Busara kidogo inahitajika katika hili

Carleen

JF-Expert Member
Nov 6, 2018
7,503
25,116
Hey guys..!
Huwa napenda kuja hapa na uchiinga' wa hapa na pale, ila naombeni Leo niwe serious kidogo, hii ni issue ya kweli kabisa ya maisha yangu..!!

Sijui kwanini nataka kushare kama ni ushauri nitaupokea, ila kama kuna la kujifunza mtu aweza lichukua pia likamsaidia..

Mimi ni kati ya watu wachache waliobahatika kulelewa na 'baba mlezi' kwa ule upendo ambao lije jua, ije mvua I am 100% sure siwezi upata popote pale, I hate to call it Him baba mlezi, ila huo ndiyo ukhalisia..!!

Na bahati nzuri nilipewa bahati ya kujua ukweli nikiwa mdogo, Baba hakupenda hili jambo lakini kama ningekuja kujua sasa nadhani ningedata kabisa kujua Huyu Mwanaume anayenipenda kuliko chochote kuwa He is not My Real Father...!

Nakumbuka nikiwa mdogo kabisa, nilikuwa natazama photo album ya Mama ya zamani, Nika point picha mojawapo ya mkaka ambaye alikuwa ananifanania sana sana, nikamuambia 'Mama, bila shaka huyu ndiye Fulani' (hapa nilimtaja baba mzazi kwa jina lake)..

Mama alicheka akauliza umejuaje.?? Nikamuambia nimeona tu tunavyofanana, akaniambia ni kweli ni yeye..! Hilo likaishia hapo na ni sura ya ujanani kabisa, hivyo nikabaki na wazo tu kuwa Me and that man we real look alike, maisha yakaendelea hivyo..!!

Baba mlezi ndiye Baba ambaye nimekua nikijua huyu ndiye dunia yangu, He is so proud ov Me na hivi tuko na lighting color wote, hivyo nikitembea naye natambulishwa almost everywhere like she is my first daughter, na watu wakiona hiyo rangi angavu wanajua kabisa ndiyo ni kweli na husema kabisa mmefanana hasa..!

Katika wanaume I can admit wameni spoil ni this Man, na ukubwa wangu huu imagine that man bado ananiita 'my happiness' 'totoo', 'my everything'..! ana watoto wengine wa kike kwa kiume lakini the whole family inajua kipenzi cha Baba ni nani..!

Katika watu naogopa kuumiza maishani mwangu ni huyu mwanaume, Imagine, alinambia 'binti yangu, usije kuniaibisha', hayo maneno huwa natembea nayo chochote nachofanya nawaza nisije m-dissapoint yule mwanaume, japo ni muda mrefu ila huwa yanaishi moyoni mwangu daima..!!

Baada ya yote hayo, nikiwa binti mkubwa kabisa mwaka Jana mwishoni, napokea simu ya mtu anajitambulisha kuwa Mimi ni mwanae, kwanza I was shocked sababu najua baba yangu nilishapiga naye story mchana, mpaka aliponitajia jina ndiyo nikaelewa..!!

Nikajikuta nalia machozi, sijui ni kwanini nililia vile, anyways, nilizungumza naye kwa nidhamu na utulivu mkubwa nikawa namsikiliza, akaniambia anaomba sana samahani kwa kuniacha miaka yote hiyo, na alikuwa akinitafuta sana bila mafanikio ila hivi sasa ndiyo kafanikiwa kunipata..!

Anaomba sana samahani, kwa kuniacha, kutokuwa pale kwa ajili yangu na pia kwa kumuumiza Mama, na kinachomuuma hakufanikiwa kupata mtoto wa kike huko alikokwenda Mimi ndiyo bintiye wa pekee, kapata watoto wa kiume woote..!!

Huruma ni kweli alikuwa anatia me nikamuambia Mimi sina tatizi lolote na wewe, ila kwa jinsi ulivyomuumiza yule Mama sijui ni kitu gani utafanya mpaka tu akuelewe na kukusamehe maneno uliyomtamkia na jinsi ulivyomuacha Mimi nikiwa tumboni na nikuambie tu ukweli hajawahi kusahau..!

Akawa anataka tuonane japo anione tu, nikamuambia ongea kwanza na Mama, ndiyo naweza nikakuona japo kwa sehemu tulizokuwepo tulikuwa jirani kiasi ila sikuweza tu kwenda kumuona bila ruhusa, na pia sikutaka kabisa kumshirikisha hili Baba nilihisi tu kama atajiskia vibaya, sijui ni kwanini nilifikiri hivyo, kama nilivyosema mwanzo sikutaka nimfanye ajiskie vibaya kwa ajili yangu kwa namna yoyote ile,

Mpaka Leo sikuwahi muambia Baba yangu chochote na yeye hakuwahi niuliza chochote japo Mama alishamuambia kuwa baba mzazi kanitafuta, Nadhani anasubiri kama nitamuambia chochote ila Mimi siwezi muambia kitu kiukweli..!!

Japo kiukweli niliwahi enda kumuona baba mzazi, I was just curious kumuona na ni kitu nilikuwa natamani sana, I can admit he is very charming person kama Mimi anapenda kufurahi mno pia.! Ila nimekaa naye na kuongea naye it's like talking to a stranger, ana maisha yake tu anajiweza lakini Ile furaha hupata nikiwa na Baba yangu mlezi it was never there.! tulifanikiwa kuongea mengi na kupiga story na akawa anajutia sana lakini on my side nilimuambia ni sawa tu nilishamsamehe..!

Tatizo linaanzia wapi, sahii analalamika anataka ule ukaribu na bond ya Baba na Mwanae, anahisi namtenga, anahisi sijamsamehe, lakini sina tatizo naye ni kuwa almost every day the only Man that came into my mind ni Baba Mlezi, the only Man niwe na siku nzuri ama mbaya lazima nimuambie na ni lazima anitafute ama nimtafute, na ukubwa huu lakini ni kawaida kuona 'Imethibitishwa' zake kwa simu yangu, huwa ananitreat bado kama vile Mimi ni kabinti kadogo, mpaka niliwahi muambia nikija olewa nitahakikisha naolewa na mwanaume anayenipenda at least nusu ya upendo wako, akacheka akaniambia tu Muombe Mungu sana na ulivyo tu huyo mwanaume kazi atakuwa nayo, nikamuambia wewe ndiyo umeniharibu lakini, akatabasamu akajibu, ipo siku nitakuja kuelewa..!

Kabla nisahau, Mama hataki ushirika naye kabisa anasema Baba anayemtambua yeye ni Baba Mlezi tu, japo yeye pia alimuambia ashamsamehe hivyo asijali aendelee na maisha yake kwa amani, Naomba nikazie hapa My Ma hajawahi nizuia Mimi kuwasiliana wala kumuona Baba sababu ni yeye ndiye alipambana nitumie jina la Baba mzazi alisema hataki nipoteze haki ya kumjua baba mzazi pia, na alikuwa anaimani sana kuwa ipo siku baba yako mzazi atarudi tu na utamuona, na kweli yakatimia..!!

tukirudi huku kwa baba mzazi, analalamika mpaka namuonea huruma lakini sipati ile feeling ya ubaba juu yake what am I supposed to do.? Na huwa ananitumia pesa za hapa na pale ananiambia vocha namuambia tu ahsante, hata ile kuita 'Baba' naona ugumu, me huwa naishi zangu kama vile he doesn't exist, nikikumbuka ni mara moja namjulia hali mpaka nikumbuke tena siyo Leo, most of the time yeye ndiye hunitafuta na malalamiko juu anahisi nafanya kusudi kumkomoa lakini hapana, moyo wangu unaishi huku kwingine toka utotoni..! anataka nikawajue ndugu zake lakini I don't feel like I do belong there, kawapa ndugu zake namba wananitafuta lakini siwafurahii all the same pia, na kumsamehe nishamsamehe lakini the bond ain't there, na malalamiko yake yananiumiza lakini nimeshindwa yafanyia kazi..!!

Nashindwa hata nimfanye nini maskiini..!!
 
Una kesi kama ya shosti angu mmoja ila yeye aliamua kusimama upande wa Mama yake na Baba mlezi. Huyo Baba mzazi muache alalamike weee atachoka mwenyewe kamwe usije umiza waliokua nawe kipindi kigumu na cha furaha.

Hawa jamaa wa hit and run ndo kawaida zao hizo. Anakimbia huku akijua kuna mimba au mtoto katelekeza anabaki kujipa matumaini atanitafuta akikua.

Ukisogeza ukaribu zaidi kituo cha pili kitakua kutembeleana,leo atataka uende huku kesho kule kesho kutwa pale.

Muheshimu tu kama mmoja wa wazazi wako.
 
Hey guys..!
Huwa napenda kuja hapa na uchiinga' wa hapa na pale, ila naombeni Leo niwe serious kidogo, hii ni issue ya kweli kabisa ya maisha yangu..!!

Sijui kwanini nataka kushare kama ni ushauri nitaupokea, ila kama kuna la kujifunza mtu aweza lichukua pia likamsaidia..
Seat ya mbele kabisa
 
Una kesi kama ya shosti angu mmoja ila yeye aliamua kusimama upande wa Mama yake na Baba mlezi. Huyo Baba mzazi muache alalamike weee atachoka mwenyewe kamwe usije umiza waliokua nawe kipindi kigumu na cha furaha.

Hawa jamaa wa hit and run ndo kawaida zao hizo. Anakimbia huku akijua kuna mimba au mtoto katelekeza anabaki kujipa matumaini atanitafuta akikua.

Ukisogeza ukaribu zaidi kituo cha pili kitakua kutembeleana,leo atataka uende huku kesho kule kesho kutwa pale.

Muheshimu tu kama mmoja wa wazazi wao.
Hapa nakazia.
 
Ni Kazi sana kutengeza Bond kwa sasa.

Bond inatengenezwa toka mtoto yuko tumboni, anazaliwa.
Pale analia anabebwa na mikono ya Baba. Anamkojolea, anakua, anachezea viatu vya Baba, anamchafua, anaanza shule, anachapwa kisha anabembelezwa. And so on...... Na hakuna shortcut

Baba yako ali- mess up, asitegemee mambo yatakuwa sawa tuu.

Kwa upande wako wewe hauna kosa, usijilazimishe kumlidhisha.
 
Katika wanaume I can admit wameni spoil ni this Man, na ukubwa wangu huu imagine that man bado ananiita 'my happiness' 'totoo', 'my everything'..! ana watoto wengine wa kike kwa kiume lakini the whole family inajua kipenzi cha Baba ni nani..!

Katika watu naogopa kuumiza maishani mwangu ni huyu mwanaume, Imagine, alinambia 'binti yangu, usije kuniaibisha', hayo maneno huwa natembea nayo chochote nachofanya nawaza nisije m-dissapoint yule mwanaume, japo ni muda mrefu ila huwa yanaishi moyoni mwangu daima..!!
Natumaini unaona hizo sehemu nilizoBold na kuweka strikethrough
-
Kwa tamaduni zetu za kiafrika mtu ambae unamuheshimu kama mzazi hutakiwi kumu-Address kama ulivyofanya hapa, kwa muono wangu sidhani kama inaleta picha nzuri kumuita baba yako mzazi au mlezi "Huyu Mwanaume" hilo ni jina analoweza kuita mama yako pekee. Otherwise Ukifanya kama ulivyofanya hapa wengine wanaweza kuhisi kuna hali ya incest kati yenu. Maybe ndio maana nae inakua rahisi kukuita "Toto langu"

I'm so sorry for saying this to you I might be wrong too but my point is pinned to the fact that the way you address your father figure is not Healthy. Change!!!!
______
Rolling to the main topic!!

Kuna Father na Daddy, Father anatia mimba hajali Mtoto atakua vipi na kuishi vipi...Daddy anatia mimba na kujali kiumbe hicho alicholeta duniani kwa "Kuwepo" pembeni ya kiumbe huyo siku zote. Kwa maelezo ulivyoeleza huyo aliyekuzaa he was your father but wasn't your Daddy. Anachokifanya ni kutaka kula mavuno ya shamba ambalo hakulipalilia, jambo hili Hata Mungu kakataza. Maana anasema...

Mathayo 25:24,28,30
[24]Akaja na yule aliyepokea talanta moja, akasema, Bwana, nalitambua ya kuwa wewe u mtu mgumu, wavuna usipopanda, wakusanya usipotawanya;
[26]Bwana wake akajibu, akamwambia, Wewe mtumwa mbaya na mlegevu, ulijua ya kuwa navuna nisipopanda, nakusanya nisipotawanya;
[27]basi, ilikupasa kuiweka fedha yangu kwa watoao riba; nami nikija ningalipata iliyo yangu na faida yake.
[28]Basi, mnyang’anyeni talanta hiyo, mpeni yule aliye nazo talanta kumi.
[30]Na mtumwa yule asiyefaa, mtupeni mbali katika giza la nje; ndiko kutakuwako kilio na kusaga meno.

Btw Kwakua hatujajua kisa cha mzazi halisi kukutelekeza basi Siwezi mlaumu. Ila cha msingi ongea na mama yako akupe kisa chote cha baba yako kukuacha kisha msikilize na baba yako pia upande wako then wewe mwenyewe utaamua cha kufanya. Choose wisely

Obvious naamini baba yako anachotaka ni kupata recognition ya kua wewe ni mtoto wake if so basi mpatie. Mjulie hali hata kwa simu mara moja moja mtembelee, ila mapenzi kwa baba mlezi usipunguze kamwe.
 
My dear huyo ni sperm donor sio baba ako anaona haya na kuumia kwa kua umelelewa vzr umekua vzr mama na mwanaume mwingine wameplay part vzr usije kumuumiza aliyekula nawe toka utotoni rafiki,jus mchukulie kama wengine.Jiulize ungekua jambazi au huna direction angekutafuta?!!achana nae

Sent from my Infinix X559C using JamiiForums mobile app
 
Natumaini unaona hizo sehemu nilizoBold na kuweka strikethrough
-
Kwa tamaduni zetu za kiafrika mtu ambae unamuheshimu kama mzazi hutakiwi kumu-Address kama ulivyofanya hapa, kwa muono wangu sidhani kama inaleta picha nzuri kumuita baba yako mzazi au mlezi "Huyu Mwanaume" hilo ni jina analoweza kuita mama yako pekee. Otherwise Ukifanya kama ulivyofanya hapa wengine wanaweza kuhisi kuna hali ya incest kati yenu. Maybe ndio maana nae inakua rahisi kukuita "Toto langu"

I'm so sorry for saying this to you I might be wrong too but my point is pinned to the fact that the way you address your father figure is not Healthy. Change!!!!
______
Rolling to the main topic!!

Kuna Father na Daddy, Father anatia mimba hajali Mtoto atakua vipi na kuishi vipi...Daddy anatia mimba na kujali kiumbe hicho alicholeta duniani kwa "Kuwepo" pembeni ya kiumbe huyo siku zote. Kwa maelezo ulivyoeleza huyo aliyekuzaa he was your father but wasn't your Daddy. Anachokifanya ni kutaka kula mavuno ya shamba ambalo hakulipalilia, jambo hili Hata Mungu kakataza. Maana anasema...

Mathayo 25:24,28,30
[24]Akaja na yule aliyepokea talanta moja, akasema, Bwana, nalitambua ya kuwa wewe u mtu mgumu, wavuna usipopanda, wakusanya usipotawanya;
[26]Bwana wake akajibu, akamwambia, Wewe mtumwa mbaya na mlegevu, ulijua ya kuwa navuna nisipopanda, nakusanya nisipotawanya;
[27]basi, ilikupasa kuiweka fedha yangu kwa watoao riba; nami nikija ningalipata iliyo yangu na faida yake.
[28]Basi, mnyang’anyeni talanta hiyo, mpeni yule aliye nazo talanta kumi.
[30]Na mtumwa yule asiyefaa, mtupeni mbali katika giza la nje; ndiko kutakuwako kilio na kusaga meno.

Btw Kwakua hatujajua kisa cha mzazi halisi kukutelekeza basi Siwezi mlaumu. Ila cha msingi ongea na mama yako akupe kisa chote cha baba yako kukuacha kisha msikilize na baba yako pia upande wako then wewe mwenyewe utaamua cha kufanya. Choose wisely

Obvious naamini baba yako anachotaka ni kupata recognition ya kua wewe ni mtoto wake if so basi mpatie. Mjulie hali hata kwa simu mara moja moja mtembelee, ila mapenzi kwa baba mlezi usipunguze kamwe.
Yaani umeshauri kitaalam sana big up watu kama wewe ni wachache! Mtoto anaweza kulishwa sumu ya maneno na akajenga chuki bila kujua upande wa pili
 
Natumaini unaona hizo sehemu nilizoBold na kuweka strikethrough
-
Kwa tamaduni zetu za kiafrika mtu ambae unamuheshimu kama mzazi hutakiwi kumu-Address kama ulivyofanya hapa, kwa muono wangu sidhani kama inaleta picha nzuri kumuita baba yako mzazi au mlezi "Huyu Mwanaume" hilo ni jina analoweza kuita mama yako pekee. Otherwise Ukifanya kama ulivyofanya hapa wengine wanaweza kuhisi kuna hali ya incest kati yenu. Maybe ndio maana nae inakua rahisi kukuita "Toto langu"

I'm so sorry for saying this to you I might be wrong too but my point is pinned to the fact that the way you address your father figure is not Healthy. Change!!!!
______
Rolling to the main topic!!

Kuna Father na Daddy, Father anatia mimba hajali Mtoto atakua vipi na kuishi vipi...Daddy anatia mimba na kujali kiumbe hicho alicholeta duniani kwa "Kuwepo" pembeni ya kiumbe huyo siku zote. Kwa maelezo ulivyoeleza huyo aliyekuzaa he was your father but wasn't your Daddy. Anachokifanya ni kutaka kula mavuno ya shamba ambalo hakulipalilia, jambo hili Hata Mungu kakataza. Maana anasema...

Mathayo 25:24,28,30
[24]Akaja na yule aliyepokea talanta moja, akasema, Bwana, nalitambua ya kuwa wewe u mtu mgumu, wavuna usipopanda, wakusanya usipotawanya;
[26]Bwana wake akajibu, akamwambia, Wewe mtumwa mbaya na mlegevu, ulijua ya kuwa navuna nisipopanda, nakusanya nisipotawanya;
[27]basi, ilikupasa kuiweka fedha yangu kwa watoao riba; nami nikija ningalipata iliyo yangu na faida yake.
[28]Basi, mnyang’anyeni talanta hiyo, mpeni yule aliye nazo talanta kumi.
[30]Na mtumwa yule asiyefaa, mtupeni mbali katika giza la nje; ndiko kutakuwako kilio na kusaga meno.

Btw Kwakua hatujajua kisa cha mzazi halisi kukutelekeza basi Siwezi mlaumu. Ila cha msingi ongea na mama yako akupe kisa chote cha baba yako kukuacha kisha msikilize na baba yako pia upande wako then wewe mwenyewe utaamua cha kufanya. Choose wisely

Obvious naamini baba yako anachotaka ni kupata recognition ya kua wewe ni mtoto wake if so basi mpatie. Mjulie hali hata kwa simu mara moja moja mtembelee, ila mapenzi kwa baba mlezi usipunguze kamwe.
Relax mkuu. Kuna vitu sio vya kuchukulia serious namna hii. Umewaza mpaka habari za incest, that's too much imagination for such an ordinary storyline!

Back to the topic, nimeona vitu kadhaa:

- Baba mzazi hakufanikiwa kupata mtoto wa kike huko aliko. Ndugu mleta mada, do you really think the old man angekutafuta kama huko aliko angepata mabinti kadhaa? Hata usinijibu hili swali.

- Baba mlezi hajui kama unawasiliana na baba mzazi. You're about to hurt that old man. Sisi wanaume tunakuaga very territorial. Once we have what we consider to be family, haturuhusu another man aingilie chain of command and how we're running the show. Mlezi akigundua baba mzazi is back, and you're sneaking behind his back, ataumia kinoma. Ni either umwambie mwenyewe, au uache ku-hangout na upande wa baba mzazi.

- Hakuna bond kati yako na baba mzazi, zaidi ya baiolojia iliyokuleta duniani. Umekua na undugu na upande wa baba mlezi. Brothers, sisters na wengineo, they all consider you one of their very own. Huko kwa baba mzazi hautaweza kutengeneza bond mpya, na kama ukiweza kuna mahala utavunja kwa ndugu zako wa upande wa baba mlezi. Pick your side wisely sweetheart!


Kwa upande wangu, undugu sio kushare damu. Undugu ni nani yuko na wewe through thick and thin. Nani anaguswa na shida zako? nani anaumia ukipitia magumu? Binafsi, kuna washkaji tu nawathamini kuliko "ndugu". It's because they've got my back when shit goes down!

Nashauri ukae na baba mzazi, umpe ukweli. Mwambie nakutambua mzee, and I do respect you. Ila hatuwezi kua na bond like family. I already belong somewhere else. Kuna watu wamenikuza like one of their own, itakua ngumu kuswitch sides kwa sasa. Tuendelee tu hivihivi.

Ukimaliza hapo, rudi kwa Baba mlezi umpe picha nzima. And maybe, muulize anashauri nini. It will make him feel better, kuliko kukaa kimya huku akiwa anajua kinachoendelea.

NB: kumbe mleta mada uko na light skin sio? Uko na kapicha tuone?
 
duh! haya mambo yapo sana kwa sisi tunaoishi na masingle mother, ila pia unatakiwa kuelewa kuwa huyo baba ako mzazi aliachana na ur mumy kwa7bu zipi! usukute labda alifumaniwa, au usikute labda huyo baba ako mzazi ndiye aliyeharibu mahusiano yake kayi ya baba mlezi na mama ako
 
Lil sis don't stress yourself; Wala hata usiwaze huyo baba yako anajisikiaje; sio shida zako hata kama umemsamehe.

Baba yako ni mtu selfish; wakati wewe unamuhitaji kwenye maisha yako; yeye hakuwa tayari. Muda huu yeye anakuhitaji wewe na anakulazimishia; sio sawa.

Ukweli ni kwamba sio kila mwanaume ni baba. Kuna watu wengi waliolelewa na baba zao; lakini hicho alicho/anachokupa baba yako mlezi; kuna millions of people hawajawahi kuki_experience. Mshukuru huyo baba yako mlezi sanaaaaa. Hujapata ombwe/ trauma kwa sababu ya kutokulelewa na baba; kwa sababu yeye aliamua kuwa baba ambaye hukuwa naye. Mimi ninajua umuhimu wa uwepo wa baba kwenye maisha ya mtoto wa kike; kwa kukukubali wewe na kukufanya mtoto wake uuuh; kitu kikubwa mnoooo, ni neema.

Tena mama yako mmmh basi tu; mimi binafsi ningekupa na surname ya huyo baba mlezi period; ingebaki tu damu yake kwako maana haiwezi kutolewa. Ubaba sio tu kumwaga mbegu; ubaba ni malezi. Baba ni yule anayejua umekula nini, umevaa nini, umelala wapi; anakupenda, anakujali, anakufundisha, anakuoyna, anakuwa concerned na wewe kwa Kila hali. Ukiumwa, ukiwa na changamoto yoyote; he is always there you. Huyo ndiyo baba na hicho kinacho-form bond kati ya mtoto na mzazi. You are an absentee parent; don't expect any bond with your child

Huyo baba yako mzazi; kaa naye kwa kina mwambie tu you are at peace with him, unamtambua kama baba yako mzazi; ila huwezi kuwa karibu naye kama anavyotamani. Ni mtoto wake kwa kukuzaa; but alishauza hiyo haki kwa mwanaume mwingine.

Nenda kamwambie baba yako mlezi ukweli wote; asije akakuona you are an ingrate. Naamini amefanya Kila kitu kwenye maisha yako kwa sababu ya upendo na sio kungoja shukrani. But kiubinadamu tu; mpe tu shukrani zake; una deni juu yake. Mpe na msimamo wako juu ya huyo baba yako mzazi. Hakikisha baba yako mlezi ana amani juu yako. Don't lose than man, don't hurt him, don't disappoint him. Make him proud; isije siku akasema "mtoto wa watu ni wa watu tu".
 
Back
Top Bottom