Bora kumkimbiza Rais nchi nzima kuliko Mwenge

Bora kumkimbiza Rais nchi nzima kuliko Mwenge

Kaka Mtenga

JF-Expert Member
Joined
Feb 25, 2013
Posts
347
Reaction score
87
Samahani Wakuu,

Mimi napendekeza kuwa ni bora kumtembeza Rais wetu kila kijiji ajionee mwenyewe hali ya wananchi wake kuliko kuukimbiza Mwenge ambao hauna macho wala mdomo.

Rais anaweza kupata walau fursa ya kujibu maswali ya wananchi kwa kukumbushwa ahadi alizotoa wakati wa kampeni

Vile vile atapata fursa ya kukiaminisha chama chake kikongwe kwa wenye akili kongwe.
 
Ha ha ha.....We bwana we sijui uliwaza nini?
 
Kweli,mambo mengine kama safari Za ulaya amwachie makamu wake mpaka atalapo kamilisha hizo mbio Za raisi
 
nakubaliana nawe ila hadi amalize vijiji vyote atakuwa kazi zingine hafanyi.
 
Alishajikimbiza wakati wa kampeni, akimbizwe tena?
 
mkuu ni kweli,kwani faida ya mwenge mie siioni kabsa,zaidi ya kushusha taaluma ya wanafunzi wetu.kwani wanafunzi ndio hutumika zaidi kusafisha maeneo kwa ajili ya kukalibisha mwenge ana kupoteza ratiba ya masomo kwa muda wote wa kipindi cha maandalizi ugeni wa mwenge.wanachi hawajitokezi kabsa licha ya kupewa T-sheti na kofia ili kuja kuupokea mwenge.upelekwe kwenye makmbusho ya kitaifa tu,kwani hauna maana kabsa.
 
Samahani Wakuu,

Mimi napendekeza kuwa ni bora kumtembeza Rais wetu kila kijiji ajionee mwenyewe hali ya wananchi wake kuliko kuukimbiza Mwenge ambao hauna macho wala mdomo.

Rais anaweza kupata wala fursa ya kujibu maswali ya wananchi kwa kukumbushwa ahadi alizotoa wakati wa kampeni

Vile vile atapata fursa ya kukiaminisha chama chake kikongwe kwa wenye akili kongwe.
Mungu akubariki na akujaalie utajari wa duniani, Asante Mkuu umekuja na maono ya maana na mtazamo wako mema kwa jamii..... Tunakubaliana hili kwa pamoja na kupendekeza Rais JK atoe kipaumbele katika kutembea kote nchini ili atambue yanayowakabili wananchi uso kwa uso. Kwa sababu aliyowaakilisha hawatoi taswira halisi na repoti za uhakika na ukweli.Umasikini vijijini ni tishio kubwa na uzururaji mijini na ukosefu ajira ni TIMEBOOM linaweza ripuka na kuaathiri umma na taifakwa ujumla. mwenge huu ni change la macho!! halisaidii kitu isipokuwa USHIRIKINA na ubadhirifu wa mali ya walipa kodi. Nashukuru tena wakuu kulitambua hili. Kila la amani na jema kwa Taifa letu.
 
Samahani Wakuu,

Mimi napendekeza kuwa ni bora kumtembeza Rais wetu kila kijiji ajionee mwenyewe hali ya wananchi wake kuliko kuukimbiza Mwenge ambao hauna macho wala mdomo.

Rais anaweza kupata wala fursa ya kujibu maswali ya wananchi kwa kukumbushwa ahadi alizotoa wakati wa kampeni

Vile vile atapata fursa ya kukiaminisha chama chake kikongwe kwa wenye akili kongwe.
mwenge ni kitu kingine na rais ni kitu kingine, so kaa kimya
 
Samahani Wakuu,

Mimi napendekeza kuwa ni bora kumtembeza Rais wetu kila kijiji ajionee mwenyewe hali ya wananchi wake kuliko kuukimbiza Mwenge ambao hauna macho wala mdomo.

Rais anaweza kupata wala fursa ya kujibu maswali ya wananchi kwa kukumbushwa ahadi alizotoa wakati wa kampeni

Vile vile atapata fursa ya kukiaminisha chama chake kikongwe kwa wenye akili kongwe.

Ukisema rais unanichanganya mana mi namjua kwa jina la FASTJET ndo huyu unamwongelea? kama ndiye 100%
 
Afu gharama ya chakula cha raisi kila siku itakuwa nafuu kuliko gharama ya chakula cha mwenge kwa siku(mafuta).
Naunga mkono hoja pia.

afu atakuwa analala kwa mawaziri wake.
any way mleta mada ana wazo bomba sana!!! kila mwaka rais awe na ziara ya kila wilaya na mkoa tena hili wazo liwepo kwenye katiba.
safi sana!!!
 
mh rais wa tanzania anajua anachokifanya, ana wawakilishi kina kona ya nchi hii. mwenge ni alama ya taifa una umuhimu wake kwa taifa.
 
Back
Top Bottom