WA-UKENYENGE
JF-Expert Member
- Oct 1, 2011
- 2,918
- 1,236
Na bunge ni sehemu nyeti sana ya nchi, tena yenye kutolea maamuzi mazito. Hii anatakiwa awajibike zaidi siyo kusema tu samahani. Pengine, iwe ndo mwanzo wa sheria kali dhidi ya watumia lugha chafu sehemu za public kama hizo.Mimi hainiingii akilini kwamba unatukana matusi ya nguoni kisha unaishia kuomba radhi tu basi!! Mtu unafahamu kabisa kwamba hili ni tusi lakini unaenda nalo kwa kujua tu kwamba nitasema samahani?!
Sasa bunge limegeuka kuwa kichaka cha watu kutukanana na kutukana. Demokrasia sasa inakuwa karaha.
Nilisema mwanzoni kabsa kuwa huyu jamaa mh; serukamba nmemskiliza ktk vkao vingi anajua kujenga hoja na ana busara sana ndio maana nilisema lazma ataomba radhi huyu ni bnadamu nazani kaptiwa...ila nawashangaa kina nkamia na waliosema watawapga maadui zao wakiwemo waandshi wawili wa habari kwa mkono wao mpaka leo hawajawaomba radhi watanzania....hongera sana serukamba tunataka vijana kama wewe...
Mkuu hapa sio facebookWajinga xana hawa wabunge,hopelec m uselec.
Naangalia bunge sasa hivi..Selukamba kasimama na kuomba radhi kwa maneno aliyotoa mchana.
Wenje nae kaomba muongozo kwa Ndugai..akirejea agizo la Makinda jana kwamba mbunge yoyote atakayetukana atatatolewa nje na polisi. Na anasema Selukamba katoa tusi kubwa kuliko matusi yote yaliyowahi kutolewa bungeni.
Ni matusi gani Selukamba katukana..mliosikia tafadhali mtujuze.
Ccm ni wendawazimu haswaa
Hahahaa, ni sawa na huku kwetu Sikonge, mtoto akiachia uchuzi wakati wa Chakula na anasema "Kimeniponyoka".
Ila kwa Kinyamwezi huwa ina-Sound vizuri sana. Sasa sijui yeye kaomba msamaha kwa lugha gani.
Kinyamwezi angelisema "Kanfyumpuluka......"
Kaunga , KIKUNGU , @ELNINO , St. Paka Mweusi ,na wengine mnasemaje? Nimepatia?