Ndugu Watanzania,
Mimi Binafsi ni msomi , daktrari mwenye masters degree mbili. Nimebahatika kusoma nje na ndani ya nchi. Pia nimefanikiwa kuishi nchi mbali mbali zilizoendelea.Kwanini ninatanguliza hizo statements? Najaribu kuonyesha kwamba kidogo nina uwezo wa kulinganisha siasa za nchi yetu na nchi mbali mbali pia nina uwezo wa kulinganisha fikra za wananchi wetu kama citizens na wanachi wa nchi nyingine zilizoendelea na zisizo endelea.
Binafsi nasikitishwa saaana tena saaana na hoja za wabunge bungeni. Sitoongelea upande wowote kwa sababu sina chama na sijawawahi kuwa na chama nchi hiii kwa sababu ya kutoamini upeo wa siasa za nchi hiiii.
Kinachoshangaza , wengine wana shule ila naanza kutia mashaka ni viwango vya shule walizosomea, au ni kwa njia zipi walikuwa wanatahiniwa kupima uelewa wao kimasomo, au ni zile degree za ujanja ujanja tuu, au basi tu masomo ya darasani hayajawasaidia kuchanganua hoja ( Poor analytical thinking).Msomi anatakiwa kuwa na uwezo wa kufikiri nje ya boksi( Thinking out of the box), Msomi anatakiwa aweze kujitofautisha na yule ambaye hajasoma ( Ellite VS Illiterate).
Nashauri hawa the so called wabunge...kwanza siwezi kuwaita waheshimiwa hata siku moja maana mawazo yao hayasupport hiyo heshima. Nawashauri , shambulieni agenda , tena kwa kutumia data zaidi, acheni kushambulia mtu (dont attack a person neither their personality), attack the agenda with evidence).Na nathubutu kusema , yule anaye shangilia tabia mbovu za baadhi ya wabunge wenye kutukana na kutumia maneno ya kudharirisha bungeni badala ya kuchangia agenda ni sawa mbumbu mbumbu hasiyejua kusoma na kuandika. Mwishowe wewe na huyo mbunge unayemshangilia hakuna hata chembe moja ya kumsaidia Mtanzania aondokane na umaskini. TOENI MAWAZO NAMNA GANI TUNAWEZA KUISAIDIA HII NCHI IONDOKANE NA UMASKINI , THAT IS OUR TOP AGENDA .WEWE KAMA MTANZANIA UNAPOAMKA ASUBUHI UMECHANGIAJE KUJISAIDIA WEWE MWENYEWE, FAMILIA YAKO ,NA NCHI KWA UJUMLA KUJIKWAMUA NA UMASIKINI? ask that question , what should you do to have a better a life ? Hayo mengine yote ni blaa blaaa tupu