Katika hali ya kusikitisha ni pale sisi wananchi tunapoambiwa na kiongoz flan wa serikali yako kuwa Bunge halitaonyeshwa livee. Kwakweli swala hili si haki kabisa kwetu sisi raia maana tutashindwa kuwasikia wabunge wetu wawapo bungeni wakichangia hoja kuhusiana na bajet naomba mh. rais ukiagize kile kikosi chako cha utafiti kikuletee taarifa kama ni kweli kurusha bunge live ni gharama kama ulivyoshauliwa.
Maana naona hiyo inaweza ikirudisha nyuma sana jitihada zako za kutumbua majipu na badala yake wale wasiopenda utumbuaji wako wa majipu kukurudisha nyuma kwa kuwafanya wananchi kutoona jinsi bajet yako ulivyoisukaa na namna serikali itakavyochukua hatua juu ya watafunaji wa pesa kulitia ripot ya CAG. Mh rais kwa heshma kubwa tunaomba uliangaliiee hili laweza likawa ni hujuma juu ya utawala wako.
Naomba waandishi wa habarr mtumie kalamu zenu na karasi kupigia kelele swala hili linalotukwaza sana sisi wananchi