PreGE2025 Butiama: Mbunge Sagini achinja ng'ombe 500 kutoka uturuki na kugawia wananchi sikukuu ya ‘Eid al-Adha’

PreGE2025 Butiama: Mbunge Sagini achinja ng'ombe 500 kutoka uturuki na kugawia wananchi sikukuu ya ‘Eid al-Adha’

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla)

Just Pray

JF-Expert Member
Joined
Nov 7, 2023
Posts
2,142
Reaction score
4,779
Wakuu

Wananchi wa Wilaya ya Butiama mkoani Mara wamejikuta wakinusuru fedha zao kwaajili ya bajeti ya kitoweo cha sherehe ya sikukuu ya kuchinja ‘Eid al-Adha’ baada ya Mbunge wa Jimbo la Butiama Jumanne Sagini kuchinja Ng’ombe zaidi 500 na kuwagawia.

Tukio hilo limetokea mapema leo Juni 7, 2025 hatua inayotajwa kuwawezesha wananchi hao bila kujali dini zao wanaungana na wenzao ulimwenguni kusherehekea Eid.

Akizungumzia tukio hilo lililoandaliwa nyumbani kwa Mbunge wa Jimbo la Butiama kwa niaba ya mbunge huyo, Ofesa Mahusiano kutoka ofisi ya Mbunge, Japheth Changalawe amesema Ng’ombe hao 500 wametolewa na marafiki zake kutoka nchini Uturuki.

Amesema hatua hiyo ni ishara ya mshikamano baina yake na marafiki wa nje, viongozi na wananchi na kunaonesha namna tunavyothamini ibada, amani na undugu katika jamii.

Aidha, amesema Ng’ombe hao wamegawanywa kwenye vitongoji 370 na taasisi zote za umma na binafsi zilizopo katika jimbo hilo, kwa ajili ya kitoweo kwa wananchi kipindi hiki cha kusherehekea Sikukuu ya Eid Al-Adha.

Screenshot 2025-06-07 160108.png

Ugawaji wa sadaka hiyo umefanyika kwa siku mbili mfululizo kuanzia jana na leo, kwa kile kinachodaiwa kuwa ni kuonesha moyo
1749301681660.png
wa upendo na mshikamano wa Mbunge Sagini kwa wananchi wa jimbo hilo.
 
Wakuu

Wananchi wa Wilaya ya Butiama mkoani Mara wamejikuta wakinusuru fedha zao kwaajili ya bajeti ya kitoweo cha sherehe ya sikukuu ya kuchinja ‘Eid al-Adha’ baada ya Mbunge wa Jimbo la Butiama Jumanne Sagini kuchinja Ng’ombe zaidi 500 na kuwagawia.

Tukio hilo limetokea mapema leo Juni 7, 2025 hatua inayotajwa kuwawezesha wananchi hao bila kujali dini zao wanaungana na wenzao ulimwenguni kusherehekea Eid.

Akizungumzia tukio hilo lililoandaliwa nyumbani kwa Mbunge wa Jimbo la Butiama kwa niaba ya mbunge huyo, Ofesa Mahusiano kutoka ofisi ya Mbunge, Japheth Changalawe amesema Ng’ombe hao 500 wametolewa na marafiki zake kutoka nchini Uturuki.

Amesema hatua hiyo ni ishara ya mshikamano baina yake na marafiki wa nje, viongozi na wananchi na kunaonesha namna tunavyothamini ibada, amani na undugu katika jamii.

Aidha, amesema Ng’ombe hao wamegawanywa kwenye vitongoji 370 na taasisi zote za umma na binafsi zilizopo katika jimbo hilo, kwa ajili ya kitoweo kwa wananchi kipindi hiki cha kusherehekea Sikukuu ya Eid Al-Adha.

View attachment 3359440
Ugawaji wa sadaka hiyo umefanyika kwa siku mbili mfululizo kuanzia jana na leo, kwa kile kinachodaiwa kuwa ni kuonesha moyo View attachment 3359444wa upendo na mshikamano wa Mbunge Sagini kwa wananchi wa jimbo hilo.
Kuua mnyama kama wewe mtu binafsi ni dhambi. Hairuhusiwi kuua myama kwa furaha. Tuńaua mnyama kwa lishe
 
Wakuu

Wananchi wa Wilaya ya Butiama mkoani Mara wamejikuta wakinusuru fedha zao kwaajili ya bajeti ya kitoweo cha sherehe ya sikukuu ya kuchinja ‘Eid al-Adha’ baada ya Mbunge wa Jimbo la Butiama Jumanne Sagini kuchinja Ng’ombe zaidi 500 na kuwagawia.

Tukio hilo limetokea mapema leo Juni 7, 2025 hatua inayotajwa kuwawezesha wananchi hao bila kujali dini zao wanaungana na wenzao ulimwenguni kusherehekea Eid.

Akizungumzia tukio hilo lililoandaliwa nyumbani kwa Mbunge wa Jimbo la Butiama kwa niaba ya mbunge huyo, Ofesa Mahusiano kutoka ofisi ya Mbunge, Japheth Changalawe amesema Ng’ombe hao 500 wametolewa na marafiki zake kutoka nchini Uturuki.

Amesema hatua hiyo ni ishara ya mshikamano baina yake na marafiki wa nje, viongozi na wananchi na kunaonesha namna tunavyothamini ibada, amani na undugu katika jamii.

Aidha, amesema Ng’ombe hao wamegawanywa kwenye vitongoji 370 na taasisi zote za umma na binafsi zilizopo katika jimbo hilo, kwa ajili ya kitoweo kwa wananchi kipindi hiki cha kusherehekea Sikukuu ya Eid Al-Adha.

View attachment 3359440
Ugawaji wa sadaka hiyo umefanyika kwa siku mbili mfululizo kuanzia jana na leo, kwa kile kinachodaiwa kuwa ni kuonesha moyo View attachment 3359444wa upendo na mshikamano wa Mbunge Sagini kwa wananchi wa jimbo hilo.
Kula nyama nyamaza.
 
Huu sasa ni upuuzi, mbunge mzima msomi anashadidia ibada za sanamu, ibada za makafara. Huku kwingine tumekatatazwa tusile makafara hayo ya ibada za sanamu. Kwanza huu mtindo wa kutoa makafara ukiendelea nchini mifugo itaisha. Mifugo inayochinjwa ni mingi balaa. Kondoo na ng'ombe wanateketezwa balaa! Tutakosa maziwa na mbolea ya samadi. Nchi yetu imegeuzwa ni ya kufanyia makafara ya kidini, tena ni wageni ndio wanaonunua mifugo hiyo kwa wingi na kuchinjwa! Ni ibada ya makafara
 
Unakuta masikini wanaenda kupata nyama eneo zilikochinjwa ng'ombe huko misikitini, cha ajabu masikini wanarudi viroba vitupu na wenye nguvu ndio hupata nyama. Kuna wengine hufanya misheni wapate ng'ombe mzima kwa elfu thelathini tu, ni vurugu tupu licha ya kuwa kuna polisi na migambo kulinda wizi na njama za kutaifisha nyama za kwenda buchani. Sasa hii ni ibada gani ya kuchinja kama si uhuni na ushetani?
 
Back
Top Bottom