Utotole
JF-Expert Member
- Oct 28, 2010
- 6,608
- 4,265
Ni kweli ulichosema. Mgawanyo huo wa divide and rule ndio ulioanzisha matabaka haya. Watutsi walitumika kama viranja wa kutekeleza majukumu ya wakoloni. Wahutu wakawa tabaka la watawaliwa na watu wa hadhi ya chini. Hii ilichochea uadui ambao hata leo unaendelea. Mtutsi anajihisi kama yupo kifungoni anapokuwa chini ya uongozi wa Mhutu, kwa sababu yeye anaamini 'aliumbwa ili atawale'. Na hii yote kafanya mbeligiji. Bahati mbaya hii nchi kimsingi ina makabila hayo mawili. Sasa uhasama wa makabila mawili ni ngumu sana kuisha. Ingekuwa rahisi kama haya makabila yangekuwa absorbed na kuwa 'dissolved' ndani ya jamii yenye makabila mengi zaidi. Kwa hali ilivyo sasa, mchezo utakuwa huo huo wa kupinduana na kuchocheana.Inasikitisha sana,Huyu Buyoya ni hatari sana,yaani hawa wahutu na watusi ;Mkoloni ndo alifanya huu uadui wa watutsi ukolee,Maana Mbelge alipofika Rwanda na Burundi ndo akawakoleza wasielewane zaidi ili awatawale kirahisi,unaambiwa hata kwenye mitihani yao walikuwa wanaandika ethinic groupe zao,unaandika kama wewe ni mtutsi au mhutu,sasa hapo mwalimu akiwa mtutsi halafu asahihishe paper ya mhutu ,huyo mhutu lazima afeli,yaani mimi niliposimuliwa jinsi wanavyouishi huo uadui wa kiethenic mpaka nilitoa machozi.HIYO IMESAMBAA VIZAZI MPAKA VIZAZI