Fue Fue
Senior Member
- Jan 6, 2013
- 107
- 128
BMK limesambaratika kimawazo na kivitendo baada ya kugawanyika vipande zaidi ya vitatu. Katika bunge hili kuna makundi haya matatu moja kundi linaundwa na vyama vya upinzani -Ukawa, kundi la CCM na kundi la washiriki tu.
Makundi haya yameleta msongo mkubwa sana wa mawazo kwa wananchi kwani yameshindwa kuafikiana hasa nini tuliwatuma dodoma.
Tuliipa fedha nyingi sana tume ya Jaji warioba kukusanya maoni, na wote kati ya makundi haya walishiriki kutoa maoni yao binafsi na kwa kikundi. Mkusanyiko wa maoni yale ndio wanatakiwa wayajadili. Ni mshangao tu kusikia kuna rasimu kadhaa Dodoma.
Katiba sio ya chama cha siasa wala kiongozi wa chama cha siasa. Busara ni wao kujadili maoni yetu ambayo tumewakusanyia. Wajenge hoja kama wanapinga maoni yetu wayapinge kwa hoja, kisha walete hoja zao kwetu tuzipigie kura sio kutunga rasimu nyingine ili wailete kwetu. Tumewatuma dodoma kujadili maoni yetu tu sio kupeleka rasimu zao ili wazijadili.
Bunge hili litatafuna kodi za watanzania na kumalizika bila ya katiba au katiba ya chama cha mapinduzi ambayo itatumika lumumba peke yake.
Kama chama cha mapinduzi kilitaka muundao wa serikali mbili, kwanini kilishindwa kutoa maoni yake ili yawe kwenye rasimu? Je si wanasema wapo wengi ilikuwaje uwingi wao haukuonekana kwenye maoni ya rasimu pale walipokuwa wanatoa maoni ?
Ombi bunge hili liahirishwe, tuunde tume ya uchaguzi huru, ili uchaguzi mkuu upite turudi kujadili rasimu.
Makundi haya yameleta msongo mkubwa sana wa mawazo kwa wananchi kwani yameshindwa kuafikiana hasa nini tuliwatuma dodoma.
Tuliipa fedha nyingi sana tume ya Jaji warioba kukusanya maoni, na wote kati ya makundi haya walishiriki kutoa maoni yao binafsi na kwa kikundi. Mkusanyiko wa maoni yale ndio wanatakiwa wayajadili. Ni mshangao tu kusikia kuna rasimu kadhaa Dodoma.
Katiba sio ya chama cha siasa wala kiongozi wa chama cha siasa. Busara ni wao kujadili maoni yetu ambayo tumewakusanyia. Wajenge hoja kama wanapinga maoni yetu wayapinge kwa hoja, kisha walete hoja zao kwetu tuzipigie kura sio kutunga rasimu nyingine ili wailete kwetu. Tumewatuma dodoma kujadili maoni yetu tu sio kupeleka rasimu zao ili wazijadili.
Bunge hili litatafuna kodi za watanzania na kumalizika bila ya katiba au katiba ya chama cha mapinduzi ambayo itatumika lumumba peke yake.
Kama chama cha mapinduzi kilitaka muundao wa serikali mbili, kwanini kilishindwa kutoa maoni yake ili yawe kwenye rasimu? Je si wanasema wapo wengi ilikuwaje uwingi wao haukuonekana kwenye maoni ya rasimu pale walipokuwa wanatoa maoni ?
Ombi bunge hili liahirishwe, tuunde tume ya uchaguzi huru, ili uchaguzi mkuu upite turudi kujadili rasimu.