CAG: Magufuli na Mwakyembe wawajibishwe

CAG: Magufuli na Mwakyembe wawajibishwe

Shondola

Member
Joined
Apr 2, 2014
Posts
95
Reaction score
58
Kila kunapokucha Taifa letu linaendelea kuingia katika giza tororo hasa kutokana na baadhi wa wale walioaminiwa na Raisi kuhakikisha kuwa wanaendelea kuziacha Wizara zikiwa hoi kutokana na Ufisaidi wa kutisha.

Kabla hata swala la Escrow halija futika katika mioyo na fikra za Watanzania jambo ambalo limepelekea baadhi ya Mawaziri kuwajibishwa sasa limeibuka lingine kubwa na la aibu.

Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Serikali amependekeza hatua stahiki zichukuliwe dhidi ya Dkt. John Pombe Magufuli (Waziri wa Ujenzi) na Dkt. Harrison Mwakyembe (aliyekuwa Naibu Waziri) kutokana na Ufisaidi unaofikia kiasi cha Shilingi Bilioni 256.

Hoja hii ilishawahi kuibuliwa Bungeni ila kama kawaida yake Magufuli aliizima kiujanja ujanja jambo ambalo sasa limeibuka upya na CAG kujiridhisha kuwa majibu waliyoyatoa Waziri hayakiwa na usahihi wowote hivyo alilidanganya Bunge na fedha hizo hazijulikani zilikopelekwa kwa kuwa hakukuwa na barabara mpya zilizojengwa na kama haitoshi madeni ambayo Magufuli alisema yamelipwa hayaendani ama kulingana na kiasi hicho cha zaidi ya Bilioni 256.

Akizungumza na Gazeti la Mwananchi Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya PAC Mhe. Zitto Zuberi Kabwe amesema huwa ana mashaka sana na majibu ya Magufuli manake kujiamini kwake hupelekea watu wengi kumwani hivyo hata anapofanya mambo ya hovyo watu hucheka na kumpigia magofi.... Hivyo yale majibu aliyoyatoa Bungeni kipindi kile hakuyaamini na kuamua kuendelea kulifuatilia jambo ambalo sasa limeibua ukweli kwamba Magufuli alilidanganya Bunge na hili halivumiliki hata kidogo lazma hawa mabwana sasa wakatujibu Bungeni na wajiandae kuwafuata wenzao kwa kuwajibika.

Itakumbukwa kuwa Magufuli amekuwa akitunukiwa jina la "The Chosen" kwamba ndiye anayetakiwa kumrithi JK baadhi ya watu wakisema kwamba huyu bwana ni msafi kumbe ndo yale yale waliwahi kuyasema wahenga Usilolijua ni kama usiku wa kiza........

Kama ilivyokuwa kwa Escrow sasa hili nalo Watanzania wanalisubiri kwa hamu kubwa.

Chanzo: Mwananchi

 
Huyu jmaa wizi wake wa akili sana kweli yawezekana ameiba lkn ni mpiganaji sana kma anyosema zitto kujiamini kwake uwezi kujua kma fisadi lzm na yeye amfate muhongo
 
Huyo magufuli ndiye mwenye afadhari huko ccm na mkianza tena kwa huyo ccm watajuta mwaka huu.
ZZK wa siku hizi mmmhhh,hapo yeye kamaliza kazi yake
 
Maghufuli hachafuliki kirahisi hivi, wewe mleta mada , Gazeti la Mwananchi na huyo fisadi kupitia Leka Dutigite jipangeni upya
 
Huyu jmaa wizi wake wa akili sana kweli yawezekana ameiba lkn ni mpiganaji sana kma anyosema zitto kujiamini kwake uwezi kujua kma fisadi lzm na yeye amfate muhongo
Hahaaa, mmechelewa sana
 
Huyo magufuli ndiye mwenye afadhari huko ccm na mkianza tena kwa huyo ccm watajuta mwaka huu.
ZZK wa siku hizi mmmhhh,hapo yeye kamaliza kazi yake
Zitto naye ni mtu wa kujificha kwa wenzie, Ngelejakamtingisha kidogo tu juzi ameibukia kwa Maghufuli? Maghufuli tunaye na tutasonga naye mbele.
 
Si kila data ni geinuine,
Ndo maana kuna kufanya verification ili ku-determine ukweli wa data hizo!
Maghufuli hata kama kweli angwkuwa ameiba tofauti wanavyomsongizia bado kura za watanzania atazizoa endapo ataamua kugombea
 
Alishapewa nafasi hiyo ya kumwaga hizo data ila kaishia kutema uongo na porojo tuu!!! Data gani nyingine ataleta?ama kwanza atakiri kuwa zile za awali zilikuwa za uongo?
Cc Ruttashobolwa
Semeni yote ila kwa Maghufuli wananchi watawapigeni mawe. MAGHUFULI ni lulu. Hayo anayozushiwa ni saw kwa binadamu yeyote kama ilivyo kwa ZITTO na Leka Dutigite.
 
msikilizeni C.A.G jamani zito hawezi ongea lolote kuhusu hesabu bila idhin ya C.A.G
 
Tatizo la watanzania wengi wanaishi kwa ushabiki na kudanganywa na mbwembwe za kipuuzi... kama atagombea urais ataishia kuambulia kura za vichwa maji, sija wahi kumuelewa huyu jamaa, na kujiona anajua kila kitu kumbe ni kama kima wengine
 
Semeni yote ila kwa Maghufuli wananchi watawapigeni mawe. MAGHUFULI ni lulu. Hayo anayozushiwa ni saw kwa binadamu yeyote kama ilivyo kwa ZITTO na Leka Dutigite.
Unazungumzia ya leo tu!! Huyajui ya kesho,hata prof muhongo tulimwamini sana tu usiku,ila kulipokucha tukajisahihisha na matokeo yake umeyaona!!tuhuma moja tu ya maana itamfanya huyo "wakwenu"arushiwe mawe popote atapopita.
 
Back
Top Bottom