Bungeni: Muswada wa Katiba Unajadiliwa!

tundu; pendekezo la 12 limekubaliwa kama kambi ya upinzani ilivyopendekeza.
 
moja ya mapungufu ni kutokuwepo utoaji wa elimu juu ya mabadiliko ya katiba. na hii inaendeleza ujinga wa kutokujua kwa umma.
 
kambi ya upinzani inaunga mkono marekebisho ya kifungu cha 17.10. kambi lasmi ya upinzani sio kwamba inaunga mkono bali inatoa rai kwa wabunge wote kuungana na rais katika jambo hili. kamaliza kwa kusema "KWA MALA YA KWANZA NAUNGA MKONO HOJA".lissu.
 
Hadi makinda kampigia makofu na hoja imeungwa mkono. spika kasema hivi ndivyo inavyo takiwa, msisikilize maneno ya watu huko nje sijui ya kupigana. tunapokuwa humu Bungeni tofauti ya vyama tuiweke pembeni tuwe kitu kimoja hata wananchi inabidi wawe kitu kimoja. by makinda.
 
Tundu Lisu na Chadema wamfagilia kikwete bungeni, utadhani si hawa waliotoka nje wakidai hawamtambui... Hata hivyo ni ukomavu kisiasa, kumtambua Rais na nia yake njema ya kutaka nchi yetu ipate katiba nzuri kwa masilahi ya watanzania wote! Bravo Lisu, bravo Chadema kwa kuamua kula matapishi yenu... Mwendo mdundo
" Rais Kikwete ameonyesha uungwana na busara za hali ya juu sana, hakika ametoa muda wake mwingi kuhakikisha nchi yetu inapata katiba bora na safi kwa miaka ijayo, huu ni uzalendo na ukomavu mkubwa wa kiuongozi. Rais Kikwete anastahili pongezi"

Ni mtu mjinga tu ndie atakaeshindwa kuona matusi na madongo ya kiutu uzima aliyowapa Mh Lissu (Kikwete in general na wabunge wa magamba in particular)! Mtu mzima na mwenye busara hatukani hadi mtoto mdogo aelewe! Hapa hakuna ubishi, magamba wamechukua za uso.
 
Aliye anza kuchangia ni mh. Mnyaa.anasema; mala ya kwanza tuliupitisha mswaada huu japo ulikuwa na mapungufu. chama changu kilikuwa moja wapo ya vyama vilivyo enda kumuona rais. na mapendekezo yetu yalikubaliwa kwa asilimia 90. hata mimi naunga mkono hoja huu mswaada. naamin hakuna atakaye kataa kukubaliana na huu mswaada. nampongeza rais. kilicho nifurahisha ni kitendo cha makundi yote kukubalwa kushiriki. by Mnyaa.
 
mh mnyaa ampongeza jk kwa kukubali wanasiasa kuhusishwa kwenye tume ya katiba.... ni hatua kubwa sana. mwanzo hakuona kasoro hizo ? kiukweli mswada huu unawambua wengi san
 
Mnyaa;
kuna kitu chama changu kilipendekeza lakini sijakiona kwenye marekebisho ni asilimia 49.1 wakikataa na asilimia 50.9. wakakubali hiyo inapita wakati inakuwa ni kama sawa kwa sawa. sisi tulitaka katiba ikubaliwe kuanzia asilimia 60. na zanzibar walete majibu yao na bara walete majibu yao. by mnyaa
 
Anna kilango amfagilia tundu lisu amewasilisha vizuri. amesema baada ya mapendekezo kutolewa na vyama vya siasa yakishaletwa bungeni yanakuwa mapendekezo ya serikali na si ya vyama tena
 
ndani ya tumbo la shari kuna heri pia, eti wenzao waliokua hawamtambui rais jakaya kikwete sasa wanamtambua
 
Anna kilango anasema;
nakili kuwa na uhakika kwamba vyama vya siasa vilikwenda kumuona Rais. tundu lissu amewakilisha kistaraabu sana nampongeza.
Ni vyema watanzania wote wakaelewa hakuna mapendekezo ya ccm wala chadema bali ni mapendekezo ya serikali. ndani ya tumbo ya shari kuna heri pia. kuna wenzetu walikuwa hawamtambui rais wa tanzania. kwa shari hii imewezesha watu kutambua kikwete ndo rais wa tanzania. by kilango.
 
ndani ya tumbo la shari kuna heri pia, eti wenzao waliokua hawamtambui rais jakaya kikwete sasa wanamtambua maneno ya a6a kilango
 
kama waliweza kukaa ikulu na kutengeneza mabadiliko mazuri ya mswaada wa sheria ya tume ya katiba mpya kiasi hiki.kuna haja gani? Ya kuwa na bunge lisilo na memo mpaka watu wakutane ikulu.ok ni jema ila bado tunataka mgombea binafsi ata kama wameungana katika hili sisi raia hatutaki kufungwa na vyama.
 
Yes yes mambo safi sana............huku tulipo tabu maana Uganda umeme umekatika kwa hiyo Bukoba tupo gizani
 
kilango;
17c anaondolewa mkuu wa wilaya analetwa mkurugenzi. hawa ni watu wawili tofauti. mkurugenzi anasimamia maendeleo. dc ni mtawala wa ile wilaya.ndiye mwenye dola na mwenyekiti wa baraza la usalama. mwenye polisi ni mkuu wa wilaya. je tume ikienda usalama watautoa wapi?. huu ndo umuhimu wa mkuu wa wilaya kuliko mkurugenzi. kwani yeye ndo anadola na ni muwakilishi wa rais. mkurugenzi aondolewe sehemu zote anazo husika kwenye kifungu cha 17.(spika amemwambia hapo unaleta taarifa)
 
Back
Top Bottom