Boniface Mwabukusi: Si kila Kiongozi wa Dini ni Mtumishi wa Mungu

Boniface Mwabukusi: Si kila Kiongozi wa Dini ni Mtumishi wa Mungu

Safi sana. Na jamii yetu ipo kwenye mkanganyiko mkubwa kujua tofauti kati ya dini na Mungu. Dini ni man made system kumtafuta MUNGU. Mungu anamifumo yake ya kumtafuta mwanadamu. Utaona mtu kaishikilia dini yake kama kitu
cha maana kumbe ujinga tu
 
Kila wakili ni mwanasheria lakini sio kila.mwanasheria ni wakili

Nadhani hiwa ilo hivi

Mwabukusi ni mwanasheria na wakili
Hapepesi penye shida
 
Umesema uwongo bwashee,

unapenda sana kutukana uislam kireja reja,
Pole sana
 
Muwaoga saanaaaa, haya muishi milele duniani basi
 
Katika historia ya mwanadamu na hata katika maandiko matakatifu, ipo tofauti kubwa kati ya viongozi wa dini na watumishi wa kweli wa Mungu.

Ni muhimu kwa jamii kutambua kuwa si kila kiongozi wa dini ni mtumishi wa Mungu. Na si kila anayesema "Bwana, Bwana" ataingia katika Ufalme wa Mungu (Mathayo 7:21).

Tatizo kubwa linalojitokeza katika jamii zetu ni kwamba watu wengi huchanganya hawa wawili kana kwamba ni kitu kimoja.

Hii ni hatari, maana si kila anayevaa vazi la kidini au kusimama madhabahuni ni mjumbe wa Mungu.

1. Viongozi wa Dini ni wa mfumo – Watumishi wa Mungu ni wa kweli ya kiroho.

Viongozi wa dini mara nyingi wamejikita kwenye kulinda taasisi zao, mamlaka yao, na maslahi yao. Wanaweza hata kutumika kama vinyago vya nguvu za kisiasa au kiuchumi.

Katika Biblia, Yesu aliwakemea vikali Mafarisayo, Masadukayo na walimu wa sheria kwa unafiki na kupindisha sheria kwa manufaa yao binafsi:

"Ole wenu walimu wa sheria na Mafarisayo, wanafiki! Kwa kuwa mnafunga Ufalme wa Mbinguni mbele ya watu; ninyi wenyewe hamwingii, wala hamkubali wale wanaotaka kuingia waingie." – Mathayo 23:13.

2. Watumishi wa Mungu wamesimama na Haki, hata ikiumiza.

Watumishi wa Mungu, kama manabii wa zamani – Eliya, Isaya, Yeremia, na Yohana Mbatizaji – waliikemea jamii kwa uovu wake bila kuogopa. Hawakubembeleza mamlaka wala kukubali kununuliwa. Walikuwa tayari hata kufungwa, kuteswa au kuuawa kwa ajili ya kusimamia ukweli wa Mungu. Watumishi wa namna hii ni nadra sana leo.

3. Viongozi wa Dini hutafuta makundi – Watumishi wa Mungu hutafuta nafsi za watu.

Viongozi wa dini hujenga maelfu ya wafuasi lakini mioyo ya watu hubaki tupu. Wanahubiri kwa faida, wakigeuza watu kuwa chanzo cha kipato. Lakini watumishi wa Mungu hujenga watu, si majengo wala majina. Huduma yao huzaa toba, haki, na ukombozi wa kweli.

4. Hadithi za Mafarisayo na Masadukayo ni onyo la historia.

Yesu Kristo hakuwahi kuwa karibu na viongozi wa dini wa wakati wake. Aliwakemea kwa unafiki wao, kwa kutumia dini kama silaha ya kuwatesa wengine.

Hili ni onyo kubwa kwa vizazi vya sasa – kwamba dini isipotenganishwa na mamlaka ya kiroho, inaweza kuwa chombo cha uonevu na utumwa mpya wa kiakili na kiroho.

Tuwaangalie kwa matendo yao, si maneno yao. Na tuwaogope wale wanaoitumia dini kama kinga ya uovu wao.

Unapokwenda kwenye Nyumba za Ibada hakikisha akili yako ni Timamu.

BAK Mwabukusi.
Amepiga kwenye mshono wa homeboy wake
 
Kwa ni lazima kila mada atoe maoni?
 
Katika historia ya mwanadamu na hata katika maandiko matakatifu, ipo tofauti kubwa kati ya viongozi wa dini na watumishi wa kweli wa Mungu.

Ni muhimu kwa jamii kutambua kuwa si kila kiongozi wa dini ni mtumishi wa Mungu. Na si kila anayesema "Bwana, Bwana" ataingia katika Ufalme wa Mungu (Mathayo 7:21).

Tatizo kubwa linalojitokeza katika jamii zetu ni kwamba watu wengi huchanganya hawa wawili kana kwamba ni kitu kimoja.

Hii ni hatari, maana si kila anayevaa vazi la kidini au kusimama madhabahuni ni mjumbe wa Mungu.

1. Viongozi wa Dini ni wa mfumo – Watumishi wa Mungu ni wa kweli ya kiroho.

Viongozi wa dini mara nyingi wamejikita kwenye kulinda taasisi zao, mamlaka yao, na maslahi yao. Wanaweza hata kutumika kama vinyago vya nguvu za kisiasa au kiuchumi.

Katika Biblia, Yesu aliwakemea vikali Mafarisayo, Masadukayo na walimu wa sheria kwa unafiki na kupindisha sheria kwa manufaa yao binafsi:

"Ole wenu walimu wa sheria na Mafarisayo, wanafiki! Kwa kuwa mnafunga Ufalme wa Mbinguni mbele ya watu; ninyi wenyewe hamwingii, wala hamkubali wale wanaotaka kuingia waingie." – Mathayo 23:13.

2. Watumishi wa Mungu wamesimama na Haki, hata ikiumiza.

Watumishi wa Mungu, kama manabii wa zamani – Eliya, Isaya, Yeremia, na Yohana Mbatizaji – waliikemea jamii kwa uovu wake bila kuogopa. Hawakubembeleza mamlaka wala kukubali kununuliwa. Walikuwa tayari hata kufungwa, kuteswa au kuuawa kwa ajili ya kusimamia ukweli wa Mungu. Watumishi wa namna hii ni nadra sana leo.

3. Viongozi wa Dini hutafuta makundi – Watumishi wa Mungu hutafuta nafsi za watu.

Viongozi wa dini hujenga maelfu ya wafuasi lakini mioyo ya watu hubaki tupu. Wanahubiri kwa faida, wakigeuza watu kuwa chanzo cha kipato. Lakini watumishi wa Mungu hujenga watu, si majengo wala majina. Huduma yao huzaa toba, haki, na ukombozi wa kweli.

4. Hadithi za Mafarisayo na Masadukayo ni onyo la historia.

Yesu Kristo hakuwahi kuwa karibu na viongozi wa dini wa wakati wake. Aliwakemea kwa unafiki wao, kwa kutumia dini kama silaha ya kuwatesa wengine.

Hili ni onyo kubwa kwa vizazi vya sasa – kwamba dini isipotenganishwa na mamlaka ya kiroho, inaweza kuwa chombo cha uonevu na utumwa mpya wa kiakili na kiroho.

Tuwaangalie kwa matendo yao, si maneno yao. Na tuwaogope wale wanaoitumia dini kama kinga ya uovu wao.

Unapokwenda kwenye Nyumba za Ibada hakikisha akili yako ni Timamu.

BAK Mwabukusi.
Josephat Gwajima siyo mtumishi wa Mungu
 
Katika historia ya mwanadamu na hata katika maandiko matakatifu, ipo tofauti kubwa kati ya viongozi wa dini na watumishi wa kweli wa Mungu.

Ni muhimu kwa jamii kutambua kuwa si kila kiongozi wa dini ni mtumishi wa Mungu. Na si kila anayesema "Bwana, Bwana" ataingia katika Ufalme wa Mungu (Mathayo 7:21).

Tatizo kubwa linalojitokeza katika jamii zetu ni kwamba watu wengi huchanganya hawa wawili kana kwamba ni kitu kimoja.

Hii ni hatari, maana si kila anayevaa vazi la kidini au kusimama madhabahuni ni mjumbe wa Mungu.

1. Viongozi wa Dini ni wa mfumo – Watumishi wa Mungu ni wa kweli ya kiroho.

Viongozi wa dini mara nyingi wamejikita kwenye kulinda taasisi zao, mamlaka yao, na maslahi yao. Wanaweza hata kutumika kama vinyago vya nguvu za kisiasa au kiuchumi.

Katika Biblia, Yesu aliwakemea vikali Mafarisayo, Masadukayo na walimu wa sheria kwa unafiki na kupindisha sheria kwa manufaa yao binafsi:

"Ole wenu walimu wa sheria na Mafarisayo, wanafiki! Kwa kuwa mnafunga Ufalme wa Mbinguni mbele ya watu; ninyi wenyewe hamwingii, wala hamkubali wale wanaotaka kuingia waingie." – Mathayo 23:13.

2. Watumishi wa Mungu wamesimama na Haki, hata ikiumiza.

Watumishi wa Mungu, kama manabii wa zamani – Eliya, Isaya, Yeremia, na Yohana Mbatizaji – waliikemea jamii kwa uovu wake bila kuogopa. Hawakubembeleza mamlaka wala kukubali kununuliwa. Walikuwa tayari hata kufungwa, kuteswa au kuuawa kwa ajili ya kusimamia ukweli wa Mungu. Watumishi wa namna hii ni nadra sana leo.

3. Viongozi wa Dini hutafuta makundi – Watumishi wa Mungu hutafuta nafsi za watu.

Viongozi wa dini hujenga maelfu ya wafuasi lakini mioyo ya watu hubaki tupu. Wanahubiri kwa faida, wakigeuza watu kuwa chanzo cha kipato. Lakini watumishi wa Mungu hujenga watu, si majengo wala majina. Huduma yao huzaa toba, haki, na ukombozi wa kweli.

4. Hadithi za Mafarisayo na Masadukayo ni onyo la historia.

Yesu Kristo hakuwahi kuwa karibu na viongozi wa dini wa wakati wake. Aliwakemea kwa unafiki wao, kwa kutumia dini kama silaha ya kuwatesa wengine.

Hili ni onyo kubwa kwa vizazi vya sasa – kwamba dini isipotenganishwa na mamlaka ya kiroho, inaweza kuwa chombo cha uonevu na utumwa mpya wa kiakili na kiroho.

Tuwaangalie kwa matendo yao, si maneno yao. Na tuwaogope wale wanaoitumia dini kama kinga ya uovu wao.

Unapokwenda kwenye Nyumba za Ibada hakikisha akili yako ni Timamu.

BAK Mwabukusi.
Screenshot_20250705_202413.jpg

kama huyo kobazi hapo eti shekhe! m nina
 
Kweli kabisa
Kama wale masheikh waliondega kwa geodavie wakadai wao masheikh wa mkoa 😄
Mule kulikuwa na janja wengi
Kuna kama watatu walikuwepo mule tena mmoja alishawahi kuwa serikali ya mtaa kino mjini
Ila kwa sasa ni marehemu
Wako wengine nawajua wanatumika kupangwa kufanya cheating, na wanalipwa
Ila mwisho wa siku mambo ya kiimani yakikuingia ngumu kutoka
Wajinga waliwaooo

Ova
 
Mwabukusi na Lisu hawa ndio kina Martin Luther king Jr wa kizazi chetu
Hongo wanayoikataa na matisho wanayopewa wangekuwa na mioyo mepesi wangesha nyanyua mikono

Mwabukusi ni mtu mwenye heshima mbele za Mungu kuliko viongozi wengi wa kidini.
Naungana na wewe!
 
Back
Top Bottom