Amba Samedi
Senior Member
- Apr 5, 2024
- 193
- 326
Habari wanaJF,
NIPO kwenye basi la Laviha inayotoka Dar kuelekea Ifakara. Tupo mkambarani tunakaribia Moro.
Sasa ameingia jamaa mmoja hivi na dawa ya meno ya Vigo Doctor. Akajitambulisha, shughuli ikaanza.
Alivyoishika mfuko wa bidhaa, akaelezea Aina zake na mabadiliko yaliyokuwepo. Akaelezea faida, na product inavyofaa watoto, watu wazima na wenye meno mabovu.
Akaelezea miswaki kwa ina yake, na mwisho akatoa ofa (mswaki na dawa kwa elfu 2)
Bwana ee! Abiria si wakamwagika. Miito ya "leta hapa" si ikawa mingi. Jamaa aliuza aisee.
Soko ni lugha, ni presentation skills, ni emotional connection. Kaka huyu alikuwa nazo zote.
Siku tukijifunza kuuza, fursa zitafunguka.
NIPO kwenye basi la Laviha inayotoka Dar kuelekea Ifakara. Tupo mkambarani tunakaribia Moro.
Sasa ameingia jamaa mmoja hivi na dawa ya meno ya Vigo Doctor. Akajitambulisha, shughuli ikaanza.
Alivyoishika mfuko wa bidhaa, akaelezea Aina zake na mabadiliko yaliyokuwepo. Akaelezea faida, na product inavyofaa watoto, watu wazima na wenye meno mabovu.
Akaelezea miswaki kwa ina yake, na mwisho akatoa ofa (mswaki na dawa kwa elfu 2)
Bwana ee! Abiria si wakamwagika. Miito ya "leta hapa" si ikawa mingi. Jamaa aliuza aisee.
Soko ni lugha, ni presentation skills, ni emotional connection. Kaka huyu alikuwa nazo zote.
Siku tukijifunza kuuza, fursa zitafunguka.