Always...Sheikh Mohammed said,..
Naomba nkushaur mwalim wangu..
Umefka wakat Utuandikie kitabu cha Maisha yako na Picha zoote za Kihistoria zako utuwekee Lkn Utupe uhusiano na wote waloipgania Nchi yetu..
Hyo ni Kumbu Kumbu Nzur kwetu..
Ahsante
Kede...Mwapachu sio mkenya?Na jabe ni mkenya pia na wendo pia ni mkenya!
JK,..Sheikh Mohamed Said pole kwa kuondokewa na rafiki yako.
Uchuro kujiandikia kitabu,akiandika tu bye bye.Sheikh Mohammed said,..
Naomba nkushaur mwalim wangu..
Umefka wakat Utuandikie kitabu cha Maisha yako na Picha zoote za Kihistoria zako utuwekee Lkn Utupe uhusiano na wote waloipgania Nchi yetu..
Hyo ni Kumbu Kumbu Nzur kwetu..
Ahsante
Pole mzee,nasikia mzee wao na akina mwapachu wakati anafariki watoto wake including wendo walikuwa wadogo sana hivyo wakalelewa na mwalimu nyerere sijui ikulu sijui msasani sijuiKede...
Nifafanulie sijaweza kuelewa.
Hamza Mwapachu baba yao ni Mdigo wa Tanga.
Mbona umetaja Kenya?
Au kuna mahali mimi sijaeleweka?
Tafadhali nifahamishe.
Baba yao akiitwa hamza mwapachu alikuwa naibu katibu mkuu wizara ya mambo ya ndani .alifariki 1962,akiwa na miaka 49,Tanga ni kwao kwa asili tu ila hao mjini kitamboNilijua MWAPACHU walikuwa wakiishi Tanga?
Mdukuzi,Uchuro kujiandikia kitabu,akiandika tu bye bye.
Baba yao akiitwa hamza mwapachu alikuwa naibu katibu mkuu wizara ya mambo ya ndani .alifariki 1962,akiwa na miaka 49,Tanga ni kwao kwa asili tu ila hao mjini kitambo
The Boss,Hamza si alisoma n Nyerere Makerere?
Duh alikufa mapema sana kumbe
Kibu...Mzee kumbe ulisoma St. Joseph's Convent!
Watu wengi wa zamani wamepita hapo, marehemu babangu mmojawapo
The Boss,
Naam walikuwa pamoja Makerere.
The Boss,Mwapachu kafariki 1962
Sheikh Amri Abeid mwaka 1963..
Fundikira alishafukuzwa cabinet mwaka huo ..
Prominent Muslims were becoming even more fewer in the government..
"Nimemjua Wendo kwa kujulishwa kwake na Ted kama tulivyozoea kumwita.Buriani rafiki yangu Wendo Mwapachu!
Leo jioni katika makaburi ya Kisutu tumemzika Wendo Mwapachu.
Nimemjua Wendo kwa kujulishwa kwake na Ted kama tulivyozoea kumwita.
Ted sasa hivi Chief Edward Makwai wa Siha ndiye aliyenijulisha kwake.
Wao ni ndugu wa damu na ni siku hiyo hiyo nilimjua kaka yake Juma Mwapachu na mdogo wao wa mwisho Jabe.
Siku hiyo nilikwenda kuhudhuria birthday party ya Ted rafiki na classmate form 1 D St. Joseph's Convent School.
Ilikuwa mwaka wa 1967.
Wendo akawa rafiki yangu hadi leo tunamtia kaburini.
Kuna picha mbili za kwanza za tukio moja nimeweka hapo chini, hii picha ina umri wa nusu karne.
Katika picha hiyo waliokaa kulia ni Wendo, Esther Mzena, Stella Emmanuel aliyesimama ni Kamili Mussa kulia waliosimama ni Haitham Rashid na mimi mwandishi na nyuma yangu ni Philip sikumbuki jina lake la pili ila namkumbuka alikuwa mtoto wa mmoja wa wapigania uhuru wa Afrika Kusini akisoma Shule ya Wakimbizi Kurasini sasa (Centre for Foreign Relations).
Tulikwenda picnic Kigamboni kwenye nyumba ambayo wakati wa ukoloni magavana ndipo walipokuwa wakienda kupumzika.
Baada ya uhuru nyumba hii ikawa mahali alipotakiwa apumzike rais wa Tanganyika Julius Nyerere na familia yake.
Taarifa ni kuwa Mwalimu hakuwa mtu wa kupenda kupumzika pwani mchangani hivyo nyumba hiyo sisi tukawa na fursa ya kuitumia kila tulipotaka kwani baadhi ya watoto waliokuwa wanaishi State House walikuwa vijana wenzetu.
Picnic hii ilikuwa mwaka wa 1968.
Leo naiangalia picha hii machozi yanataka kunitoka.
Hakika tumetoka mbali.
Namtazama Wendo na sura yake jamil.
Naona ni kama jana.
Picha nyingine kundi zima ''The Scorpions,'' lime ''pose.''
Kulia waliosimama Mohamed Said, Yusuf Zialor, Kleist Sykes, Bubby Bokhari, Abdallah Tambaza.
Waliochutama kulia: Abdul Mtemvu, Wendo Mwapachu na Kais.
Hii ilikuwa party ya kumuaga Liliane Abbas Sykes anakwenda shule Ufaransa mwaka wa 1968.
Lily kama tulivyopenda kumwita tulikuwa tukisoma pamoja hapo St. Joseph's Convent.
Hakika ni nusu karne lakini kila nikiipeleka akili yangu nyuma naona kama jana.
Namkumbuka Wendo kama alivyokuwa tukiwa watoto wadogo na jinsi alivyokuwa ukubwani.
Wendo alikuwa mtu wa kupendeka.
Nimeweka picha nyingine Wendo akiwa na Chief Edward Makwaia na Jenerali Ulimwengu ambae leo nyumbani kwa marehemu alimzungumza Wendo na akaeleza ule moyo wake wa huruma aliokuwanao na mkono mwepesi wa kuwasaidia wahitaji.
Picha hii nilimpiga kwenye msiba wa Kleist.
Namkumbuka Wendo Mtega Mwapachu.
Wendo alikuwa mtu mwema karim hujapata kuona.
Wendo hakuwa mzungumzaji alikuwa mtu mkimya.
Mara moja moja miaka ya nyuma mimi na yeye na jamaa tukiwa pamoja Wendo kwa kutambua mapenzi yangu kwa Prof. Ali Mazrui atanieleza jinsi alivyokuwa anaburudika na "lectures," za Mazrui wakati akisoma Makerere katika miaka ya mwanzoni 1970s.
Miaka hiyo Mazrui alikuwa akifundisha chuoni hapo.
Hapo chini ni moja kati ya kumbukumbu inayoishi moyoni kwangu ambayo Wendo ameniachia.
Mwaka wa 1991 nilikuwa naondoka Dar es Salaam kwa kipindi kirefu kidogo na safari siku ya pili.
Siku hiyo kabla ya safari wakaja vijana nyumbani kwangu wanatafuta msaada wa kujenga madrasa ya kisasa ya chekechea na kuendelea Mwananyamala A wawafundishe watoto kusoma, kuandika, hesabu na Qur' an.
Hii madrasa ilikuwa imeanzishwa na Bi. Fatuma na akisomesha mwenyewe kisha wanafunzi wake wakaichukua wakimsaidia kusomesha.
Hawa vijana ndiyo wakaja na fikra mpya ya kuiboresha madrasa yao iende na nyakati.
Hawa vijana wakaamua kuja kwangu niwatafutie mfadhili.
Mimi nikawachukua hadi kwa Wendo ofisini kwake Business Centre International (BCI).
Wendo akaniambia mimi nindelee na safari yangu na wale vijana nimwachie yeye.
Kama nilivyosema kuwa Wendo hakuwa mtu wa maneno mengi.
Tukaagana.
1992 niliporudi wale vijana wakanichukua hadi Mwananyamala A kunionyesha aliyofanya Wendo.
Nimeingizwa kwenye darasa safi la kisasa lina madawati mazuri wanasoma watoto wadogo.
Wale ndugu zangu wakaniambia kuwa fedha walizopewa na Wendo wao hawakutegemea zitakuwa nyingi kiasi kile alichowapa.
Siwezi kusema mengi kwani chuo hicho kimesomesha watoto wengi Qur'an na kinaendelea kusomesha hadi leo.
Allah mfanyie wepesi mja wako huyu, msamehe dhambi zake na mtie peponi.
Amin.
Buriani rafiki yangu Wendo Mwapachu