Breakthrough in Discovery of An AIDS Vaccine

Ndugu watanzania jana tu hapa nilitowa fikra za kulisaidia taifa na ulimwengu kwa ujumla, kwa kuitaka nchi yetu iweke sheria ya kuwatumia watu walio hukumiwa vifo badala ya kuwauwa wawe wanatumika katika Maabara kujaribia madawa yatakao vumbuliwa kwa kinga au tiba ya Binadamu, kwa mfano hawa wezetu wamevumbuwa chanjo hii na kama sisi tutavumbuwa aina ya madawa yatakao weza tibu binadamu wahukumiwa vifo wawe ndio wa kwanza kujaribia .

Chanjo ya HIV yapunguza maambukizi

t.gif
20080729173655_hivparticle_spl203cred.jpg

Chanjo imejaribiwa kwa wanawake na wanaume wasioathirika nchini ThailandWatafiti wanasema kwa mara ya kwanza chanjo ya UKIMWI iliyofanyiwa majaribio imeweza kupunguza uwezekano wa kuambukizwa virusi vya ugonjwa huo.
Chanjo hiyo ambayo ni mchanganyiko wa chanjo mbili zilizofanyiwa majaribio hapo awali, iligaiwa kwa watu 16,000 nchini Thailand.
Watafiti hao wamesema imepunguza kwa takriban theluthi ya hatari ya kuambukiza ukimwi, virusi vinavyosababisha ukimwi.
Imesifiwa kuwa ni hatua muhimu hasa katika nyanja ya kisayansi, licha ya kuwa chanjo hiyo bado ina safari ndefu ya kutumika duniani kote.
Utafiti huu ulifanywa na jeshi la Marekani na serikali ya Thailand kwa zaidi ya miaka saba kwa watu waliojitolea.
Watu hao waliojitolea walikuwa wanawake na wanaume wa kati ya umri wa miaka 18 hadi 30 katika maeneo yaliyoathirika sana na ugonjwa huo huko Thailand.


t.gif
20080729173655_hivparticle_spl203cred.jpg

Chanjo imejaribiwa kwa wanawake na wanaume wasioathirika nchini Thailand
 
sasa hiyo chanjo imeharibiwa kwa wanawake na wanaume wasioathirika ili ilete nini?
kuwa ukingonolize na muathirika usiambukizwe au ?
 
sasa hiyo chanjo imeharibiwa kwa wanawake na wanaume wasioathirika ili ilete nini?
kuwa ukingonolize na muathirika usiambukizwe au ?

Ndiyo maana ya chanjo mama wa kwanza. Lengo ni kuzuia usiambukizwe na wala si kutibiwa baada ya kuambukizwa.
 
Mbu, unakosea kidogo. Sio kwamba watu walivoluntia kuambukizwa, ni kwamba, unakwenda sehemu unayofahamu kuwa maambukizi ni makubwa, unawaeleza watu juu ya utafiti wako na wanakua huru kushiriki au kutoshiriki. Wale wanaokubali, wanagawanywa katika makundi mawili bila wao kufahamu. Kundi moja linapewa chanjo inayojaribiwa na jingine linapewa "kanyaboya", halafu unawaacha waendelee na maisha yao ya kila siku (wapo watakaoduu bila kinga na watakaotumia kinga kwa utashi wao wenyewe), siku ya mwisho unakuja kuwapima kupata idadi ya walioambukizwa katika kila kundi.
Hapo umenene kaudaktari upo kichwani nini,maana watu mnazaliwa na vipaji kama dr mmoja wa dispensary moja dar anatarajia kufanya mtihani wa QT mwaka huu lakini dr anaongoza kituo,
 
Habari njema sana hii,hope hawa capitalist hawatakuwa walafi kuichelewesha/spin ili watengeneze faida kubwa.
 
Mbu, unakosea kidogo. Sio kwamba watu walivoluntia kuambukizwa, ni kwamba, unakwenda sehemu unayofahamu kuwa maambukizi ni makubwa, unawaeleza watu juu ya utafiti wako na wanakua huru kushiriki au kutoshiriki. Wale wanaokubali, wanagawanywa katika makundi mawili bila wao kufahamu. Kundi moja linapewa chanjo inayojaribiwa na jingine linapewa "kanyaboya", halafu unawaacha waendelee na maisha yao ya kila siku (wapo watakaoduu bila kinga na watakaotumia kinga kwa utashi wao wenyewe), siku ya mwisho unakuja kuwapima kupata idadi ya walioambukizwa katika kila kundi.

...Ok, kwa hiyo nini maana ya matokeo ya utafiti wa mafanikio iwapo mtafitiwa alipewa chanjo ya kinga, halafu naye akajikinga kwa kutumia condom?
 
...Ok, kwa hiyo nini maana ya matokeo ya utafiti wa mafanikio iwapo mtafitiwa alipewa chanjo ya kinga, halafu naye akajikinga kwa kutumia condom?

Nice observation Mbu...if thats the case then it defeats the whole
purpose of 'trying out' the vaccine
 
Back
Top Bottom