Kwahyo amewazidi Kidayo na Obo kwa sasa huku Afrika?
Brother kwa era hii Burna ni habari nyingine asee hivi unajua wiki kama mbili zilizopita kaweka rekodi yake ya kujaza Arena huko Uingereza?
Mafanikio ya msanii sio kwenye views, followers na skendo, fuatilia historia ya Burnaboy jamaa alikuepo kitambo tu sema hakuwai wika kiivyo nliwai soma documentary flan wanasema jamaa alianza imba ana 10 yrz na 19 yrz alikuwa anaendesha Range.
Huyu jamaa ana management ya kipekee kwanza mama yake ndio msimamizi wa kazi zake na show kwa ujumla, wanakwambia hata matumizi ya simu kwa jamaa wanacontrol na Management na simu yake wamemuachia Whatsapp tu. Angalia katika account ya Jamaa vitu anavyopost kama sio show na picha za akiwa anatumbuiza au yuko katika harakati za kwenda tumbuiza, kwangu Mimi Burna ni Mkali sana kuliko hata hao kina Davido wanaotumia nguvu nyingi kupambana just imagine jamaa kaja na style yake na kapenya simple tu