Lakini ninyi akina Kikwete, Chikawe na Membe, mumepokeaje fedha na hata kuzipangia malengo ikiwa fedha hizo hazikwenda huko kimakosa? Najua wengi tuna tatizo katika Logics na figures za syllogism, lakini hapa hata mtoto atajiuliza, hivi ni mfanyabihashara gani atakosea hesabu kiasi hicho, halafu akubali kurudisha fedha kwa kuambiwa tu? Na huyu mnunuzi aliwezaje kukaa kimya kwa makosa ya hesabu makubwa namna hii? Tunajua kununua Rada si sawa na kununua fungu la nyanya. Sasa nawaambieni, mkitaka kututawala kwa mabavu tuambieni tu, sio kucheza na akili zetu ambako hamuwezi, mnajiaibisha tu.