Mwanajamii
JF-Expert Member
- Mar 5, 2008
- 7,063
- 68
Mama Porojo,
Punguza porojo zako. Butiku alikuwa Private Secretary wa Mwalimu mpaka Mwalimu anaondoka mamlakani. Mwinyi akamwomba amsaidie pale Ikulu wakati alipoingia na Butiku amekaa na Mwinyi kwa miaka miwili kama Private Secretary wake. Baadaa ya hapo kwa sababu Mwalimu alikuwa anapata wageni wengi pale Butiama akamwomba Mwinyi amruhusu Butiku kuwa mkuu wa mkoa wa Mara pale Musoma ili aweze kumsaidia Mwalimu na wageni wake wanapokwenda kumtembelea Butiama. Butiku alikuwa mkuu wa mkoa mpaka pale Mwalimu alipoanzisha Nyerere Foundation akamchukua kumsaidia pale. Aliyemteua Butiku kuwa mkuu wa mkoa Mara ni Mwinyi na wala si Mwalimu.
Ni Butiku ndio aliefilisi mfuko wa mwalim Nyerere Foundation,amekula pesa za wafadhili waliokuwa wanatoa kuuendeleza mfuko huo sasa anatafuta huruma ya watanzania.kama kweli alikuwa mzalendo sana,ameifanyia nini tanzania kwa nafasi alizowahi kushika ikiwamo hiyo ya ukuu wa mkoa.mwizi tu huyo.