Bodi ya TRA kwanini haijavunjwa, Bade kaonewa?

Bodi ya TRA kwanini haijavunjwa, Bade kaonewa?

Hii bodi inajua kuwa siku zao zinahesabika. Magufuli ataivunja tu. anasubiri ripoti yake. Baada ya hapo. kaput.
 
Hahaha JK anakuwa mis led na kila mtu amekuwa kichwa cha mwendawazimu? ? Tukubali tu JK hakujali ilimradi interest zake haziguswi.

Jamaa ametulostisha sana kwa kweli
 
Akili ya kawaida kabisa Mtendaji Mkuu unashughulikiwa kwanza kwa upuuzi uliopo.Walio juu yako wasio watendaji wanafuata baada ya uthibitisho. Utetezi wa kupungua au kuongezeka kwa wizi in wa kipuuzi. Wizi/ukwepaji kodi dawa yake kuumaliza si kuupunguza. Wezi hawataisha lakini wadhibitiwe,wasilelewe.
 
Kwani kuna mahali Bade ametuhumiwa kuhusika na skendo Fulani moja kwa moja?

Ulifunguliwa waraka na PM kama anatambua namb za hizo kontena , akaonyeshwa idadi ya containers 349 zilizopotea, akakiri kuzitambua na aka ahidi thamani yake yote itarudi!
- Kama alikuwa akilifahamu hili, alichukuwa hatua gani kabla?
-Je, waziri mkuu asingeenda pale, hizo jitihada za kuyatafuta zingeanza lini au ndiyo ingekuwa imetoka?

Bado mambo yanaendelea hapo TRA, pengine lipo ndani ya mkakati wa JPM, naona ni mapema mno tukihukumu ukizingatia kamishna wa sasa anakaimu! Umesikia pia leo wamepewa siku kadhaa waelezo mali na madeni yao!

Tuwe wavumilivu tu kwa sasa, vile mimi naona!
Lakini pia ukumbuke, uwezo wake wa kufuatilia ulikuwa na umbali gani?

Tunapouliza maswali lazima tuangalie kwa upana wake. Hivi Kamishna akitoa kimemo, itakuwaje!

Ukisoma maelezo ya The Boss utaona ni vurugu tupu. Kamishana anateuliwa na Rais, wajumbe wa Bodi wanateuliwa na Rais, wapo wajumbe wanateuliwa na bodi ili wafanye kazi na mteule wa Rais ingawa mhusika ametetuliwa na Bodi

Hapa kwa kamishna kuna mengi, kama angeamua kumwaga mtama tungeona yasiyotakiwa.
 
Last edited by a moderator:
Kuna uzi niliweka hapa kuhusu kina nani wanafaa ku run economy hivyo Magufuli amteue mmoja wao...katika list hiyo alikuwepo Rishad Bade.....sasa baada ya skendo la makontena TRA baadhi ya watu wamekuwa wakiniuliza kama Rishad Bade nilikosea kumtaja katika list hiyo na mwingine ni Harry Kitilya.Sasa wakati natafakari yaliyotokea TRA.

Hapa JF kuna uzi wa mkuu R.B wa mwaka 2013, kwenye huu uzi kuna mambo yamejitokeza yamenishangaza sana.

https://www.jamiiforums.com/jukwaa-...-kwa-tuhuma-makontena-kupotea-mikononi-2.html

Kumbe bodi ya TRA inateua watendaji na ilimteua Masamaki huku akiwa tayari ana tuhuma za kupotea ka makontena mengine.Nna sio hilo tu kamati ya bunge ililiona hilo na kuihoji Bodi kwa maamuzi hayo mtu mwingine ambae nae inaonekana bodi ya TRA ilimteua ni Blandina Nyoni.

Sasa kama bodi kwanza ina nguvu hivyo ya kuteua watendaji halafu pili watendaji wenye tuhuma tayari...ilikuwa ni busara kumuwajibisha Kamishna wakati mamlaka kamili ya kuteua watendaji wa chini yake yako bodi,na bodi imeachwa kama ilivyo?

Pili hii structure ya TRA ambapo kamishna anateuliwa na Rais na naibu pia na Rais halafu watendaji wa chini yake wanateuliwa na bodi nani ali design hii?

Inawezekana kweli kamishna akawa na nguvu TRA huku anateuliwa watu? na mamlaka ambazo ziko juu yake? Rais na Bodi?

Na kama hizi tuhuma sio mpya labda uchunguzi ungefanyika wa mda mrefu wa tatizo hili? kontena zimepungua kupotea au zimezidi baada ya Bade kuteuliwa?

What if zimepungua sana despite the fact hana nguvu kuliko Bodi?

Why bodi iteue watuhumiwa?

Je, wajumbe wa bodi ya TRA wanachunguzwa?wamehojiwa? why bodi haijavunjwa?

Ikidhihirika Bade alikuwa hahusiki kabisa na alikuwa anapambana na 'powerful forces' kumaliza hilo tatizo atarudishwa? Ataombwa radhi kwa kuchafuka?

Aisee...hili nalo neno
 
Bade no mhujumu uchumi full stop..haina haja ya kuulizana maswali ya kitoto umu na kujifanya una logic thinking capacity kubwa kuliko rais aliyemsimamisha kazi
 
Ajabu leo Magufuli kavunja bodi ya TPA na kmfukuza mkurugenzi
wakati bodi ya TRA bado ipo....
 
Lakini pia ukumbuke, uwezo wake wa kufuatilia ulikuwa na umbali gani?

Tunapouliza maswali lazima tuangalie kwa upana wake. Hivi Kamishna akitoa kimemo, itakuwaje!

Ukisoma maelezo ya The Boss utaona ni vurugu tupu. Kamishana anateuliwa na Rais, wajumbe wa Bodi wanateuliwa na Rais, wapo wajumbe wanateuliwa na bodi ili wafanye kazi na mteule wa Rais ingawa mhusika ametetuliwa na Bodi

Hapa kwa kamishna kuna mengi, kama angeamua kumwaga mtama tungeona yasiyotakiwa.



Sasa leo kwa kesi hoyo hiyo TPA kavunja bodi na kumuondoa mkurugenzi
while TRA bodi hajaivunja
 
Sasa leo kwa kesi hoyo hiyo TPA kavunja bodi na kumuondoa mkurugenzi
while TRA bodi hajaivunja


hiyo bodi lazima anairudia... huyu ndie magufuli..

anaefata sijui nani.. nahisi anaetutesa watanzania kwa mgao wa umeme....

maana style ya kutimua tu hii sio mchezo
 
Sasa leo kwa kesi hoyo hiyo TPA kavunja bodi na kumuondoa mkurugenzi
while TRA bodi hajaivunja
Kuna kusita sita na ugumu. Ndio hasa msingi wa kuuliza endapo Kamishna alikuwa 'mzembe' au kuna maeneo yasiyotakiwa kuguswa. Hili suala lina tatizo ambalo halipo wazi
 
Kuna kusita sita na ugumu. Ndio hasa msingi wa kuuliza endapo Kamishna alikuwa 'mzembe' au kuna maeneo yasiyotakiwa kuguswa. Hili suala lina tatizo ambalo halipo wazi

Bila kuangalia structure ya haya mashirika ni bure kabisa
watafukuza kila mtu
umeona ya TPA?
'kaimu' mkurugenzi katimuliwa
jiulize 'kaimu' mkurugenzi anaeomba awe confirmed ataweza kweli kukataa maagizo na vimemo
vya wizara na bodi?

Sasa leo wamemtimua huyo kaimu pamoja na bodi na katibu mkuu
 
Bila kuangalia structure ya haya mashirika ni bure kabisa
watafukuza kila mtu
umeona ya TPA?
'kaimu' mkurugenzi katimuliwa
jiulize 'kaimu' mkurugenzi anaeomba awe confirmed ataweza kweli kukataa maagizo na vimemo
vya wizara na bodi?

Sasa leo wamemtimua huyo kaimu pamoja na bodi na katibu mkuu
That's the point. Kila siku tunasema jamani structure nzima haihakikishi kama tupo njia sahihi. Si kufukuza tu, bali tunaishia kupata viongozi waliofeli kuongoza taasisi kubwa kama bunge. Tumeona fast track ya mheshimiwa na jinsi alivyoingizwa mjengoni kwa FedEx kama si DHL

Tunasema bila kuangalia mfumo mzima, mh ata feli muda si mrefu.
Mashabiki hawataki kusikia neno hilo kabisa. Wanataka tushangilie hata kama tunaona tatizo.

Mfumo mzima upo nyang'anyang'a halafu tunaambiwa unasafishwa.

Hivi gari iki noki injini suluhu ni kufanya nini, overhaul ya injini au kusukuma na kubadilisha madereva wanaoshtua wakatai tunatoka jasho kusukuma
 
Nimepitia thread nyingii humu naona the boss una defend bade n kama hurithishwi na utendaji wa magufuli..nahisi unapersonal interest na bade haiwezekani ukawakila siku unamkingia kifua au unajua container zilipo unaanza kujitetea kupitia jf..mwache raisi apige kazi utajua mwisho wa bodi ya tra linii..#hapakazi tu
 
The Boss
Hewalaa, kwamba kaimu akatae kimemo hata cha naibu waziri!

Tunasikia wameamua kumuweka speed governor.
Wanajua vimemo vikiibuka itakuwa aibu kuu

Ndio mana tumeuliza saa , hivi kmishna wa TRA kwleli angeklia majina tu kwa garama za kibarua chake




Na kwavilehatuna mfumo, watapeta tu na mtu mzima kunywea

 
Last edited by a moderator:
Sasa leo kwa kesi hoyo hiyo TPA kavunja bodi na kumuondoa mkurugenzi
while TRA bodi hajaivunja
Unataka Raisi wa JMTZ aongoze nchi kwa matakwa yako? Yaani wewe unavyoona ni sawa basi na Raisi aone hivyo hivyo? Wewe lazima utakuwa ni narcissist!
 
The Boss
Hewalaa, kwamba kaimu akatae kimemo hata cha naibu waziri!

Tunasikia wameamua kumuweka speed governor.
Wanajua vimemo vikiibuka itakuwa aibu kuu

Ndio mana tumeuliza saa , hivi kmishna wa TRA kwleli angeklia majina tu kwa garama za kibarua chake




Na kwavilehatuna mfumo, watapeta tu na mtu mzima kunywea

mkuu Nguruvi3 kuna kitu watu hatukioni na wala hatujui hasara zake

Kwa sababu mfumo umeoza na watu wengi wakiingia wanajikuta hawana namna
na hii ya sasa ya ku target watu zaidi badala ya mfumo

hasara kubwa tutakayopata ni wale watu 'very decent na very qualified'
kukataa teuzi za aina hii kwa hofu ya kuchafuka
hiki hatukitazami sana lakini mwisho ni kuwa Rais anaweza jikuta
anao watu 'aina ile ile tu available'

Kwa sababu kama mfumo hauruhusu watu kung'aa inavyostahili
na unapelekea watu kuchafuka...wale ambao tunawahitaji
ambao ni 'very decent na very qualified' watafikiri mara mbili kuingia serikalini
wakati they can go anywhere in the world....
 
Last edited by a moderator:
Bade wakati rais JP aliita wafanya biashara alikuwepo, kumweka pembeni ni kumlinda ili asijulikane ndio mtoa siri, usisahau huyo jamaa alikua anamsuport nani kwenye kampeni,
 
Back
Top Bottom