Bustani ya Eden

Bubu Msemaovyo

JF-Expert Member
May 9, 2007
3,832
2,790
Mungu alitupenda sana sisi wanadamu akatujengea bustani nzuri sana ya Eden ambako binadamu wliobahatika waliweza kuishi kwa raha mustarehe. Kulikuwa na vivutio mbali mbali kama vile mito inayotiririka maji safi kabisa, matunda ya kila aina wanyama wengi na wa kuvutia mabwawa mazuri yaliyojaa ndege wa kila aina ya rangi wakiogelea.
Siku moja Mungu akawaambia binadamu waliokuwa wakiishi pale bustanini kwamba kesho saa sita kamili mchana wote wawe wamekusanyika katika bwawa akawatajia kwa ajili ya kuoga. Kesho yake kama alivyokuwa ameagiza kila mmoja akaondoka kwa wakati wake kama ifuatavyo.
1. Alianza kuondoka Mr. Blair baada ya kuona muda unakaribia aliona bora kuwahi. Alipofika pale bwawani akamkuta malaika aliyemweleza kwamba Mungu ameagiza kila anayefika avue nguo na ajitose bwawani kuoga, wakati huo maji yalikuwa na joto kiasi cha sentigredi 100.
Baada ya saa nne na nusu, akaja Mr Patel anye akapata maagizo akajitosa kwenye maji wakati huo maji yalikuwa yamepoa na kuwa sentigredi 75.
Ilipofika saa 12 jioni akafika Mr. Mwaipopo alipotaka kuingia kuoga Mungu akawa amewaita hivyo Mwaipopo akaloweka viganja na nyayo.
Mungu aliwaita wote akawaona wamebadilika rangi zao, akawaambia.
Blair wewe ni mtiifu na kwa kuwa ulitii kama nilivyokuamuru nawe ukafuata muda utabaki na ngozi yako nyeupe milele, kila mahala utakuwa mtawala mwenye akili na tajiri na kila atayekuona atakujali kuwa ni mwenye akili na atakuheshimu.
Mungu akamwambia Patel ulichelewa kufika bwawani, Patel akabisha, Mungu akasema tazama ngozi yako haijatakata, kwa kuwa umechelewa na ngozi yako haijatakata utabaki hivyo milele. Utatangatanga kila mahali kujitafutia riziki nawe nakupa utajiri kidogo kwa utii wako kidogo.
Akafuta Mwaipopo, Mungu akamwambia Mwaipopo kwanini hujaoga Mwaipopo akamwambia Mungu tazama nilipofika tu nawe ukawa unatuhitaji, nami nikachovya viganja vya mkono wangu na nyayo za miguu yangi na tazama ee Mungu zimetakata, Mungu akamwambia utawatumikia hawa wote kwa kujitafutia riziki yako, nawe nakupa utajiri katika nchi yako nawe hutagundua hilo bali utachelewa kama ulivyochelewa kwenda bwawani. Nakupa akili nyingi lakini utachelewa kugundua kama ulivyochelewa kufika hapa, utatawaliwa muda wote nawe utaweza kutawala dakika za mwisho muda mfupi kabla ya ujio wangu wa mwisho.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom