BURIANI Mhariri Willy Edward tutakukumbuka kwa hili!

Mongoiwe

JF-Expert Member
Feb 26, 2008
524
263
Siyo vyema kumsema marehemu, hivyo name sikusudii kumsema bali kueleza nitakachomkumbuka nacho. Lakini kwa desturi ya makabila ya Wajita, Wakerewe na kabila la Wajaruo ambalo ninaamini marehemu kama mtani wangu, lilikuwa kabila lake (Kama nitakosea kabira nisamehewe), msibani hulia wakati wa maombolezo kwa kueleza mambo ambayo marehemu alifanya wakati wa uhai wake.

Kwa kuwa ni mtani wangu, ninachoeleza ni hiki ambacho kitanifanya kumkumbuka sana marehemu Willy Edward Ogunde.

Ni kile ulichoakiandika kwa jina lako kwenye Gazeti lako la JAMBO LEO (Aprili 16, 2012) Ukurasa wa kwanza Maneno yakiwa na kichwa cha Habari kisemacho "Chadema Inahusishwa na mashetani, kwamba ‘Dk. Slaa ana jini lake linalomsaidia katika mambo yake ya kisiasa', na ukaongeza kwamba katika dini hiyo (Freemason) ‘Kiongozi wa kanisa Katoliki Duniani Papa naye yumo".

Ulikwenda zaidi ya hapo na hata kuwagusa Marehemu Kanumba na dini hiyo ya mashetani ambaye sasa nina hakika mkikutana huko mtaulizana vyema na kisha utuletee majibu ya uhakika.

Katika kujenga hoja amewaonyesha viongozi mbalimbali wa Dunia kuwa ni waumini wa dini hyo ya kishetani..

Ki ukweli andiko lako hili lilishambuliwa na kuitwa upotoshaji mkubwa, uzushi, uzandiki na uongo kwa umma. Nakumbuka hata mmoja alijaribu kukueleza ukweli huu, nanukuu hapa:
"MY TAKE: Alama ya "V" inayotumiwa na Chadema haina uhusiano na mashetani.. ni ya miaka mingi iliyopita, Jemedari wa vita toka Urumi (Roma) Julius Caiser aliwavamia maadui zake na kuwapiga kwa kusafiri umbali mrefu, alipofika katika himaya ya adui aliua na kuteketeza kila kilicho cha adui.. kufikisha ujumbe kwa walio Rome, Senator J. Caiser alisema "Veni, Vidi, Vici" = "I came, I saw, I conquered".. kuanzia hapo V hiyo ndiyo ikawa alama ya ushindi, na J. Caiser alipopita mbele za watu alikunja vidole kwa alama ya V kama tafsiri ya ushindi, na askari wote waliopigana katika vita hivyo waliwekewa alama ya "V" tatu ktk mabega yao kama alama ya ushujaa, na toka hapo V ikawa alama ya cheo katika majeshi... kumbe alama ya V kwa Chadema si ushetani, haina mahusiano na mashetani...ni alama ya "Victory"...

Hata mashabiki wa mpira hutmia, wachezaji na hata makocha wao (japo wengine hufikili kuwa wanamanisha watashnda goli mbili) siyo Chadema peke yao!"

Hii ilianzia hapa jamiiforumu: https://www.jamiiforums.com/jukwaa-la-siasa/251267-upotoshaji-huu-wa-gazeti-la-jambo-leo-ni-mpaka-lini.html

Ninayakumbuka haya Mhariri, lakini ninakumbuka ulivyokoa busara hata ukamshambulia mwandishi mwenzako Frederick Katulanda pale alipoiweka habari hiyo katika Jukwaa la Mabadiliko, (sijui mliishia wapi ila nikusihii kumsamehe maana katika majadiliano yenu alisema kukusamehe).

Ulichomjibu Katulanda kilikuwa hiki; nakukumbusha maana najua unaweza kuwa umeondoka bila ya kumbukumbu, kwani ninaamini wanaofariki hawabebi vitu kwenda navyo huko mbinguni ama ahera, soma majibu yako haya:

Subject: [Mabadiliko ] JAMBO LEO WAJIBU MAPIGO KWA KATULANDA

Wewe Fredrick Katulanda, acha mambo ya kisenge, naona unatufuatilia >>> sana nyendo zetu, kila mara hatutoki akilini mwako! Nakusoma mara kwa mara unaandika ujinga na kuweka kwenye forum kwa mtazamo wako wa kipuuzi, kishenzi na kifedhuli! Rejea kauli yako hii iliyojaa mashobo na dharau, kuonesha kwamba sisi hatuwezi kufanya kitu chochote eti mpaka tumtegemee mtu fulani! Wakiandika watu wengine kwako ni sahihi, tukiandika sisi si sahihi au tumepewa na mtu fulani!"


Nikusihi basi huko uliko kuchunguza kwa makini jambo hili na kasha tutumie majibu yake, natambua mawasiliani ni shida baina ya huko na hapa duniani, lakini jaribu hata kutushushia kwa ndoto ili tujue ukweli maana kwa jinsi ulivyokufa Ghafla na hali ya mambo ilivyo sasa hapa Tanzania huku na wewe sasa utaanza kutajwa kuwa Ulikuwa Freemason.

Ni hayo tu ambayo niliyawaza haraka baada ya kupata aarifa za msiba wako. Buriani mimi nitakumbuka kwa hayo!
 

Attachments

  • WE.jpg
    WE.jpg
    27.2 KB · Views: 49
...Ni kile ulichoakiandika kwa jina lako kwenye Gazeti lako la JAMBO LEO (Aprili 16, 2012) Ukurasa wa kwanza Maneno yakiwa na kichwa cha Habari kisemacho "Chadema Inahusishwa na mashetani, kwamba ‘Dk. Slaa ana jini lake linalomsaidia katika mambo yake ya kisiasa', na ukaongeza kwamba katika dini hiyo (Freemason) ‘Kiongozi wa kanisa Katoliki Duniani Papa naye yumo".

Ulikwenda zaidi ya hapo na hata kuwagusa Marehemu Kanumba na dini hiyo ya mashetani ambaye sasa nina hakika mkikutana huko mtaulizana vyema na kisha utuletee majibu ya uhakika.


Hii ilianzia hapa jamiiforumu: https://www.jamiiforums.com/jukwaa-la-siasa/251267-upotoshaji-huu-wa-gazeti-la-jambo-leo-ni-mpaka-lini.html

Ninayakumbuka haya Mhariri, lakini ninakumbuka ulivyokoa busara hata ukamshambulia mwandishi mwenzako Frederick Katulanda pale alipoiweka habari hiyo katika Jukwaa la Mabadiliko, (sijui mliishia wapi ila nikusihii kumsamehe maana katika majadiliano yenu alisema kukusamehe).
...

Mungu ailaze Roho ya marehemu mahali inapostahili.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom