Bungeni: Serukamba aomba radhi

Bungeni: Serukamba aomba radhi

Ameomba Bungeni, Naibu Spika alitaka kumaliza. Wenje kamshikilia kwamba maelekezo ya Spika hayakuwa kwamba ukiomba msamaha ndo unaachwa. Amemtaka Naibu Spika aite polisi mara moja ili Serukamba atolewe. Atatoa majibu baadae

endelea kutuhabarisha, sisi wengine tupo mbali na tv
 
Hamna cha bahati mbaya. Wamezoea kujichanganya na watu wanaopenda matusi ndio maaana yapo nje nje.
 
Naangalia bunge sasa hivi..Selukamba kasimama na kuomba radhi kwa maneno aliyotoa mchana.
Wenje nae kaomba muongozo kwa Ndugai..akirejea agizo la Makinda jana kwamba mbunge yoyote atakayetukana atatatolewa nje na polisi. Na anasema Selukamba katoa tusi kubwa kuliko matusi yote yaliyowahi kutolewa bungeni.
Ni matusi gani Selukamba katukana..mliosikia tafadhali mtujuze.
 
CCM wamejisahau sana kwa wingi wao Bungeni,lakini ikumbukwe,Daudi alimuua Goliati.Tuombe tu uzima haya yana mwisho.Leo ni moja ya siku ambazo nimekereka sana
 
Hana mashiko. Sanasana ni kete dume kwa cdm
 
Wenje ameomba mwongozo ili serukamba awajibishwe na naibu spika kasema atatoa mwongozo muda sio mrefu.
 
Kwa hiyo asubuhi aliingia bungeni akiwa kanywa viroba?
 
Natumai Selukamba amepitiwa na mihemko...pole kwake ila atutake radhi, matusi aliyotoa ni makubwa sana.....
 
mh bahati mbaya wapi mtu akishazoea matusi hutukana ovyoovyo
lakini ustaarabu ukiwa nao kamwe huwezi kutukana kwa bahati mbaya kwa sababu hata tusi kuelea kichwani kwako haiwezekani.
Sawa kabisa. Utasikia mtu katembea na mama mkwe au shemeji au hg na kusingizia pombe, UONGO mtupu tamaa hujengwa kabla na pombe huwa kisingizio tu.
 
Tatizo la kulala Chako ni Chako kula bia na kuku ambao hawajaiva!! Mkiamka asubuhi bado mmevimbiwa kuku na pombe kichwani halafu badala ya kujadili mambo ya kitaifa mnaporomosha matusi. Aibu hii haitawatoka hawa wabunge!! Mtu mzima hovyo sana.
 
Ukizowea kujamba ukiwa pekee yako, huja siku ukasahau ukajamba mbele ya kadamnasi. Fundisho ni kuwa private na public lives zina tabia ya kuambukizana.
 
Bongo mtu anaiba mapesa ya epa akishakiri aliiba anaambiwa tulia hutotangazwa na hakuna hukumu we rudisha tu chini chini na taifa zima likakubaliana na hali hiyo. Je uzito wa tusi unaweza piku hii mpaka waadhibiwe? labda serikali nyingine sio hiii tunayoiona.
 
Back
Top Bottom