Return Of Undertaker
JF-Expert Member
- Jun 12, 2012
- 4,572
- 26,892
TAIFA LINAVUJA DAMU!
Na Bollen Ngetti
NAWASALIMU marafiki zangu wote kwa matumaini kuwa hamjambo. Ukimya wangu unawaumiza wengi wenu na kuwafurahisha wachache wenu. Ninapitia kipindi kigumu sana kiusalama kwa hiyo nafasi inapopatikana ndipo tunaweza kutafakari kama sasa.
Hali ya mambo nchini kwa sasa ni ya kukatisha tamaa na hakuna maneno matamu zaidi Taifa kuvuja damu. Nimetafuta mchora picha anichoree Tanzania inayovuja damu nimekosa ndio maana andiko hili halina picha.
Ndugu zangu, miezi kadhaa niliandika nikionya kuwa njaa yaja nikabezwa mno na mkuu wa nchi akasema "hakuna chakula cha bure" na ole wake DC ataayegawa chakula. Sasa huko Shinyanga baa la njaa ni tete na wanagawiwa chakula cha bure. Tulipuuza maonyo, Taifa linavuja damu.
Uchaguzi wa Serikali za Mitaa umekuja ukapita kama upepo na laana juu. Hakuna waliochaguliwa wala hakuna waliopiga kura. Wababe wamejitangazia ushindi. Taifa linavuja damu. Vijana wamekata tamaa si tu kushiriki siasa lakini hata maisha. Taifa linavuja damu.
Rais anasema huko Udom kuna watu wanamkatisha tamaa lakini hatokata tamaa. Lakini amesahau kuwa ni wateule wake ndio Mayuda Isariote wanaomsaliti kwa tamaa ya kushibisha matumbo yao. Tunaona Mkurugenzi wa moja ya mkoa kanda ya ziwa akishinda Kigamboni kuporomosha mahekalu ukimuuliza anakwambia JPM rais wa wanyonge. Taifa linavuja damu.
Niseme kidogo kuhusu Yuda aliyekuwa mwanafunzi wa mwisho kuteuliwa na Bwana Mkubwa lakini malengo yake yakiwa ni kutengeneza faida si uzalendo wa kiimani ndio maana ikawa rahisi kumuuza Yesu kwa fedha. Hawa mayuda yamemzunguka Magufuli wanaotumia umaarufu wake kutengeneza faida si kutumikia umma. Wanamsaliti Magufuli. Ndege yetu inakamatwa Canada wanamdanganya bosi wao. Taifa linavuja damu.
Miradi inayotatiza uchumi inajengwa bila ridhaa ya umma kupitia bunge sawa na baba anayejenga tiles kila mahali lakini watoto wakilala njaa. Taifa linavuja damu.
Tundu Lissu amegoma kurudi nchini akihofia kuuawa. Demokrasia imetoweka nchini Tanzania. Taifa linavuja damu.
Gharama za maisha imepanda kila mahali hadi washirikina wanalia. Taifa linavuja damu. Viongozi wa dini ambao wangeponya Taifa nao wanavuja damu. Mbele ni kiza kinene. Hata hivyo,
#AchaWoga2020
Na Bollen Ngetti
Na Bollen Ngetti
NAWASALIMU marafiki zangu wote kwa matumaini kuwa hamjambo. Ukimya wangu unawaumiza wengi wenu na kuwafurahisha wachache wenu. Ninapitia kipindi kigumu sana kiusalama kwa hiyo nafasi inapopatikana ndipo tunaweza kutafakari kama sasa.
Hali ya mambo nchini kwa sasa ni ya kukatisha tamaa na hakuna maneno matamu zaidi Taifa kuvuja damu. Nimetafuta mchora picha anichoree Tanzania inayovuja damu nimekosa ndio maana andiko hili halina picha.
Ndugu zangu, miezi kadhaa niliandika nikionya kuwa njaa yaja nikabezwa mno na mkuu wa nchi akasema "hakuna chakula cha bure" na ole wake DC ataayegawa chakula. Sasa huko Shinyanga baa la njaa ni tete na wanagawiwa chakula cha bure. Tulipuuza maonyo, Taifa linavuja damu.
Uchaguzi wa Serikali za Mitaa umekuja ukapita kama upepo na laana juu. Hakuna waliochaguliwa wala hakuna waliopiga kura. Wababe wamejitangazia ushindi. Taifa linavuja damu. Vijana wamekata tamaa si tu kushiriki siasa lakini hata maisha. Taifa linavuja damu.
Rais anasema huko Udom kuna watu wanamkatisha tamaa lakini hatokata tamaa. Lakini amesahau kuwa ni wateule wake ndio Mayuda Isariote wanaomsaliti kwa tamaa ya kushibisha matumbo yao. Tunaona Mkurugenzi wa moja ya mkoa kanda ya ziwa akishinda Kigamboni kuporomosha mahekalu ukimuuliza anakwambia JPM rais wa wanyonge. Taifa linavuja damu.
Niseme kidogo kuhusu Yuda aliyekuwa mwanafunzi wa mwisho kuteuliwa na Bwana Mkubwa lakini malengo yake yakiwa ni kutengeneza faida si uzalendo wa kiimani ndio maana ikawa rahisi kumuuza Yesu kwa fedha. Hawa mayuda yamemzunguka Magufuli wanaotumia umaarufu wake kutengeneza faida si kutumikia umma. Wanamsaliti Magufuli. Ndege yetu inakamatwa Canada wanamdanganya bosi wao. Taifa linavuja damu.
Miradi inayotatiza uchumi inajengwa bila ridhaa ya umma kupitia bunge sawa na baba anayejenga tiles kila mahali lakini watoto wakilala njaa. Taifa linavuja damu.
Tundu Lissu amegoma kurudi nchini akihofia kuuawa. Demokrasia imetoweka nchini Tanzania. Taifa linavuja damu.
Gharama za maisha imepanda kila mahali hadi washirikina wanalia. Taifa linavuja damu. Viongozi wa dini ambao wangeponya Taifa nao wanavuja damu. Mbele ni kiza kinene. Hata hivyo,
#AchaWoga2020
Na Bollen Ngetti