BoT wajitafakari kabla ya kuwatuhumu Bloomberg

BoT wajitafakari kabla ya kuwatuhumu Bloomberg

Serikali ni malaymen wa uchumi aisei...
 
Kwa hiyo MCHUMI Malisa anataka kutuaminisha Tanzania inaelekea kwenye 'Hyper inflation? Kasomea uchumi chuo gani?
Kwenye currency, maduka ya kubadilisha fedha bei zikoje? Tsh 2500 za 'Bloomberg' ya Malisa & co, au 2,248?
Vijana wadogo mnajikita kwenye siasa za viwango vya chini mkizeeka lazima muwe wachawi.
Usiishie kutoa lawama tu kwa Malisa utendee haki uchumi wako tunahitaji inputs zako.
 
Fani ya akina nani, unaijua fani ya Malisa? changia mada iliyopo na sio kujua credentials za mwandishi jibu hoja kwa hoja.

siku zote watu wasiokua na hoja baadala ya ku-argue hoja wanakimbilia kumu-attack mtoa hoja sasa ww melisa umjue ili iweje??

kosoa point zake hapo kama unahisi anapotosha kama huna kausha
Hata wewe ni mbumbumbu wa maswala ya kiuchumi...
Huyo unaemtetea nimeacha kusoma aliposema tanzania ilipitia inflation ya sukari????? Inflation inapimwa kutokana na bidhaa nyingi..mchumi kuongelea inflation ya bidhaa moja ni kuonyesha hujui unachosema....Consumer Price Index (CPI) ni 'kikapu' na hakipimwi kwa bidhaa mojamoja in isolation..thats Ecos 101..alafu unadanganya Tanzania inapitia Hyperinflation na kuelekea Galloping inflation...upuuzi mtupu!!!!! niko barabarani nitarudi
 
Hata wewe ni mbumbumbu wa maswala ya kiuchumi...
Huyo unaemtetea nimeacha kusoma aliposema tanzania ilipitia inflation ya sukari????? Inflation inapimwa kutokana na bidhaa nyingi..mchumi kuongelea inflation ya bidhaa moja ni kuonyesha hujui unachosema....Consumer Price Index (CPI) ni 'kikapu' na hakipimwi kwa bidhaa mojamoja in isolation..thats Ecos 101..alafu unadanganya Tanzania inapitia Hyperinflation na kuelekea Galloping inflation...upuuzi mtupu!!!!! niko barabarani nitarudi
Mtaalamu hizo formula zako ukipiga unaona lini sukari itakuwa angalau 2000?
 
Hata wewe ni mbumbumbu wa maswala ya kiuchumi...
Huyo unaemtetea nimeacha kusoma aliposema tanzania ilipitia inflation ya sukari????? Inflation inapimwa kutokana na bidhaa nyingi..mchumi kuongelea inflation ya bidhaa moja ni kuonyesha hujui unachosema....Consumer Price Index (CPI) ni 'kikapu' na hakipimwi kwa bidhaa mojamoja in isolation..thats Ecos 101..alafu unadanganya Tanzania inapitia Hyperinflation na kuelekea Galloping inflation...upuuzi mtupu!!!!! niko barabarani nitarudi
Kasema kwa mfano sukari... mbona Lumumba mnakuja kwa jaziba tulieni si ndio nyie mlisema tuko kwenye vita ya kiuchumi vita yenyewe ndio hii kwanini mnaanza kulialia, mlibeep wenzenu wameanza kupiga.

CPI inapimwa kwa bidhaa mojamoja huku kila bidhaa ikiwa na uzito(weight) yake, huwezi kusema mafuta ya taa yana hadhi sawa na kilo ya unga kwa mlaji hivyo yawekwe kwenye kapu moja, hapana.
 
Mkuu pamoja na hoja yako ndefu unajua wakati Rais Magufuli anachukua madaraka mwaka 2015 uchumi wa Tanzania ulikuwa una hali gani na alikuta akiba za fedha za kigeni kiasi gani Benki Kuu.
Kimsingi pamoja na kila hujuma zinazofanywa na baadhi ya Tanzania kwa kutumiwa na vibaraka wa kiuchumi Tanzania itajikwamuua kiuchumi chini ya serikali ya awamu ya tano.
Kwa imani za nchi marafiki kwa serikali ya awamu ya tano wafadhili wanazidisha kutoa missada mingi kwa serikali hiyo ni dalili tosha kuwa serikali ipo kwenye njia sahihi kurekebisha uchumi wa nchi hii.
Nyie kama viongozi wa vyama vya upinzani msifurahie kuona nchi inakwamwishwa katika kujenga uchumi imara. Wekeni uzalendo kwanza badala ya maslahi ya vyama.
Thamani ya fedha ya Tanzania ipo vilevile kama Benki kuu ilivyotangaza nenda maduka ya kuchenji fedha upate uhalisia.
 
Hali ni mbaya xe. Com bado ni 2500!! Kweli kuongoza nchi si kuswaga ng'ombe
 
Mkuu pamoja na hoja yako ndefu unajua wakati Rais Magufuli anachukua madaraka mwaka 2015 uchumi wa Tanzania ulikuwa una hali gani na alikuta akiba za fedha za kigeni kiasi gani Benki Kuu.
Kimsingi pamoja na kila hujuma zinazofanywa na baadhi ya Tanzania kwa kutumiwa na vibaraka wa kiuchumi Tanzania itajikwamuua kiuchumi chini ya serikali ya awamu ya tano.
Kwa imani za nchi marafiki kwa serikali ya awamu ya tano wafadhili wanazidisha kutoa missada mingi kwa serikali hiyo ni dalili tosha kuwa serikali ipo kwenye njia sahihi kurekebisha uchumi wa nchi hii.
Nyie kama viongozi wa vyama vya upinzani msifurahie kuona nchi na kuunga mkono njama dhidi ya serikali ya awamu ya tano.
Msitafute visingizio kila kitu nyie mnahujumiwa, mnaambiwa shilingi imeshuka si kwa dola tu hata kwa Kshs nyie mnasema ni hujuma za Bloomberg, Bloomberg wahujumu shilingi ya Tanzania ili wapate nini kwanini wasihujumu Yen au Rupees zinazo trend vizuri na nchi zao zina biashara ya kuaminika waje wahujumu weak shilingi ya nchi masikini kama Tanzania.

Pambaneni na hali yenu hii ndiyo vita ya kiuchumi mlivyokuwa mnaitaka, if you can't stand the heat get out of the kitchen.
 
Msitafute visingizio kila kitu nyie mnahujumiwa, mnaambiwa shilingi imeshuka si kwa dola tu hata kwa Kshs nyie mnasema ni hujuma za Bloomberg, Bloomberg wahujumu shilingi ya Tanzania ili wapate nini kwanini wasihujumu Yen au Rupees zinazo trend vizuri na nchi zao zina biashara ya kuaminika waje wahujumu weak shilingi ya nchi masikini kama Tanzania.
Nenda Bureau de change ukaone au ukachenji uone rate ya dola badala ya blah blah nyingi
 
Nenda Bureau de change ukaone au ukachenji uone rate ya dola badala ya blah blah nyingi
That's local market we are talking about global market, mhindi wa Bombay anayekuja kununua mbaazi Mtwara hatouliza exchange rate kwenye duka la Manzese bureau de change ata check na rates za Bloomberg a well known, globally, trusted and reliable source.
 
Malisa ukienda sokoni physically hizo bei zako za mitandaoni hazipo kabisa.

Smilling haijashuka thamani.
 
Malisa GJ
________
Nimeona taarifa ya BOT ikikanusha kuwa sarafu ya Tanzania haijaporomoka, badala yake ni kwamba kuna watu kwenye financial software ya Bloomberg wameamua kuchezea data kwa makusudi kwa kuweka figure zisizo sahihi ili kupotosha. BOT wanasema kuwa tayari wameshawasiliana na Bloomberg ili kurekebisha makosa hayo.

Utetezi huu wa BOT una kasoro nyingi. Kwanza wanajitetea kuporomoka kwa shilingi dhidi ya Dola, lakini ukweli ni kwamba shilingi imeporomoka dhidi ya sarafu zote za kigeni na sio dola tu. Jana majira kama haya shilingi moja ya Kenya ilikuwa sawa na shilingi 21 za Kitanzania (bei ya kuuza), lakini leo shilingi moja ya Kenya ni sawa na shilingi 24.5.

Yani jana ulihitaji shilingi 21,000/= tu za Kitanzania kupata 1,000/= ya Kenya. Lakini leo ili upate 1,000/= ya Kenya unahitaji 24,500/= za kitanzania. Kwa hiyo shilingi yetu imeporomoka dhidi ya sarafu zote, sio dhidi ya dola tu kama BOT wanavyojaribu kueleza.

Pili nashauri BOT wajielekeze kwenye kiini cha tatizo badala ya kuficha tatizo. Kwanini wanajaribu kuficha? Kwa faida ya nani? Shilingi imeporomoka na hata waliotuma fedha leo ni mashahidi. Kwanini waseme data zimechezewa Bloomberg?
Njia rahisi ya kutatua tatizo ni kwanza kukiri kuwa lipo. Ukikataa tatizo huwezi kamwe kulitatua.

Moja ya sifa ya kuongoza taasisi za fedha ni kuwa mkweli katika kiwango cha juu kabisa, na kufanya mambo kwa nia njema sio kwa nia ya kufurahisha wanasiasa (Honesty and utmost good faith). Moja ya mambo yaliyofanya uchumi wa Uganda kuharibika vibaya na thamani ya sarafu yao kuporomoka sana ni Benki kuu ya nchi hiyo kukubali kutumika kisiasa. Idd Amin alikuwa akimuamuru Gavanor wa benki kuu nchini humo aseme uchumi upo imara hata pale mambo yalipokuwa magumu.

Anyway, kwangu taarifa hii ya kuporomoka kwa sarafu yetu ni jambo nililotegemea kulisikia. Pengine limeshtua watu kwa kuwa imekuwa ghafla sana na kwa kiwango kikubwa mno kuwahi kutokea katika historia ya nchi. Ndani ya masaa machache tu dola moja ya kimarekani imepanda kutoka shilingi 2,200/= hadi 2,500/=. Tumepoteza shilingi 300/= kwa kila dola moja ndani ya masaa machache.

Yani kwa mtu aliyetaka kutuma pesa nje ya nchi jana, letz say dola 5000, akachelewa na kutuma leo amepata hasara ya Shilingi milioni moja na nusu. Katika kila dola elfu moja amepata hasara ya laki tatu. Hali hii haijawahi kutokea tangu Tanzania ipate uhuru.

Zipo sababu kadhaa zinazoweza kuwa zimesababisha mporomoko huu mkubwa kabisa katika historia.

[HASHTAG]#Mosi[/HASHTAG]; ni mfumuko wa bei (Inflation rate). Kwa kaawaida mfumuko wa bei unapokuwa mkubwa, sarafu inapoteza ile nguvu yake ya manunuzi (purchasing power) na matokeo yake inaporomoka dhidi ya sarafu za nje. Hapa nchini mfumuko wa bei umeanza kutishia wanunuzi wa bidhaa mbalimbali. Kwa mfano wakati Rais Magufuli anaingia madarakani mwaka 2015 bei ya sukari ilikuwa shilingi 1,500/= hadi 1,800/= kiwa kilo, lakini leo bei ni kati ya shilingi 2,500/= hadi 3,000/= kwa kilo.

Mfumuko wa bei umekuwa kwa zaidi ya asilimia mia moja kwenye bidhaa ya sukari. Maana yake ni kwamba we are no longer at Moderate inflation, rather tunakaribia kwenye Hyper Inflation from Galloping one. Hali hii inasababisha sarafu yetu kuoporomoka kwa kiasi kikubwa.

[HASHTAG]#Pili[/HASHTAG]; ni kuwa na uchumi tegemezi wa knunua zaidi nje kuliko kuuza (import oriented economy). Tunaponunua zaidi nje maaana yake ni kwamba tunahitaji akiba kubwa ya fedha za kigeni. Tunapokuwa na demand kubwa ya fedha za kigeni maana yake pesa za kigeni zinakuwa na thamani kubwa kuliko sarafu yetu (the higher the demand the higher the price), na hivyo sarafu yetu inaporomoka. Na hii inaweza kuwa imecahangia sana kwa sababu ni kweli tunanunua zaidi nje kuliko tunavyouza.

Leo mtu akipata mtaji wa milioni 10, 20 anakimbilia China kwenda kuleta nguo, simu, saa, hereni etc. Thamani tunayouza nje ni ndogo sana kuliko tunayonunua.

Unaponunua zaidi nje unapunguza reserve ya pesa zako za kigeni na hivyo sarafu yako kuporomoka. Lakini unapouza zaidi nje unamaintain reserve ya pesa za kigeni na sarafu yako itapanda kwa sababu wanunuzi wa nje wataitafuta sarafu yako ili waweze kufanya purchase. Kabla BOT hawajabisha waangalie upya thamani tunayouza na kununua nje ya nchi ikoje (Balance of Payments).

[HASHTAG]#Tatu[/HASHTAG]: ni madeni ya serikiali (Government Debt). Serikali inapokopa sana nje inapunguza security ya sarafu yake. Ni sawa na nyumba yako uliyojenga kwa milioni 100, ukitaka mkopo wa haraka bank na wakajua una shida sana wanaweza kuithaminisha hata kwa milioni 70. Na wewe utakubali tu kwa sababu una shida. Mkopoo wowote unaokopa kwa sababu una shida saaana, led to undervalue your capital asset.

Sasa jiulize je Tanzania tumewahi kuwa kwenye shida kubwa saaana kiasi cha kukopa mkopo unaoweza kuwa umepelekea capital asset zetu kuwa undervalued? Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Ndugu Zitto Kabwe mwezi September mwaka huu, Taasisi ya fedha ya Credit Suisse ya nchini Uswisi, ilikiri kuikopesha Tanzania dola milioni 500 (karibu shilingi Trilioni 1.2) kwa masharti ya kulipa kwa miaka mitano, kwa riba ya karibu asilimia mia moja.

Mkopo huo ambao Tanzania inadaiwa kukopa kwa siri unatolewa na kundi mabenki (Syndicated loan) kupitia taasisi hiyo ya Credit Suisse uliibuliwa na Ndugu Zitto na Credit Suisse wakakiri kutukopesha, japo serikali ilikataa kutoa majibu ya tuhuma hizo. Kwa hiyo ikiwa taarifa hizi ni za kweli basi hii inaweza kuwa moja ya sababu ya sarafu yetu kuporomoka (A country with higher government debt is less likely to acquire foreign capital, leading to inflation and currency depreciation).

[HASHTAG]#Nne[/HASHTAG]; ni masharti ya biashara (Terms of Trade). Kwa kawaida kama masharti yako ya biashara ni magumu maana yake unafukuza wawekezaji na hivyo unapunguza kiasi cha fedha za kigeni ambacho kingekuja kwako. Tanzania tuna masharti magumu sana ya biashara kwa waeekezaji kutoka nje. Hivi majuzi tulitajwa kuwa nchi ya 137 kwa urahisi wa biashara dunian, huku Rwanda wakitajwa kuwa wa 41.

Maana yake ni kwamba wawekezaji wengi watakimbilia kuwekeza Rwanda badala ya Tanzania. Hata ada za usajili kwa wawekezaji Tanzania ni dola 250 wakati Rwanda ni dola 35. Sasa unategemea mwekezaji apeleke mtaji wake wapi? Wawekezaji wakipeleka mitaji yao Rwanda moja ya faida watakayopata wanyarwanda ni sarafu ya nchi yao kuimarika. Kwa hiyo kabla BOT hawajatoa tuhuma Bloomberg wapitie upya mashrti ya uwekezaji nchini.

[HASHTAG]#Tano[/HASHTAG]; ni matumizi holela ya fedha za kigeni ndani ya nchi. Unaporuhusu watu kufanya purchase kwa kutumia fedha za kigeni maana yake unapunguza nguvu ya manunuzi kwa sarafu yako, na matokeo yake sarafu yako itaporomoka.

Leo ukienda maduka makubwa utakuta watu wanafanya manunuzi kwa kutumia Dollar, Euro, British Pound etc. Na serikali ipo kimya tu. Inasubiri sarafu yetu iporomoke ije kukanusha kuwa kusema data zimekosewa huko Bloomberg, wakati ilipaswa kuchukua hatua mapema.

Jaribu kutembelea maduka makubwa kama Mlimani city, Rock city mall utakuta baadhi ya bidhaa zinauzwa kwa dollar. Yani mtu amebandika beji ya dola kwenye nguo anayouza na wala haoni ajabu. Ukienda anakwambia hiyo shati dola 20. Na viongozi wetu wanapita kwenye maduka hayo na wanafanya manunuzi wanaona huo ujinga na hawakemei. This is dolarization of Economy.

Nchi makini huwezi kukuta huu ujinga. Nakumbuka nilipokuwa Kenya kwenye hoteli niliyofikia nje kuna kuna duka la kubadilisha fedha. Kama umeenda na dollar zako au shilingi za kitanzania unabadilisha kwanza, unapewa pesa za Kenya ndio unaenda kulipa hotelini. Ukienda reception na pesa za kigeni hawapokei. Wanakushauri ubadili kwanza. Hii inaonesha namna walivyoi serious kulinda uchumi wao.

Hapa kwetu mtu akija dukani kwako akafanya manunuzi kwa dolar ndio unamuona wa maana, na kukenua meno yote bila kujua unaporomosha uchumi na kushusha sarafu ya nchi yako. Kwahiyo kabla BOT haijawasingizia Bloomberg ihakikishe kwanza inadhibiti matumizi holela ya pesa za kigeni kwenye manunuzi ya ndani. Pesa za kigeni zisiruhusiwe kabisa kwenye domestic market.

[HASHTAG]#Sita[/HASHTAG]; Ni hali ya kisiasa ya nchi (Political stability). Hali ya kisiasa inapokuwa nzuri inavutia wawekezaji wa kigeni kuja kuwekeza mitaji yao hapa na hivyo kuimarisha sarafu yetu (Increase in foreign capital, in turn, leads to an appreciation in the value of its domestic currency). Lakini hali ya kisiasa inapokuwa inatilia mashaka, wawekezaji wengi hukimbiza mitaji yao na hivyo kusababisha sarafu ya nchi kuyumba.

Hakuna muwekezaji anayependa kubughudhiwa na vyombo vya dola. Hivi majuzi tumeshuhudia magari ya Dangote yakifungwa cheni, hii inaweza kusababisha Dangote kuamua kufunga uwekezaji wake nchini ambao ni wa zaidi ya Dola Bilioni kadhaa. Ikitokea hivyo maana yake anahamisha mtaji, na moja ya athari zake ni kwenye kuporomoka kwa saraf yetu.

Lakini ukiacha Dangote, je hakuna wawekezaji wengine walibughudhiwa na kuamua kuhamisha mitaji yao? Kama wapo basi wameathiri sarafu yetu. Kwa hiyo kabla BOT hawajatupa tuhuma Bloomberg, ni vizuri wakaangalia hali ya kisiasa nchini kama inafavor wawekezaji na wakashauri serikali ichukue hatua zinaizofaa.

Zipo sababu nyingi, hizi ni baadhiu tu. Lakini hoja yangu ni kwamba BOT watafakari upya kabla ya kutupa tuhuma Bloomberg. Kuna mengi yamechangia kuporomoka kwa sarafu yetu zaidi ya hizo data kuchezewa huko Bloomberg. Tusifiche tatizo, tuliweke bayana na tusaidiane kulitatua. Tanzania ni yetu sote, tushirikiane kuijenga.

Malisa GJ
Wanasiasa wanacheza na akili za watanzania,binafsi sifahamu kwanini kila kitu kiendeshwe kisiasa badala ya kitaaluma,ndio maana kila kitu kinaporomoka, ni aibu kubwa sana nchi tajiri kama Tanzania watu wanakufa na njaa

Nafikiri tatizo kubwa katika serikali ya CCM ni kuendesha kila kitu kisiasa,wenye taalamu wa kitu fulani hawapewi uwezo,matokeo yake Profesor wa uchumi kama Lipumba anahangaika na siasa badala ya kuifanyia kazi taaluma yake...
 
That's local market we are talking about global market, mhindi wa Bombay anayekuja kununua mbaazi Mtwara hatouliza exchange rate kwenye duka la Manzese bureau de change ata check na rates za Bloomberg a well known, globally, trusted and reliable source.
Kwenye mitandao inategemea na denominator walitoweka. Inaonekana kunaweza kuwa na hujuma
 
PHD zmejaa sana pale BOT lakin wanakotupeleka mungu ndo anajua
 
Sio kila taasisi head of department anakuwa mwanasiasa wenzetu walishatoka huko,lazima professionalism iheshimike ili kesho tukikuhoji utupe mpaka majibu uliyo fundishwa mwaka wa kwanza!!leo unasema gavana wa BOT ni mwanasheria ila hakita haribika kitu kisa msaidizi wake ni mchumi harafu unasahau kuwa meno uliompa mkuu wa kazi!!sio kila mahali anatakiwa akae mpiga propaganda sehemu nyingine ni nyeti zinabeba maisha ya watu
 
Back
Top Bottom