Bosi wa Airbus kulipwa kifuta jasho cha Sh94.3 bilioni kwa kustaafu

Kanungila Karim

JF-Expert Member
Apr 29, 2016
20,744
25,446
PARIS,UFARANSA
Ofisa mtendajiu mkuu wa kampuni ya kutengeneza ndege ya Airbus anatarajiwa kuweka mfukoni dola 41 milioni ya kifuta jasho wakati atakapoachia ngazi wiki ijayo, kwa mujibu wa mahesabu yaliyofanywa na kampuni ya ushauri kwa wawekezaji na kutolewa leo.
Kampuni hiyo ilikubaliana na ukubwa wa ukokotoaji huo uliofanywa na Proxinvest, ambao ulitokana na taarifa za kifedha zilizokuwa zinajazwa chini ya utawala wa ofisa huyo mtendaji mkuu Mjerumani, Tom Enders.
Enders, 60, ataachia ngazi wakati wa mkutano wa wanahisa utakaofanyika Amsterdam, ambako ni makao makuu ya kampuni hiyo kubwa.
Malipo hayo hayatapigiw kura katika mkutano huo wa wanahisa, kama ilivyo kwa mwongozo wa viwango vya kampuni kubwa ambao uliimarishwa na chama cha waajiri nchini Ufaransa mwaka jana.
Kwa mujibu wa Proxinvest, Enders atapokea Euro 26.3 milioni kama malipo ya kustaafu kwa kipindi cha miaka 20 ijayo, pamoja na bonasi na malipo mengine yanayofikia Euro 7.3 milioni.
Pia atanufaika na kipengele kilicho kwenye mkataba wake kinachomzuia kufanya kazi na kampuni nyingine kwa mwaka mmoja ambacho kitampatia Euro 3.2 milioni
"Kipengele hicho kinagharimu fedha nyingi, miezi 12 inakwenda haraka sana," mkurugenzi wa Proxinvest, Loic Dessaint aliiambia AFP.
"Kama anataka kuwa mshauri wa kampuni nyingine katika kipinmdi cha mwaka mmoja na nusu, anayo haki," alisema.
Kwa ujumla, Enders atapata malipo ya jumla ya euro 36.8 milioni.
Donge hilo nono litaibua mijadala nchini Ufaransa, kutokana na serikali ya Ufaransa kumiliki asilimia 11 ya hisa kwenye kampuni hiyo ya kutengeneza ndege, huku Ujerumani ikimiliki asilimia 11 na Hispania asilimia 4.2.
Taarifa za vyombo vya habari zinadai kuwa Enders alitangaza kujiuzulu baada ya kutoungwa mkono na bodi mpya.
 
wengine kupata kifuta jasho au kiinua mgongo ni laki 3 tena wanazipata kwa mbinde
 
Anasubirikufa tu lamaana aandike urithi mapelmaaa

Hongera ZAKE HUKU WAZEE WETU wanazidi kufukuzwaaa watapangiwa KAZI ZINGINE
Sio kupangiwa kazi zingine, umesahau wale wastaafu wa EA walivyomwagiwa maji ya kuwasha baada ya kujaribu kufanya mkusanyiko wakidai stahiki zao kwa serikali ya ccm
 
Asipokua makini itaisha bila kujua. Pesa inatabia ya kutekenya na.inakuwasha uitumie tu. Matumizi hayana mwisho na hatatumia peke yake.

Narudia asipokua makini atastukia imeisha. Matumizi ya huko kwao nayo ni makubwa kwa siku
PARIS,UFARANSA
Ofisa mtendajiu mkuu wa kampuni ya kutengeneza ndege ya Airbus anatarajiwa kuweka mfukoni dola 41 milioni ya kifuta jasho wakati atakapoachia ngazi wiki ijayo, kwa mujibu wa mahesabu yaliyofanywa na kampuni ya ushauri kwa wawekezaji na kutolewa leo.
Kampuni hiyo ilikubaliana na ukubwa wa ukokotoaji huo uliofanywa na Proxinvest, ambao ulitokana na taarifa za kifedha zilizokuwa zinajazwa chini ya utawala wa ofisa huyo mtendaji mkuu Mjerumani, Tom Enders.
Enders, 60, ataachia ngazi wakati wa mkutano wa wanahisa utakaofanyika Amsterdam, ambako ni makao makuu ya kampuni hiyo kubwa.
Malipo hayo hayatapigiw kura katika mkutano huo wa wanahisa, kama ilivyo kwa mwongozo wa viwango vya kampuni kubwa ambao uliimarishwa na chama cha waajiri nchini Ufaransa mwaka jana.
Kwa mujibu wa Proxinvest, Enders atapokea Euro 26.3 milioni kama malipo ya kustaafu kwa kipindi cha miaka 20 ijayo, pamoja na bonasi na malipo mengine yanayofikia Euro 7.3 milioni.
Pia atanufaika na kipengele kilicho kwenye mkataba wake kinachomzuia kufanya kazi na kampuni nyingine kwa mwaka mmoja ambacho kitampatia Euro 3.2 milioni
"Kipengele hicho kinagharimu fedha nyingi, miezi 12 inakwenda haraka sana," mkurugenzi wa Proxinvest, Loic Dessaint aliiambia AFP.
"Kama anataka kuwa mshauri wa kampuni nyingine katika kipinmdi cha mwaka mmoja na nusu, anayo haki," alisema.
Kwa ujumla, Enders atapata malipo ya jumla ya euro 36.8 milioni.
Donge hilo nono litaibua mijadala nchini Ufaransa, kutokana na serikali ya Ufaransa kumiliki asilimia 11 ya hisa kwenye kampuni hiyo ya kutengeneza ndege, huku Ujerumani ikimiliki asilimia 11 na Hispania asilimia 4.2.
Taarifa za vyombo vya habari zinadai kuwa Enders alitangaza kujiuzulu baada ya kutoungwa mkono na bodi mpya.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Asipokua makini itaisha bila kujua. Pesa inatabia ya kutekenya na.inakuwasha uitumie tu. Matumizi hayana mwisho na hatatumia peke yake.

Narudia asipokua makini atastukia imeisha. Matumizi ya huko kwao nayo ni makubwa kwa siku

Sent using Jamii Forums mobile app

Unajidanganya, hivi unadhani mtu anayefikia kupewa bonus ya 90b alikuwa na mshahara kiasi gani?

Unadhani kwa mshahara aliokuwa anapata atakuwa hana investments?

Ndiyo maana hapo umeona ataendelea kulipwa ili asiende kufanya kazi kwingine kwa muda wa mwaka na nusu, means he is highly demanded.
 
... katika hiyo 94,300,000,000 kwa mfano tuchukulie 30% ni kodi na tozo mbali mbali.
... Atabaki na 94,300,000,000 x 0.7 = 66,010,000,000.
... Tuchukulie Mungu atamjalia kuishi miaka 100; so ana miaka 40 mbele (achana na ile 12.5 ya SSRA na kikokotoo uchwara).
... Kwa maana hiyo kila mwaka ana uwezo wa kutumia 66,010,000,000/40 = 1,650,250,000 sawa na T.Sh. 137,520,833.33 kwa mwezi
...au T.Sh. 4,584,027.78 kwa siku hadi anakufa bila kuhitaji kutumia akiba yake nyingine yoyote aliyojiwekea kipindi cha ujana wake. Duh!
 
Back
Top Bottom