Kwani anawaua bure, me naona ana retaliate, sababu wanamvamia wanataka kumuua, sasa kama ww watu wanataka kukuua utafanyeje.
Turudi kwa hao wavamiaji kwenye kambi za jeshi ni kina nani hao, na kwanini kuna tuhuma toka UN na serikali ya Bujumbura kwamba wanafadhiliwa na Kagame, au UN nao wanawasingizia.
Na kwanini vurugu zinasikika Bujumbura peke yake.
Ishara zote zinaonyesha kuna mchezo mchafu sana unachezwa, prior to these Burundi election sijawai sikia Nkuruzinza kawinda watu awaue, ila Kagame kaua mpinzani wake South Africa, kaua Tz, Belgium nilisoma mmoja alikoswa koswa na RPF fortunately yake Belgium police waliwashtukia majamaa wakamwepusha, vitisho alivomchimba JK.
Haya ni mambo yametukia nikiwa na akili timamu achana na story zingine za kusoma na kufuatilia, mtu ukiwa neutral ukafuatilia hizi mambo zenu utaona kabisa Kagame na some guys wa ethnicity yake, baadhi wapo humu, ni tatizo.
Najua utapinga, ila ukweli haupingwi.