Bunge Letu Kila Mtu ana "Black Belt" kama Jackie Chan?

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Mar 10, 2006
33,475
39,991
Ukisikia watu wanasema sijui Magufuli anasema sana, anaropoka, hajali anachosema, ni mkali mkali, ujue wanamsingizia...

Hii si mara ya kwanza mimi kuandika juu ya hili. Na nina uhakika wapo watu wanajiuliza ni watu gani huwa wanaenda huko Bungeni. Wakati mwingine ukiangalia sana Bunge utadhani ni filamu ya Kichina au za Martial Arts kama Enter the Dragon, Fist of Fury, Crouching Tiger Hidden Dragon, au Kung Fu Hustle na The Drunken Master

fist_of_fury_R2_500_733.png

Kwenye filamu hizo mara nyingi - kama siyo zote - hata yule ambaye mwisho atapigwa hadi ashindwe kujitetea kuna wakati unaweza ukadhani na yeye ni stelingi Yaani kwenye filamu hizi kila mtu mbabe tu! Tatizo huwa linakuja mwishoni kabisa ambapo mtu ambaye alikuwa anazipiga vizuri kweli sehemu nyingine ati anashindwa kabisa anapigwa hadi anapepesuka mwenyewe! Unajiuliza huyu jamaa si na yeye alikuwa gangwe? Ndivyo ukiangalia kinachoendelea Bungeni wakati mwingine!

Embu angalia kama hutaona jinsi gani kila mmoja anajifanya (au anaamini) ana Mkanda Mweusi Ngazi ya Tano! (black belt fifth degree)

 
Ufala maanake ujinga,neno la kawaida tu kama mtu analeta ujinga kwenye mambo serious aambiwe tu
Maana ye Ndugai alinwambia Mdee "We nae hebu kikalishe hicho" sasa akikalishe nini??

Mwanakijiji we siasa zako za mtandaoni,ukiingia field ndio utajua lazima uwe kauzu kuwa upande qa upinzani Tz...Unyama unyamani tu!!
 
Ufala maanake ujinga,neno la kawaida tu kama mtu analeta ujinga kwenye mambo serious aambiwe tu
Maana ye Ndugai alinwambia Mdee "We nae hebu kikalishe hicho" sasa akikalishe nini??

Mwanakijiji we siasa zako za mtandaoni,ukiingia field ndio utajua lazima uwe kauzu kuwa upande qa upinzani Tz...Unyama unyamani tu!!

Matokeo yake ni kushindwa kwenye kura; kama hauna tofauti na wale unaotaka kuwaondoa kwanini watu wakuamini kukupa uongozi wa juu. Kama huo "unyama unyama" ukifanya na wao wakifanya "unyama unyama" kwanini ulie kuwa hawakutendei haki wakati na wewe hutendi haki?
 
Nitaendelea kusema, tunahitaji kupunguza wabunge wa CCM, ili kubalance bunge litawaliwe na hoja kwa hoja na si ushabiki.
Chama kinapokuwa na wabunge wengi hawawezi kujiandaa kujibu hoja kwani mwisho wa siku kura itawabeba kwa uwingi wao.
Mtaji wa wabunge wa CCM ni masikini walio vijijini, vyama vya upinzani nawashauri mkawaamshe huko. Mliwekeza sana kwa urais tu uchaguzi uliopita.

Kuna haja pia ya kufufua hoja bungeni ya mgombea ubunge binafsi, tukumbuke mbunge anawakilisha watu sio chama.

Jamani, haya yote yanayotokea leo sijui Rais na mchanga wa dhahabu, sijui demokrasia, sijui katiba, tatizo ni wabunge wa CCM, period.

Natamani kuliona bunge lenye hoja, inshaallah
 
Watu wanaotaka kuwa ultimatum kwenye mambo ambayo chanzo chake ni ubinyaji wa haki na usawa,hutetea tu mhuni anapojibiwa kihuni!!

Serukamba alitamka 'fukc you' na hatukuona uzi au lawama kwa kambi ya watetea watawala,wengine labda kwa kuwa neno hilo huko ughaibuni ni salam ya kawaida tu!

Lusinde Kibajaji huwa hachangii bila ya kutoa mipasho na mitusi kweli na hupangwa kimkakati,huishia kupigiwa makofi na vicheko vya spika. Wapo wengi.

Mfano alichokifanya spika ni upuuzi dhidi ya mtoa taarifa ambae alikuwa akisoma barua ya.bunge,spika alifanya vile kulinda uhuni tu wawagombea wa Lipumba na likely barua ya katibu ilikuwa imemuarifu kuwa pingamizi lake limepita,akaja kushangaa bungeni wakina Mnyaa wapo,spika akaspika!!
 
Jana katika mabishano ya namna ya kupiga kura mbunge wa Kawe, Halima Mdee alisikika akimwita Spika wa bunge kuwa "Fala". Kitendo hichi ni cha kukemewa kwa nguvu zote, ni utovu wa nidhamu wa hali ya juu, ni ujinga uliokithiri. Ndugai anaweza kuwa na umri wa kuwa Baba wa Halima. Pamoja na siasa zetu lakini vi vyema tukatumia lugha za staha na kuheshimu wakubwa!

Pili, lazima ujue kwa sasa wananchi hatutaki matusi. Tunataka kujenga hoja na kuleta maendeleo. Mimi kama mkazi wa Kawe kwa kweli umenidisapoint na kwa hakika kura yangu 2020 hupati.

Kama mwanamke lazima uwe na staha, ujiheshimu. Hao mambo ya kihuni yashapitwa na wakati. Kama ulifanya huko na kufurahisha watu NOT now. Kwa sasa tunataka wabunge wa kujenga hoja na sio vihoja..
 
Back
Top Bottom