Bukoba vs Moshi

Status
Not open for further replies.
Kah! mji wa Bukoba umekaa kama mahema ya wakimbizi......Una sura ya miji ya Afrika ya kati.
Bukoba itasubiri sana kuifikia Moshi.

Kabla ya Uhuru miji iliyokuwa mikubwa na ya mwanzo kujengwa ni Moshi na Tanga .....hii ni miji ambayo baada ya uhuru ilikuwa dormant sana .......hasa baada ya utaifishaji wa mashamba ikawa kama imekufa kwakuwa wakulima wakubwa wa Kahawa na Katani walioifanya miji hii kuwa maarufu waliondoka
Bandari ya Tanga miaka hiyo ilikuwa ina handle exports nyingi kuliko Dar es salaam .....,
Mji wa Moshi ndipo kulijengwa jengo la kwanza lenye lift afrika mashariki na watu walitoka hadi Nairobi kuja kula maisha Coffee Tree Hotel [KNCU].....
Miji ya ARUSHA ,DAR,MWANZA ilianza kuipiku miji ya Tanga na Moshi baada ya uhuru .
 
Wachaga wanatuzidi waTanzania wote akili ya kujenga kwao... wanatafuta pesa wanaimarisha kwao... wana ujamaa Sana
ndugu zetu wachaga kwa hill



sisi wengine tulifanikiwa tunajenga madale ,geza kibaha...
sasa makwetu wakaendeleze akina nani?!!! hapo ndipo tunaponyooshwa
 
Kuhusu mji wa Moshi kuwa dormant hilo ni kweli, lakini Bk haiwezi kufikia Moshi.
 
Wewe instanbul na wenzio mliotaka pictures za Moshi zimetosha mniambie sababu mlitaka wenyewe
Machame Route to the Mountain Kilimanjaro Huku ukifika ukiwa umefungwa macho badly enough uwe unatokea huko kanda ya ziwa utakana kabisa kama upo Tanzania

Tunapokea maelfu ya watalii daily wanaacha dollars paun euro na cash za kutosha wengine wamezamia huku tunaishi nao sasa huko bukoba hivi hata mnajua dollars nini au mnajua dollars ni vyombo vya usalama????
 
Kuhusu mji wa Moshi kuwa dormant hilo ni kweli, lakini Bk haiwezi kufikia Moshi.
Toka miaka ya 60 hadi sasa mji wa moshi ulidumaa sana at least kuanzia mwaka 2010 ndio kidogo wenyeji wameanza tena kujenga .......mfumo wa uchumi hasa Utaifishaji miaka ya 1960 ,Uhujumu uchumi 1980 ,ubinafsishaji etc ilifanya biashara kudorora na wenyeji wengi kuamua kuwekeza nje ya mkoa wa Kilimanjaro hasa mikoa ya Arusha,Mwanza,dodoma,Mwanza ........
Wakati mji wa Moshi wenyeji waliacha kujenga ...ukienda vijijini hali ni tofauti kwani hakuna hata nyumba moja ya Udongo kwa sasa .....nyumba za nyasi ziliisha miaka ya 90s ...na sasa karibu kila kaya ina nyumba self contained ...na wanashindana kumiliki ghorofa kila kaya ..hadi mabwawa ya kuogelea
Nyumba zilizoko milimani kilimanjaro ...zingejengwa mjini basi hakuna mji nchi hii ungefikia uzuri wa majumba ....kuna majumba mengi ya hadhi za masaki na mbezi yamejengwa huko milimani .
Kwa sasa taratibu wenyeji wanaanza kupata imani kujenga tena mjini .
 
Ulianza vizuri lakini mwishoni kama unapotosha, histoia inasema kuwa nyumba ya kwanza kuwa na lift Afrika Mashariki na Kati ni 'house of wonders' iliyopo Zanzibar!
 
Kama Moshi ni dormant basi hata sector ya utalii nchini ni dormant sababu Kilimanjaro inachangia zaidi ya 87% in tourism cash na sector ya utalii ndio ya pili kwenye kuchangia pato la taifa ikitoka kilimo
Kuhusu mji wa Moshi kuwa dormant hilo ni kweli, lakini Bk haiwezi kufikia Moshi.
 
Ulianza vizuri lakini mwishoni kama unapotosha, histoia inasema kuwa nyumba ya kwanza kuwa na lift Afrika Mashariki na Kati ni 'house of wonders' iliyopo Zanzibar!

basi umenifunza leo ...ila kitabu nilichosoma kilisema hotel ya kwanza ya lift afrika mashariki na mfumo wa maji moto ni Coffee Tree hotel ,iliyojengwa na Native Gorvernment ya Kilimanjaro ....ila kwa hili la zanzibar nakubaliana nawewe kwakuwa najua sio Tanzania tu bali Afrika ,Zanzibar inazo record nyingi ie street lights ziliwekwa zanzibar hata kabla ya London , TRENI YA KWENDA BUBUBU,televisheni ya rangi ya kwanza afrika , etc etc
 
Kama Moshi ni dormant basi hata sector ya utalii nchini ni dormant sababu Kilimanjaro inachangia zaidi ya 87% in tourism cash na sector ya utalii ndio ya pili kwenye kuchangia pato la taifa ikitoka kilimo
tunaamaanisha mji wa moshi ...na sio huko milimani ...kwenye njia za milima ambako pia yako mahoteli baadhi ...pamoja na kuwa Kilimanjaro ndio inaoongoza nchini kuipatia nchi mapato ya utalii ....kuna wakati mji wa moshi mahoteli yake mengi maarufu yalikufa ie Moshi hotel[livingstone] na wageni iliwabidi watokeee arusha kwenda kupanda mlima ...kwa sasa inaanza kupungua baada ya hoteli kuanza kujengwa tena mjini moshi ..na sasa moshi umekuwa ni moja ya miji ya starehe tanzania
 
Ila ukipitia mikondo ya historia fupi ya nchi yetu ni wazi 'maamuzi magumu' ya mwaka 1967 kutaifisha njia za uzalishaji na uhujumu uchumi kuna maeneo yaliathirika lakini Moshi, Bukoba na Tanga ni zaidi!
 
Ulaya Ulaya yani


Wakina David Beckham, Oprah, Angel Jolie, Chelsea lsea Manager na celebrities wengine wengi wameshafika.
 
Ila ukipitia mikondo ya historia fupi ya nchi yetu ni wazi 'maamuzi magumu' ya mwaka 1967 kutaifisha njia za uzalishaji na uhujumu uchumi kuna maeneo yaliathirika lakini Moshi, Bukoba na Tanga ni zaidi!
hili hata mwalimu alipokuwa anaaga alipoongelea maamuzi aliyajutia kwenye utawala wake alisema ni utaifishaji kuwa angepata fursa angeufanya kwa namna nyingine na alitoa mfano wa Tanga ....ni kweli hii mikoa imekuwa kwenye stagnization kwa zaidi ya miaka 50 na bahati mbaya wenyeji wa mikoa hasa Kagera ,Kilimanjaro ,Mbeya etc nao wakawa waoga ...kuwekeza kwao
pia Mwalimu alisikitikia Operesheni vijiji kuwa iliumiza baadhi ya watu na aliomba radhi.....hili ni jambo ambalo pia lilimtoa machozi RASHID KAWAWA alipokuwa anaaga .....aliomba radhi kwa operesheni vijiji .[ kuna watu waliondolewa sehemu zao za asili zenye rutuba na kupelekwa kwenye ukame ...au maporini ...wapo walioliwa na wanyama wakali ]
wakazi wa mikoa kama kilimanjaro wapo waliohamishiwa mikoa mingine na kwenda kuanza maisha mapya ie Morogoro
 
Kibosho Moshi vijijini

Hapo ni Kibosho kijijini lakini maji ni ya bomba safi na salama huku wanawake wanaobeba mitungi ya maji vichwani wamewaonea kwenye TV na visima huko ni msamiati.
 
Siku zote unapolinganisha vitu viwili ni lazima picha utoe zote na si za upande mmoja, tumeona picha za bukoba vp picha za mshindani wake? Weka picha hapo inaonekana umekuja na majib mfukoni!
 
Siku zote unapolinganisha vitu viwili ni lazima picha utoe zote na si za upande mmoja, tumeona picha za bukoba vp picha za mshindani wake? Weka picha hapo inaonekana umekuja na majib mfukoni!
Tafuta hata miwani ya mbao basi ili uone. Kiukweli nimeipitisha rasmi Moshi ni balaa aisee wachaga hongereni sana nimependa bure.
Bukoba utadhani Burundi bana teh teh teh wahaya msinipige mawe.
 
Status
Not open for further replies.
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…