilo JPM ambaye alikuwa kimya muda wote kuhusu UDA

Watu wengine bwana wao ajenda yao ni mashindano ya kitoto na wala si kupata suluhisho la matatizo.Kwao wao suluhisho sio ishu, ila ishu kwao nani katoa suluhisho, duuh, mahabat kweli uwendawazimu
 
Wewe mzima kweli kichwani? Mtu aliyepewa dhamana anageuka kuwa jizi badala ya kakasirika unaleta ngojea, angalia Ufaransa na hata Israel marais wastaafu wamepelekwa mahakamani kwa makosa mbali mbali yanayohusu rushwa na matumizi mabaya ya madaraka.

Unawaingiza CDM kuwa nao wezi ni lini walipewa nafasi ya kuongoza nchi? Juha wahed

Mwizi kumjua kwani mpaka apewe nchi? Watu wanaiba posho za safari kwa kujifanya wamekwenda lakini hawajaenda na hapo hawajapewa nchi, watu wanajifanya kukataa shangingi la serikali na kupigia kelele matumizi mabaya kisha anazunguka uani analichukua. Wewe kwani huoni. Mwizi, mwizi tu ajiunge ccm, ajiunge CDM wote wezi tu. Kuwa CDM hakumuondolei mwizi sifa yake la sivyo mtamfanya mzee wa vijisenti nae ahamiehuko kama kuna bafu linalotakatisha namna hiyo
 
Iddi Simba fisadi mkubwa sana,mbona hawaizungumzii kampuni ya fedha ya PRIDE?
 
Watu wengine bwana wao ajenda yao ni mashindano ya kitoto na wala si kupata suluhisho la matatizo.Kwao wao suluhisho sio ishu, ila ishu kwao nani katoa suluhisho, duuh, mahabat kweli uwendawazimu
Unaweza ukawaaminisha watu kuwa unatoa suluhisho kumbe lengo ni kuhodhi mchakato ili kuwalinda baadhi ya watu. Mara ngapi tumeambiwa kuwa "suala hilo lisijadiliwe, lipo mahakamani"?
 
Nasikia file lake limepitiwa upya na pcccb na mu wowote kesi ile inaanza upya! Hawezi kuruka ile kesi nzito sana lazi ianze upya
 
Hivi tuna uwezo wa kulirudisha kwa u moja wetu ?

inawezekana endapo kama taratibu za sheria zilikiukwa na kulikuwepo na vitendo vya rushwa, wizi, mgongano wa kimaslahi.

na hayo yatawezekana kujulikana ikiwa mkataba wa uda utapitiwa upya...
 
Unaweza ukawaaminisha watu kuwa unatoa suluhisho kumbe lengo ni kuhodhi mchakato ili kuwalinda baadhi ya watu. Mara ngapi tumeambiwa kuwa "suala hilo lisijadiliwe, lipo mahakamani"?

Nazungumzia suluhisho kwa maana ya suluhisho. Mawazo kinzani yanapelekea suluhisho la mambo mengi kupatikana na hii ndio faida ya mawazo kinzani, suluhisho! Kwangu ni suluhisho and not any other unnecessary speculations. maendeleo hayana vyama wala ideology, jenga barabara, lete maji, yeyote aletae nitatumia pasi kujali yametoka CUF au Jahazi asili.
 
inawezekana endapo kama taratibu za sheria zilikiukwa na kulikuwepo na vitendo vya rushwa, wizi, mgongano wa kimaslahi.

na hayo yatawezekana kujulikana ikiwa mkataba wa uda utapitiwa upya...
Ni wakati muafaka mzee Magu akaanza kujifua Kwa hili na akijumlisha Nyumba zetu za umma SI mbaya . Ila nadhani anaweza bado akawa anampa heshima mzee wa msoga akishapewa uenyekiti anaweza fanya zaidi
 
Ni changamoto, ila tukinyamaza bila kulisemea jamaa wanalikwapua. Lipo kimtegomtego kwa hawa wajanja hivi wanawasikilizia mkikaa kimya wanalikwapua, ni vema ikawekwa wazi mchakato mzima uliofanyika katika kulikwapua kiujanjajanza. Nikisema kiujanja ni maana taratibi zilizotumika zinatia mashaka sana, na si ajabu mwisho wa siku ikaonekana bado lipo serikalini.
Tushauriane hapa wananchi wa kawaida tufanyeje ? Kwa u moja wetu tufanye kila linalowezekana kufanyika ili wawakilishi wetu watusikie ni vibaya Sana Kuwa Na jamii passive na sisi tulio na viunganishi kama hivi tufanye upande wetu ili mali hizi za umma zitasaidia wote si hao matapeli wasio na huruma
 
Ni dhahiri hawa watendaji wakuu wa Serikali Awamu ya 4 walikuwa wanayashangaa maamuzi ya Serikali.

Hayo yamethibitisha na alikuwa CAG mstaafu Mzee Utouh alipohojiwa jana na kuonekana kwenye magazeti ya Leo kuwa kati ya mambo ambayo yalimshangaza na kufanywa na viongozi wa Serikali ya Mh. Kikwete ni pamoja na suala la uuzwaji wa Shirika la UDA na fedha zake kuwekwa kwenye Akaunti ya mtu binafsi Bw. Idd Simba kitendo ambacho ni kosa na kushtakiwa katika Mahakama ya Kisutu lakini katika hali ya kushangaza na kulindana kesi hiyo ilifutwa na ndicho kinachomshangaza CAG Mstaafu.

UDA in Mali ya Umma tunamwomba Mh. Rais Magufuli apitie ripoti ya CAG ya Uuzwaji wa UDA ayaone madudu. Pia naiomba PCCB ipitie upya mchakato wa uuzwaji wa UDA ijionee jinsi watu wachache walivyolila Shirima la UDA Na fedha kuwekewa kwenye akaunti zao binafsi.
Where is the long arm of the law?
 
Ni kweli JK hakuwa mwendesha mashtaka lakini lazima uelewe nguvu za Rais kwenye nchi kama TZ, jamaa alimuuzia au kumgawia UDA yule dogo na huyo Simba aliamuru aachiliwe na ikawa hivyo. Au umesahau nilichoandika kimeandikwa!!!! Si hayo tu jamaa amechomeka sana namuonea huruma JPM sijui atafanya mangapi sababu atakuwa anasafisha uchafu uliopita, kutumbua majipu n.k., na je kazi zake atafanya saa ngapi? Na huyu CAG wa zamani tena ni rafiki yangu wa zamani si alete hayo makabrasha ya UDA hapa JF sisi raia tunaweza kufungua kesi mahakamani au anaogopa ataambiwa ameiba nyaraka za serikali? Hakuna kisichowezekana duniani.
 
Mahakama ya ufisadi ianze mapema kwakuwa kesi ziko nyingi tu huku mtaani.
 
Back
Top Bottom