Duh, Mkuu, 'Inamankusweke', naona unaanza kunitisha.
Sasa ngoja nami nikuulize swali hilo hilo: Wewe uamini wako katika vyombo hivyo unatoka wapi? Wewe ni mtaalam wa huko?
Duniani kote, nchi zote, hata hiyo DRC ukiwauliza juu ya vyombo vyao hivyo unavyonitishia navyo hapa watakwambia wao wako imara sana!
Kwa hiyo ninakuelewa unakosimamia. Hata mimi ningependa sana niwe upande wako, kwa sababu huo ndio wajibu wetu kama wazalendo wa nchi hii.
Lakini hili halina maana kwamba kuhoji na kuwa na mashaka, hasa kutokana na jinsi nchi yetu inavyozidi kuparaganyika, haina maana kwamba hatuitakii mema nchi yetu na kutopenda kuviamini vyombo vyetu hivi.
Hebu nijibu tu vizuri: Wewe wakati huu unayo imani kubwa juu ya Idara yetu ya Uhamiaji, kwa mfano. Kwa sababu maswala haya kama hili tunalochangia hapa sehemu kubwa sana linaanzia huko. Hao TISS na JWTZ kuingia kwao ni wakati hali imekwisha haribika kabisa, kama ilivyo sasa hivi huko Congo..