Bomu la wanafunzi litaiangusha hii serikali!

Bomu la wanafunzi litaiangusha hii serikali!

Mwingereza

JF-Expert Member
Joined
Jan 21, 2014
Posts
1,115
Reaction score
2,771
Tunakokwenda siyo. Maelfu ya wanafunzi wamekosa mikopo, wako mitaani na bila shaka watalazimika kuandamana kudai haki yao ya msingi, yaani Elimu. Polisi watatumia nguvu nyingi kuwanyamazisha, ila haitawezekana, kwa maana kwamba wananchi nao watawaunga mkono. Na hili swala litakuwa ni tatizo ambalo halitazimika kamwe.

Nadhani serikali iangalie hili swala la mikopo kwa wananfunzi kwa jicho la pili. Hili ni bomu na tishio kubwa sana kwa huu utawala
 
Nini maana ya mkopo????
It means ni pesa unayopewa uitumie alaf baadae utairejesha....
Sasa serikali mbona inawanyanyasa wanafunzi kana kwamba ni pesa ya msaada?????
Tatizo lako umeuliza nini maana ya mkopo, halafu hukujibu, halafu unaendelea na porojo
 
Tunakokwenda siyo. Maelfu ya wanafunzi wamekosa mikopo, wako mitaani na bila shaka watalazimika kuandamana kudai haki yao ya msingi, yaani Elimu. Polisi watatumia nguvu nyingi kuwanyamazisha, ila haitawezekana, kwa maana kwamba wananchi nao watawaunga mkono. Na hili swala litakuwa ni tatizo ambalo halitazimika kamwe.

Nadhani serikali iangalie hili swala la mikopo kwa wananfunzi kwa jicho la pili. Hili ni bomu na tishio kubwa sana kwa huu utawala
Nilishasema tatizo ya hili suala ni wanafunzi kutoambiwa maana ya cost sharing.
 
Tunakokwenda siyo. Maelfu ya wanafunzi wamekosa mikopo, wako mitaani na bila shaka watalazimika kuandamana kudai haki yao ya msingi, yaani Elimu. Polisi watatumia nguvu nyingi kuwanyamazisha, ila haitawezekana, kwa maana kwamba wananchi nao watawaunga mkono. Na hili swala litakuwa ni tatizo ambalo halitazimika kamwe.

Nadhani serikali iangalie hili swala la mikopo kwa wananfunzi kwa jicho la pili. Hili ni bomu na tishio kubwa sana kwa huu utawala
Haki ya kusomesha inaanza kwa mzazi,mkopo haujaandikwa popote kwenye katiba,serikali haiwezi kuanguka kwa siasa hizi nyepesi.Somesheni watoto kwa pesa yenu,serikali inawajibu wa kujenga miundombinu ya elimu acheni kujisahau
 
Tatizo LA mikopo ni pale serikali inaposema mtakatwa kwenye mishahara 8% or 15%. Sasa kama hana mshahara utamshitaki kwa kosa gani?
 
Wee kapime akili yako naona INA shida kubwa sana
Hiyo mikopo ni sehemu ya miundominu ya elimu
Kukojoa ukojoe wewe,utegemee mwanao asomeshwe kwa mkopo wa serikali,watapata wenye vigezo kwa 100%,wengine kakopeni benki msomeshe wanenu,mmebweteka na kuona kama vile lazima,ile ilikua juhudi ya serikali kuingiza wanafunzi kwa wingi.Sasa kuna UDOM,MUHAS,UCLAS na UDSM vinatosha kabisa kufikia malengo ya serikali
 
Kukojoa ukojoe wewe,utegemee mwanao asomeshwe kwa mkopo wa serikali,watapata wenye vigezo kwa 100%,wengine kakopeni benki msomeshe wanenu,mmebweteka na kuona kama vile lazima,ile ilikua juhudi ya serikali kuingiza wanafunzi kwa wingi.Sasa kuna UDOM,MUHAS,UCLAS na UDSM vinatosha kabisa kufikia malengo ya serikali
Hongera baba
 
Sio kubweteka ila angalia kua ni kipato gani ambacho mzazi mkulima anacho cha kuweza kumsomesha mtoto bila kupewa mkopo
Ilihali serikali inamkopa hata mazao yake so kiujumla hana pesa
Kama kwenu mnazo usiwadharau wasionazo brooo
Ukiongelea mkulima awe masikini sikuelewi,mtu anavuna hadi gunia 500 za mahindi au mpunga unasema huyo ni masikini?
 
Tatizo LA mikopo ni pale serikali inaposema mtakatwa kwenye mishahara 8% or 15%. Sasa kama hana mshahara utamshitaki kwa kosa gani?
Haufahamu ulichoandika,
1. kwa hio ulitaka kukopeshwa halafu usilipe?

2. Wote wanaokopeshwa wanatakiwa kuwa na mishahara?

3. Sasa kama wakopeshwaji hawana mishahara kwa nini wanataka kukopa?
 
We ndo hufahamu ulichoandika. Mwanafunzi anaekopeshwa kusoma ana mshahara? Wee lazima ccm.
 
Haki ya kusomesha inaanza kwa mzazi,mkopo haujaandikwa popote kwenye katiba,serikali haiwezi kuanguka kwa siasa hizi nyepesi.Somesheni watoto kwa pesa yenu,serikali inawajibu wa kujenga miundombinu ya elimu acheni kujisahau
Andaeni mazingira mema ili walipa kodi wanufaike na kodi wanayo katwa,mshahara kiduchu biashara ndogondogo mnauwa sasa hawa watanzania wanasomeshaje wakati ada vyuo vya serikali ziko juu huyo mkulima mnamsaidiaje mbona mnakinzana na maneno ya mwasisi wa ccm
 
Back
Top Bottom