Bongo Movie mnashida gani?

Bongo Movie mnashida gani?

PharaohMtakatifu, hizo movie za zamani unazozisifia nazo hamna kitu, kwasababu ni tamthilia ndiyo maana unaziona zina uhalisia. Ukitaka kuamini kwamba hazina lolote, zingekuwa action movies ungejionea madudu.

Watanzania tunachoweza sisi ni tatmthilia (zile za kupiga stori vibarazani) siyo action movies. Movie zetu bajeti ni ndogo sana kwa action movies. Hata hizo tamthilia bado zina makosa sana, siyo kwa waigizaji wala maproducer, kote kuna makosa. Waigizaji hawana uhalisia kabisa na waongozaji utaona mwanga wa picha unaongezwa na kupunguzwa, sauti ya soundtrack iko juu kuliko maongezi. Mbaya zaidi movie karibia zote za siku hizi utakuta soundtrack zinafanana. Kwenye scene sasa, scene za huzuni wanaweka soundtrack za furaha, scene za adventure wanaweka soundtrack za huzuni.

Waandaaji wa filamu hapa TZ hawajui wanachofanya, maadam mkono uingie kinywani wanenepeane na wapate umaarufu mtaani basi imeisha hiyo. Hawana tofauti na wanasiasa wengi walafi, wajimilikishe wao tu basi imeisha hiyo.
Mkuu ni sawa lkn angalao zilikuwa Zina shawishi na kuonyesha maisha halisi ya jamii ya kitanzania

Movie kama Uncle JJ unaona kabisa Watoto wanavyoweza lisishwa uchawi. Angalia movie ya father James Jinsi kanumba alivyo mla sister na uhalisia wake ulivyo na jinsi jamaa alivyokuwa anapangilia matukio unaweza Angalia zaidi ya mara7 Bado huchoki!
 
Japo pia kuna issues nyingi sana ambazo zinakwamisha maendeleo bongo movie

-Wasimamizi husika .......hapa tumefeli kama nchi na industry kwa ujumla (National-personal level)

-Promotion

-Branding....hapa industry na wasaniii wenyewe (kwa wasanii wengi nadhani ni kwa sababu za kimaskini japo unaweza kuamua kujipa upekee bila pesa nyingi)

-Egoism n.k


Mambo ni mengi sana.

Sent from my SM-A107F using JamiiForums mobile app
Umeona mbali sana mkuu lkn Bado na wao wamepoteza ubunifu na ushawishi mtu anaona ni vyema aangalie za kikorea,kihindi nk!
 
Watafute story writers wakali

Watafute script writers wakali.

Selection ya wahusika na uhusika wao (kuna mtu anapewa role ya kuplay mpaka unashangaa walikosa mtu sahihi au ni uelewa mdogo kwa anayefanya hii selection?)

Budget.....Hapa ipo sehemu mbili, Budget ya movie na Budget za kununulia story....... (kama hawana watafute sponsors iwe ni nje au ndani ya nchi....kuna watu mpunga wanao na hawana pa kupeleka)

Kuna dada nilikutana naye akawa ananipa details za baadhi ya watu maarufu ambao wamemtapeli story zake na wamegoma kumlipa halafu anaona idea zake zinatumika kwenye movies zinazo rushwa live nilichoka.

Mtu kama Ray Kigosi anaweza kuwa moja ya watu ambao wanajua kuplay role wanazopewa kwa 100% huwa hakosei ila anaplay hiyo role kwa story ipi?

NB
Hata dialogue zinazowekwa kwenye story nyingi hazivutii kuziangalia mara mbili mbili.....Dialogue inaweza ikaifanya movie kuwa kali sana kama na story yake ni kali.

Kanumba alionekana kuwa beast kwenye industry kwa sababu jamaa alikuwa ni story writer hatari sana na alikuwa anajua hasa kuchagua actors sahihi na role ambazo wanatakiwa kuplay kitu ambacho kimewashinda wengi kwa sasa.

Kuna mengi sana ya kukaa kushauriana ila nani atakusikiliza? Wakubali kushauriwa na kupata ideas kutoka kwa watu ambao wapo nje ya zone yao sometimes.

Kuna actor mmoja niliwahi kumfuata nilikuwa na story moja kali mno na nilitaka nimpe bure kabisa .....nikashangaa kumbe inatakiwa nianze kubembeleza sana ndipo nisikilizwe nilibaki namshangaa.

Nilikaa naye kwa dakika 5 kuongea naye honestly kwa maelezo yake yalivyokuwa sikuwahi kurudi tena.



KUNA MUDA SANAA NI TAALUMA sio tu OCCUPATION.....watafute wataalamu wawasaidie

Sent from my SM-A107F using JamiiForums mobile app

Sent from my SM-A107F using JamiiForums mobile app
Upo sahihi kila ulichoandika ila kudai Ray ni mvaa uhusika mzuri nakupinga na nakupinga unavyosema Kanumba alikua writer mkali na mchagua xcter mzuri.

Sijaangalia bongo muvi za kuanzia kwa Kanumba mpaka mwaka huu hivyo majina sijui ya hizo muvi ila proof yangu mimi ni muvi moja Kanumba anazunguka na mshkaji huku yeye ana pistol akimuamuru kufanya vitu mbalimbali.

Muvi ya Kigosi ambayo itaprove ninachosema ni yupo na Sajuki wameenda kusoma nje halafu Kigosi anarudi ghafla kisa mkewe mgonjwa or something.

Kama kuna best movie unayoona ya hawa wawili itaje na unionyeshe strength iko wapi
 
Hawa jamaa miaka kama 12 sijawahi waangalia siku za Hivi karibuni nilitumiwa picha na wife akisema hili ni jini la bongo movie. Nikajua ni utani wa bibie.

Basi Kwa siku za Hivi karibuni nikasema Wacha Nami nishuhudie vioja Hivi vya bongo movie asee niliishia kulala tu hamna ujuzi wowote uliongezeka zaidi ya kupoteana na kupoteza mvuto kabisa.

Ile tamthiliya sikuijua hata jina japo waingizaji au waandaji wote ni wazoefu mle lkn kinachofanyika hakieleweki.

Zamani kwenye miaka ya 2007.... Ray kigos na Steve kanumba walikuwa wanafanya vizuri kweli.

Tamthiliya kama
More than pain
White maria
Big daddy
Uncle JJ
Magic house
Oprah
Dar to Lagos
Nk. Hizi Hadi waleo Huwa najikumbushia hakika huyu jamaa alikuwa anajua haswaa.

Pamoja na kukaa muda mrefu kwenye game walioachwa haajajifunza kitu.

Hii ndio picha niliyo tumiwa na wife akidai ni jini aliona kwenye tamthiliya kwenye bongo movie.

View attachment 2838222
Sasa jini la bongo siwange chukua hata picha ya samia tu ingetosha.
 
Uko sawa lkn wao ndo wameifanya kupoteza mvuto Kwa watazamaji.

Kwanza ikifika sehemu bila kwenda kitandani hivo story haijakamilika bila kiss denda nk Bado. Ikafika hata huwezi Angalia na familia Tena! Watu wakaanza kuangalia movie za ki Nigeria! Unakumbuka?


hata tatizo hilo linachangiwa na sisi, Mkuu Sex sales, ni rahisi kuuza story ya mapenzi au ngono kuliko drama nyengine yoyote, ndio mana nikasema sisi wenyewe ni part ya tatizo. TZ tuna population kubwa ila moja tatizo letu kubwa ni high number ya uncivilized people.
 
Ila bwana hayo yote sawa.

Ila kuna watu wanajitahidi sana sasa hivi...

Shout out to LAMATA na JIMMY wana tamthilia Tamu sana .....Jua kali ,Huba ,Kapuni na nyingine nyingi
Hakuna mtu makini au mwenye akili timamu anaweza kuangalia bongo movies
 
Hakuna mtu makini au mwenye akili timamu anaweza kuangalia bongo movies
😅😅🤣🤣🤣🤣🤣
Mkuu waigizaji wa Lamata wote Ni waigizaji Maarufu na ni watu wanaoheshimika sana kwenye jamii, Kwenye Juakali walishawahi kuigiza mawaziri humo waliomo madarakani na hata Watu waliokuwa Public figure wakubwa bado wanaigiza..

So ni chaguo lako tu mkuu..
Na mara nyingi watu wanaoponda bongo Movie ya sasa ni wale ambao hata Muvi za nje hawazijui zaidi ya Kikorea tu...
Watu tunaangalia movie zote Za nje ,Series zote za nje na nakuhakikishia kwa Ujuzi wangu wa kuangalia muvie almost asilimia 70% ya movie nyingi za sasa zinazotoka zina credibility ya ubora unao weza kufafanana na movie za nje..
Unless huangalii movie za nje
 
Upo sahihi kila ulichoandika ila kudai Ray ni mvaa uhusika mzuri nakupinga na nakupinga unavyosema Kanumba alikua writer mkali na mchagua xcter mzuri.

Sijaangalia bongo muvi za kuanzia kwa Kanumba mpaka mwaka huu hivyo majina sijui ya hizo muvi ila proof yangu mimi ni muvi moja Kanumba anazunguka na mshkaji huku yeye ana pistol akimuamuru kufanya vitu mbalimbali.

Muvi ya Kigosi ambayo itaprove ninachosema ni yupo na Sajuki wameenda kusoma nje halafu Kigosi anarudi ghafla kisa mkewe mgonjwa or something.

Kama kuna best movie unayoona ya hawa wawili itaje na unionyeshe strength iko wapi
Ray sio muigizaji ni mtopokaji
 
😅😅🤣🤣🤣🤣🤣
Mkuu waigizaji wa Lamata wote Ni waigizaji Maarufu na ni watu wanaoheshimika sana kwenye jamii, Kwenye Juakali walishawahi kuigiza mawaziri humo waliomo madarakani na hata Watu waliokuwa Public figure wakubwa bado wanaigiza..

So ni chaguo lako tu mkuu..
Na mara nyingi watu wanaoponda bongo Movie ya sasa ni wale ambao hata Muvi za nje hawazijui zaidi ya Kikorea tu...
Watu tunaangalia movie zote Za nje ,Series zote za nje na nakuhakikishia kwa Ujuzi wangu wa kuangalia muvie almost asilimia 70% ya movie nyingi za sasa zinazotoka zina credibility ya ubora unao weza kufafanana na movie za nje..
Unless huangalii movie za nje
Bob, mimi ukitaka tuzungumzie movies njoo tuzungumzie za Ulaya na Marekani. Movies and series. Ukitaka za Kibongo rudi miaka ya Kidedea walikuwepo waigizaji wenye kuigiza vizuri. Siangalii movies za Kibongo, Kinaijeria, kikorea, wale wa asia. Na pia hata za kizungu nachagua sana naangalia amhazo zina akili. So labda unataka tuanze na series? Nikutajie series ambazo nimeangalia since mwaka 1997 wakati huo tunaangalia VHS na pia tv shows kama Days of our lives?
 
Bob, mimi ukitaka tuzungumzie movies njoo tuzungumzie za Ulaya na Marekani. Movies and series. Ukitaka za Kibongo rudi miaka ya Kidedea walikuwepo waigizaji wenye kuigiza vizuri. Siangalii movies za Kibongo, Kinaijeria, kikorea, wale wa asia. Na pia hata za kizungu nachagua sana naangalia amhazo zina akili. So labda unataka tuanze na series? Nikutajie series ambazo nimeangalia since mwaka 1997 wakati huo tunaangalia VHS na pia tv shows kama Days of our lives?
Try me!
Mi Movie za nje naangalia sana mkuu,
Nimeanza pengine kabla yako kuangalia tumeanza kuangalia Movie kama Dragon ball ya mwaka 1989, Life goes on miaka hiyo ya 1990, American Gladiators miaka ya 94 ,..

Na kipindi hicho miaka ya 80 na 90 mwanzoni movie nyingi zilikuwa ni Comedy Themes movies na tulikuwa tunazipenda hivyo hivyo..
Muvie za serious zililkuwa Chache kama Dogie Howser ya mwaka 93 hiyo kipind ndo niko form six,

NAchotaka kukwambia kwa upande wa movie sidhani kama unaweza kunidanganya mkuu..
Africa movie zetu nyingi zimeanza miaka ya 92 na kuendelea kina Sarafina na zingine kibao ila miaka ya 98 na kuendelea ndo tulianza kukomaa sasa nchi yenye miaka ishirini na kitu kwenye movie huwezi kulingnisha na nchi yenye miaka zaidi ya 40 kwenye kiwanda cha movie
 
Try me!
Mi Movie za nje naangalia sana mkuu,
Nimeanza pengine kabla yako kuangalia tumeanza kuangalia Movie kama Dragon ball ya mwaka 1989, Life goes on miaka hiyo ya 1990, American Gladiators miaka ya 94 ,..

Na kipindi hicho miaka ya 80 na 90 mwanzoni movie nyingi zilikuwa ni Comedy Themes movies na tulikuwa tunazipenda hivyo hivyo..
Muvie za serious zililkuwa Chache kama Dogie Howser ya mwaka 93 hiyo kipind ndo niko form six,

NAchotaka kukwambia kwa upande wa movie sidhani kama unaweza kunidanganya mkuu..
Africa movie zetu nyingi zimeanza miaka ya 92 na kuendelea kina Sarafina na zingine kibao ila miaka ya 98 na kuendelea ndo tulianza kukomaa sasa nchi yenye miaka ishirini na kitu kwenye movie huwezi kulingnisha na nchi yenye miaka zaidi ya 40 kwenye kiwanda cha movie
Ukisema movies. Nimeanza angalia cinema toka miaka ya late 70s. Hapa Tz tulikuwa na sinema za akina yomba yomba. Unafahamu sinema za chale mnene na chale mwembamba? Unafahamu ni akina nani? Sasa nakutajia majina hayo ili uelewe si wewe kunitajia majina ya cinema ambazo uki google zitakuonesha ni za mwaka gani. Tv Series nimekwambia since 1990s mzee alikuwa anakuja na MIKANDA (VHS) so elewa dogo. Sisi tunazifahamu movies na tv series za miaka hiyo. SIWEZI ANGALIA BONGO MOVIES NI AFADHALI UNINYONGE
 
Ukisema movies. Nimeanza angalia cinema toka miaka ya late 70s. Hapa Tz tulikuwa na sinema za akina yomba yomba. Unafahamu sinema za chale mnene na chale mwembamba? Unafahamu ni akina nani? Sasa nakutajia majina hayo ili uelewe si wewe kunitajia majina ya cinema ambazo uki google zitakuonesha ni za mwaka gani. Tv Series nimekwambia since 1990s mzee alikuwa anakuja na MIKANDA (VHS) so elewa dogo. Sisi tunazifahamu movies na tv series za miaka hiyo. SIWEZI ANGALIA BONGO MOVIES NI AFADHALI UNINYONGE
Nafurahi kuitwa dogo!

Wewe kipindi hicho ulikuwa unaletewa na mzee wako ila mimi kipindi hicho nilikuwa nanunua mwenyewe kwa pesa nilizokuwa nazipata baada ya kufanya vibarua..

SInema nyingi Tanzania miaka hiyo zilikuwa ni Theatre Film ni za maonyesho tu ya ukumbi na hakukuwa na sinema za watanzania za kutazama kwenye viTV VYETU VYA JICHO MOJA ...
iliyokuwa even kina majuto na kina mzee small wameanza kuonekana kwenye Sinema miaka ya 97 ,98 hivi kina pwagu na pwaguzi na wengine wote walikuwa wanaigiza kwa njia ya Sauti kupitia Radio..

Muongo bhna we ulikuwa unaangalia Cinema wapi miaka ya 70s...

Nenda kamuuliza Baba yako (Ambaye yeye anaweza kukujibu) mikaKa hiyo Tanzania ilikuaje kwenye maswala ya kuangalia Sinema za nje au kutumia bidhaa za nje..

Kuna wakati unapojaribu kutetea kitu usiwe mbishi miaka ya 89 mwishoni na 90 hivii ndo namuona mzee wangu akichakarika kununua Tv na huku akinisomesha mimi Darasa la 14 mungu amrehemu aliko huko, baadaye ndo alikuwa wa kwanza kununua Tv nakumbuka kata nzima ndo baadae wengi nao wakanunua Tv...

Kunidanganya ni vigumu kwa sababu miaka hiyo nimeishi labda uniambie kuhusu Miaka ya 50s ndo sikuwepo ila miaka ya sabini na 80 na 90 sidanganyiki mkuu...

NB: mkuu point of correction huwa Sigoogle kitu ambacho sio tu Nakijua bali nimekiishi na nikuongeze tu Hatukuwa na VHS miaka ya 70,VHS ilianza kushamiri miaka 90 japo Miaka ya mwishon wa 80 kama 89 ilianza kuingia nchini..

NA HAKUNA MTU ANAKULAZIMISHA KUANGALIA BONGO Movies Nilichosema ni kwamba kuna Improvement kubwa sna ukilinganisha na tulipotoka
 
Nafurahi kuitwa dogo!

Wewe kipindi hicho ulikuwa unaletewa na mzee wako ila mimi kipindi hicho nilikuwa nanunua mwenyewe kwa pesa nilizokuwa nazipata baada ya kufanya vibarua..

SInema nyingi Tanzania miaka hiyo zilikuwa ni Theatre Film ni za maonyesho tu ya ukumbi na hakukuwa na sinema za watanzania za kutazama kwenye viTV VYETU VYA JICHO MOJA ...
iliyokuwa even kina majuto na kina mzee small wameanza kuonekana kwenye Sinema miaka ya 97 ,98 hivi kina pwagu na pwaguzi na wengine wote walikuwa wanaigiza kwa njia ya Sauti kupitia Radio..

Muongo bhna we ulikuwa unaangalia Cinema wapi miaka ya 70s...

Nenda kamuuliza Baba yako (Ambaye yeye anaweza kukujibu) mikaKa hiyo Tanzania ilikuaje kwenye maswala ya kuangalia Sinema za nje au kutumia bidhaa za nje..

Kuna wakati unapojaribu kutetea kitu usiwe mbishi miaka ya 89 mwishoni na 90 hivii ndo namuona mzee wangu akichakarika kununua Tv na huku akinisomesha mimi Darasa la 14 mungu amrehemu aliko huko, baadaye ndo alikuwa wa kwanza kununua Tv nakumbuka kata nzima ndo baadae wengi nao wakanunua Tv...

Kunidanganya ni vigumu kwa sababu miaka hiyo nimeishi labda uniambie kuhusu Miaka ya 50s ndo sikuwepo ila miaka ya sabini na 80 na 90 sidanganyiki mkuu...

NB: mkuu point of correction huwa Sigoogle kitu ambacho sio tu Nakijua bali nimekiishi na nikuongeze tu Hatukuwa na VHS miaka ya 70,VHS ilianza kushamiri miaka 90 japo Miaka ya mwishon wa 80 kama 89 ilianza kuingia nchini..

NA HAKUNA MTU ANAKULAZIMISHA KUANGALIA BONGO Movies Nilichosema ni kwamba kuna Improvement kubwa sna ukilinganisha na tulipotoka
Sijui kama kuna sehemu nimesema TV miaka hiyo ya akina Yombayomba. Hii nimeangalia home kama cinema. Siyo kwenye TV elewa tofauti yake. Ndo maana nimeshaelewa shida ipo wapi. Miaka ya 80s sisi tunaangalia sinema home. Ile mikanda inazunguka kama picha za negative. Mnaweka shuka jeupe ukutani. Sasa nimeelewa shida ipo wapi. Wewe endelea kuangalia bongoe movie bob.
 
Hawa jamaa miaka kama 12 sijawahi waangalia siku za Hivi karibuni nilitumiwa picha na wife akisema hili ni jini la bongo movie. Nikajua ni utani wa bibie.

Basi Kwa siku za Hivi karibuni nikasema Wacha Nami nishuhudie vioja Hivi vya bongo movie asee niliishia kulala tu hamna ujuzi wowote uliongezeka zaidi ya kupoteana na kupoteza mvuto kabisa.

Ile tamthiliya sikuijua hata jina japo waingizaji au waandaji wote ni wazoefu mle lkn kinachofanyika hakieleweki.

Zamani kwenye miaka ya 2007.... Ray kigos na Steve kanumba walikuwa wanafanya vizuri kweli.

Tamthiliya kama
More than pain
White maria
Big daddy
Uncle JJ
Magic house
Oprah
Dar to Lagos
Nk. Hizi Hadi waleo Huwa najikumbushia hakika huyu jamaa alikuwa anajua haswaa.

Pamoja na kukaa muda mrefu kwenye game walioachwa haajajifunza kitu.

Hii ndio picha niliyo tumiwa na wife akidai ni jini aliona kwenye tamthiliya kwenye bongo movie.

View attachment 2838222


Nsyuka
Shumileta
Roho Saba
Wameliacha mbali sana jini la twenti twenti tuu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom