BVR ni Ufisadi mtupu - Dr Slaa

Molemo

JF-Expert Member
Sep 24, 2010
14,534
13,225
Katibu mkuu wa CHADEMA Dr Wilbroad Slaa amelaani na kupinga vikali zoezi linaloendelea la uandikishaji wapiga kura kwa njia ya BVR.

Kiongozi huyo tishio kubwa kwa utawala wa CCM amesema alichojifunza akiwa nchini Marekani ni kwamba mbali ya Taifa hilo kuwa na teknolojia ya hali ya juu lakini hawatumii kitu kinachoitwa BVR

Dr Slaa amesema kuthibitisha ufisadi huo wa BVR hakuna uwazi uliofanyika kutoa tenda ya manunuzi ya vifaa hivyo.Ni wizi mtupu amesema kiongozi huyo.

Kiongozi huyo aliyekuwa Marekani kwa ziara ya siku 10 ameyasema hayo mbele ya waandishi wa habari na wanachama walioenda kumlaki uwanja wa ndege wa Dar es Salaam.

Wananchi kadhaa waliienda kumlaki walikuwa na mabango kadhaa hasa yale ya kumtambua kama Rais wa awamu ya Tano.

===================
 
Raisi wa awamu ya tano ameliona hili na ni kweli kabisa maana kinachofanyika kwa sasa na tume ni usanii tupu,mashine chache ili uchaguzi uahilishwe kwa manufaa ya ccm.
 
Rais wangu wa Nov 1 .......... 2015 , karibu nyumbani.... huku kuna wasaliti wako mbio kweli.....Wanadhani kujenga chama kunachukuwa miezi 6 tu....naomba uwape somo
 
Hapo mwanzo watawala walisema vitambulisho vya Uraia vitatumika kupiga kura..hii njiii ni ngumu
 
Rais wa moyoni kasema kweli kwani tangi waanze kuandikisha ni matatizo kibao na hakuna hata moja lililo patiwa ufumbuzi ni usanii mtupu
 

Kumcounter Dr. Slaa ujipange kweli kweli hili la BVR na Zimetoka China ni fukuto lingine ngoja tuone
 
Ajabu sana mpaka muda huu mapepo ya Lumumba hayajacharuka? Maana wakisikia jina la Dr Slaa mashetani ya kiccm na kikwao yanaanza kuchapana ngumi...!!!!!

Anyway hiyo ya Bvr Kiukweli ni maasi yajayo, kuna siri nzito iliyonyuma ya hiyo Makitu..!!

Kuna karenda iliyochapwa na Gazeti la Mwananchi ikionyesha Wakenya walitumia
13.000 kuandikisha wapiga kura 14.000.000ml kwa kipindi cha miaka mitatu...!! Wakati kule Nigeria walitumia Bvr 130.000 kuandikisha wapiga kura 40.000.000ml kama sijasahau kwa kipindi cha miaka minne...!!! Then sisi eti mpaka sasa tuna Bvr 250 plus 1.200 zinazokuja tukitaka kuandikisha wapiga kura 20.000.000 kwa kipindi cha Miezi minne..!!!!

Haya ni maajabu na kwakweli Mungu tu atusaidie Kwakweli Tanzania inakwenda kuandika historia ya machafuko makali kwa kuwahi kitokea kwasababu ya uroho wa madaraka wa watu wachache. Hili jambo linafanyika kana kwamba tulikuwa hatujui uchaguzi utafanyika lini, wakati jambo hili lipo kikatiba.

Ccm hii Ccm hiii....!!!!

BACK TANGANYIKA
 

Dr Slaa katufumbua macho leo.
 
mpaka aende marekani kwanza na kisha kuja na hayo majibu si angesema wakati zikinunuliwa hii nakumbuka kuwa siasa za slaa ni kupinga kila jambo kama ilivyokuwa kipindi cha marekani na uchina.
 
Ndiyo maana unasikia zitaletwa kwa mafungu na eti ndege ya kukodi.This is ridiculous,ullishawahi hata sikia serikali imekodi ndege kuleta dawa nchini kwa kuwa pametokea uhaba na watu wanakufa?Then why this rubish BVR?I too smell something fishy at NEC
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…