The Palm Beach
JF-Expert Member
- Dec 30, 2015
- 3,612
- 9,269
View: https://youtu.be/tfhpaLr7hBc?si=obXDytUPxizyrgqy
Advocate Boniface Mwabukusi, Rais wa TLS ameapa kuwa, mwisho wa watu Kutekwa na kuumizwa ni kwa Father Charles Kitima na Mdude Nyagali...
Amewataka Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Bwana Homera, RPC na RCO wahakikishe wanamrudisha Mdude Nyagali nyumbani kwake akiwa salama...
Mwabukusi anasema;
".Mdude Nyagali ni rafiki yangu kwa miaka 15 ni mtu mwema, hajamwibia mtu, hadaiwi na mtu. Adui wa Mdude Nyagali ni wale anaowakosoaga - serikali ya CCM. Hawa ndio ambao humsumbua na kumchukua au kumteka mara kwa mara na kwenda kumtesa huko na kisha kumwachia au kumtupa porini au mitaroni. Hawa wanajulikana kuwa ni polisi chini ya ofisi ya RPC na RCO wa Mbeya kwa amri ya Mwenyekiti wa kamati ya ulinzi na usalama ya Mkoa ambaye ni Mkuu wa Mkoa ambaye kwa Sasa ni Bw Homera. Wakati mwingine hutumwa Polisi kutoka DSM kwenda Mbeya kumdhuru Mdude Nyagali..."
Aidha alipokumbushwa kuwa RC Homera katoa na kutangaza zawadi ya TZS 5,000,000 kwa yeyote atakayempata Mdude, Mwabukusi amejibu;
"...Kwani Mdude Nyagali ana thamani ya Toyota Corolla mbovu? Hivi Mdude Nyagali binadamu unaweza kumlinganisha na milioni 5? Sisi kama ni milioni 5 tunayo. Tunachotaka ni wamrejeshe Mdude Nyagali akiwa hai, waache usanii na propaganda zao. Nasema hivi, waliomchukua Mdude Nyagali akiwa nyumbani kwake ni polisi, hivyo wamrudishe kwa njia ileile waliyomchukulia toka nyumbani kwake. Na kama wamedhuru, basi wamzae, na kumkuza na kisha kumrudisha nyumbani kwake. Hili tutahakikisha tunalisimamia kufanyika. Niko kwenye kikao, nikimaliza tu kikao wiki ijayo nakwenda Mbeya kulisimamia kuhakikisha wamemrejesha Mdude Nyagali. Na hii tabia ya kuteka na kuumiza watu badala ya kuwalinda yakome mara Moja. Tukio la Kitima na Mdude ndiyo yatakuwa matukio ya mwisho kwa watu Kutekwa na kuumizwa na wasiojulikana. Hii ni nchi yetu hatuwezi kuishi kwa hofu na mashaka kama vile hatuna mifumo na vyombo vya kulinda usalama wa watu na mali zao. Mbeya ndio itawafunua wasiojulikana wajulikane kwa kutumia matukio ya Mdude Nyagali na Father Charles Kitima...'
Looh, this is very bold and strong statement...!!