May Day
JF-Expert Member
- May 18, 2018
- 6,162
- 8,820
Mwaka huo wa 1963 Bilal Rehani Waikela akakabiliana na Nyerere katika risala aliyosoma mbele yake katika ufungaji wa Muslim Congress iliyofanyika katika ukumbi wa Shule ya Aga Khan ya Wasichana.The Boss,
Mwaka wa 1963 ulikuwa mwaka wa matukio makubwa kwa Waislam wa Tanganyika.
Ndani ya Halmashauri Kuu ya TANU Julius Nyerere alipambana kwa maneno makali na Titi Mohamed ugomvi ukiwa Aga Khan na East African Muslim Welfare Society (EAMWS).
Ugomvi huu hakuweza kumalizika kwani wote wawili walikuwa na mfundo ndani ya nafsi zao.
Shariff Hussein Badawy na mdogo wake Mwinyibaba wakafukuzwa nchini warudi kwao Kenya.
Shariff Hussein alikuwa na madrasa kubwa Msikiti wa Badawy (sasa Rawdha).
Mwaka huo wa 1963 Bilal Rehani Waikela akakabiliana na Nyerere katika risala aliyosoma mbele yake katika ufungaji wa Muslim Congress iliyofanyika katika ukumbi wa Shule ya Aga Khan ya Wasichana.
Mwaka huo Baraza la Wazee wa TANU chini ya uenyekiti wa Mzee Iddi Tulio likavunjwa kwa madai kuwa baraza lilikuwa linachanganya dini na siasa.
Wajumbe wote wa baraza hili walikuwa Waislam na lilitoa mchango mkubwa katika kupigania uhuru wa Tanganyika.
Historia hiyo hapo juu nimeieleza kwa kirefu katika kitabu cha Abdul Sykes.
Mzee Bilal (wakati huo Kijana) alipotakiwa kuchagua moja kati ya Siasa/Chama(TANU) na Muslim Walfare Societ ndipo rasmi akaachana na TANU kubaki na Muslim Walfare Societ.
Sipo kwenye aina ya misimamo yake, ila Mzee ni mfano wa Watu wenye misimamo thabiti kwa kile wanachokiamini, tofauti kabisa na Wanasiasa tulionao leo hii, wepesi sana ambapo wakitikiswa kidogo tu wanafuata upepo.