Bodi ya ATCL yaivunja Menejimenti ya Shirika hilo

Bodi ya ATCL yaivunja Menejimenti ya Shirika hilo

Baada ya Bodi ATCL kuitumbua Managementi ya ATCL, muda sio mrefu Bodi nayo itatumbuliwa na waziri husika au Rais mwenyewe.

Hapa kutumbuana tu.
 
Kuna jambo bado sijaelewa kabisa, yaani ya Bodi ya ATCL inapanga mpaka ruti za ndege, Kuchunguza mawakala wa ATCL, kupima utendaji wa mameneja, kuratibu ratiba za ndege kama zinafuatwa, kufuatilia tiketi za bure nk.
It is too local and Primitive.
Nini kazi ya Management ya ATCL sasa?
 
serikali si familia..ukitaka wale uwapendao wewe tu ndio wachukue nafasi..basi wewe ni mbaguzi kuliko chura.
Yaani kama Mbowe vile anataka kila kona weke MTU wa Kilimanjaro na hasa machame na Rombo
 
Sawa kabisa.You can't train an old dog new tricks.
Habari zilizonifikia ni kuwa Menejimenti ya Shirika la Ndege ATCL imevunjwa ili kukidhi vigezo na haja za Shirika hilo na malengo yaliyowekwa kwa miezi 8.

Imeamuliwa Wakurugenzi Wote na baadhi ya Mameneja waondolewe mara moja (Isipokuwa Mtendaji Mkuu aliyeajiriwa hivi karibuni) hatua hiyo imechukuliwa kwa sababu mbalimbali ikiwemo utendaji dhaifu, viwango hafifu vya elimu kinyume na matakwa ya nafasi hizo na uadilifu.

Aidha wakurugenzi na Mameneja waliokuwa wakikaimu nafasi mbalimbali imeamriwa warudishwe kwenye ngazi zao za chini.

Bodi imemuagiza Mtendaji Mkuu atangaze nafasi za Wakurugenzi, Mameneja na nafasi nyingine atakazoona zinafaa kutafutiwa wafanyakazi wapya.



=======
UPDATE

Hata hivyo hatua zaidi zitachukuliwa kwa mawakala wa kukatisha tiketi kwakuwa utaratibu uliokuwepo hakuangalia maslahi ya shirika na ikithibitika hakuna ulazima wa kuwatumia mawakala basi kutakuwa na zoezi la kubatilisha mikataba ya mawakala na kuwatumia wafanyakazi wa Shirika.



Mwenyekiti wa bodi ATCL amedai shirika lilikuwa linakopa sana zamani na sasa wachofanya ni kulipa madeni ya zamani



Wamesema wamepunguza sana matumizi yasiyo ya lazima na wana mpango wa kuongeza safari za ndani za Kilimanjaro na Mtwara, pia wamefanikiwa kuongeza mapato ya ndani yatokanayo na mizigo iliyozidi
Pia wanadhibiti utolewaji wa tiketi za bure unaotolewa kwa wafanyakazi wa shirika ambao unaonekana kutumiwa vibaya na wafanyakazi



Pia amesema wamejitahidi kutatua changamoto mbalimbali kama ucheweshaji wa ndege na wanaendelea kutatua changamoto ya uhaba wa marubani ambapo hadi sasa marubani wanne wamemaliza mafunzo na wengine wanne wanatarajia kumaliza mafunzo mwishoni mwa mwezi huu mafunzo hayo yanacchukua muda kwa kuwa yanategemea ndege mpya mbili tu.

Awamu ya mwisho ya ukamilishaji wa mafunzo inatarajiwa kumalizika mwezi Disemaba ambapo itaifanya ATCL kuwa na marubani 13.

======
Baada ya kuanza safari zake Octoba 14 2016,Shirika la Ndege la ATCL limekili kuwepo kwa changamoto mbalimbali zikiwemo ucheleweshaji wa ndege na kutoa huduma katika maeneo ambayo yalipaswa kuhudumiwa.

Akitoa changamoto hizo,Mwenyekiti wa Bodi ya Shirika hilo,Mhandisi Emmanuel Korosso amekili kuwepo kwa changamoto ya Marubani katika Shirika hilo ikizingatiwa mpaka sasa Shirika hilo linatarajiwa kumaliza mafunzo ya Marubani 13 katikati ya mwezi Desemba.

Amesema kuhusu Wafanyakazi Bodi yake imeagiza Menejimenti ya Shirika kusimamisha kwa muda mkataba wa hiari ambao unatoa mwanya kwa wafanyakazi kutumia vibaya ruhusa za matumizi ya tiketi za bure.

"Katokana na haja ya kuboresha Utendaji, ATCL iliamuliwa Wakurugenzi wote katika Menejimenti ya ATCL isipokuwa Mkurugenzi Mtendaji,na baadhi ya Menejimenti waondolewe katika nafasi zao Mara moja kutokana na Utendaji dhaifu na viwango vya Elimu visivyokidhi matakwa ya nafasi zao",amesema Mhandisi Korosso

"Tumeamua wakurugenzi wanaokaimu nafasi zao warudishwe katika nafasi zao za chini ambazo siyo za Menejimenti au wahamishiwe katika vituo vya mikoani",ameeleza Mhandisi Korosso

Aidha,Wakurugenzi na Menejimenti waliokuwa wamethibitishwa tumeagiza waondolewe ATCL ili wapangiwe majukumu mengine kulingana na sifa zao.

Aidha Bodi imemuagiza Mtendaji Mkuu kutangaza mara moja nafasi zote za Wakurugenzi na pia nafasi za Mameneja zilizo wazi kwa kufuata muundo wa muda uliopitishwa na Bodi (Interim Organization Structure).

Pia Mtendaji Mkuu ameagizwa kutangaza nafasi zozote ambazo anaona kuna umuhimu wa kuajiri watu wengine kutokana na utendaji usioridhisha wa wafanyakazi wanaoshikiria nafasi hizo kwa sasa.

Chanzo: Michuzi Jr
 
Mpaka tufike hii safari tutakuwa tumechoka mno
 
Yaan macho yote ya Serikali yapo ATCL kwa sasa, ndo maana wamemwaga TISS hapo Airport na Airport zingine ili kuchunguza mienendo ya ATCL, Daah! Afu kila mwezi waziri lazima aende ATCL, ndo ujue kuwa TISS kila siku lazima watoe taarifa, na kwa sasa hivi ndo watakaopachikwa kimya kimya kwenye baadhi ya nafasi za Kurugenzi hapo ATCL ili kufanya uchunguzi. Daah
 
Yaan macho yote ya Serikali yapo ATCL kwa sasa, ndo maana wamemwaga TISS hapo Airport na Airport zingine ili kuchunguza mienendo ya ATCL, Daah! Afu kila mwezi waziri lazima aende ATCL, ndo ujue kuwa TISS kila siku lazima watoe taarifa, na kwa sasa hivi ndo watakaopachikwa kimya kimya kwenye baadhi ya nafasi za Kurugenzi hapo ATCL ili kufanya uchunguzi. Daah
Haiepukiki. Roho ya Nchi hili shirika. TISS wapashughulikie kwelikweli hapo. Tumechoka kuona Rwanda Air, KQ, Ethiopian Airways, Emirates alhali nasi tuna uwezo na rasilimali zipo.
 
Naona matumaini ya ajira kwa mbali nayaona,ngoja na bodi nyingine za mashirika mengine yakururupuke kwenye menejiment zao kuhusu wafanyakazi mizigo
 
Yaan macho yote ya Serikali yapo ATCL kwa sasa, ndo maana wamemwaga TISS hapo Airport na Airport zingine ili kuchunguza mienendo ya ATCL, Daah! Afu kila mwezi waziri lazima aende ATCL, ndo ujue kuwa TISS kila siku lazima watoe taarifa, na kwa sasa hivi ndo watakaopachikwa kimya kimya kwenye baadhi ya nafasi za Kurugenzi hapo ATCL ili kufanya uchunguzi. Daah

ATCL will be a game changer ikisimawiwa vizuri ndiomana unaona Mh. Raisi na Waziri wake wameikomalia, kwa kweli kwa sasa shirika halitakiwi kushindwa kwasababu kila kitu wanacho, na wateja pia wapo kibao, tena ndani na nje ya nchi, kwa mfano nchi zinazo tumia bandari ya Dar es salaam (DRC, Zambia, Malawi, Burundi, Uganda na Central African Republic) zina wafanya biashara wengi wanaopenda kuwepo kwa usafiri wa ndege wa uhakika na wamoja kwa moja baina ya nchi zao na Dar es salaam kunakopatikana bandari.
 
Automata ninakuunga mkono kwenye hili badiko lako. Lakini ATCL wanatakiwa waangalie pia kwa sasa ni nini kinafanikisha biashara za ndege na kwa kiwango gani. Usikute hata hao wataobaki bado watakuwa mzigo kwa kufanya kazi kwa woga na kufuata akili za fulani baada ya kufata akili zao na ufahamu wa biashara kwa ujumla. Mi nashauri ATCL wafanye yafuatayo
1. Waajiri very very strong team kwa ajili ya marketing hata kama itakuwa ni wahindi ama wazungu.
2. Wajaribu kuangalia upya travel agencies na watengeneze Booking system ambayo itafuatilia kwa karibu kila itinery ticket inayouzwa.
3. Waweke mfumo mzuri wa mafuta. Mafuta ndio uhai wa ndege na bei hizi zinavyo fluctuate wasipoangalia suala la mafuta kwa ukaribu ipo siku watakwama, ikiwezekana wanunue angalau narudia tena, angalau lita laki tano in advance.
4. Waachane na watu kama skychafe waangalie ni kina nani watawapa tenda za inflight entertainments kwa bei nafuu au la watengeneze jiko lao wenyewe ambalo lita supply chakula kwenye ndege zao.
5. Waandae backup plan pindipo ndege inapata hitilafu carrier gani wanaweza kufanya nayo kazi ya kuhaulisha abiria na kwa mkataba gani. Sio leo ndege inapata hitilafu abiria mnawapeleka 5 star kulala, Ethiopia wametengeneza hotel yao wenyewe ya nyota 4 kwa mambo kama hayo.
6. Haraka sana watafute kampuni ya kutoa somo la customer care, iwe intensive course na lazima kila mfanyakazi ashiriki.
 
Sasa Bodi au menejimenti mpys wafanye maandaliza ya kuajiri wahudumu warembo,na wafundishwe lugha za kireno,kifaransa ili shirika liweze kuhudumia vyema wateja kutoka nchi za jirani(DRC-Lubumbashi na Kinshasa,Mozambique-Beira,naMaputo,Burundi-Bujumbura,Uganda-entebe,Comoro ,Zambia-lusaka,Zimbabwe-Harare)!
Kwa kuanzia,tuanze na nchi za karibu ili tupate uzoefu na kuongeza wateja!
Tusione shida kuajiri hata watumishi kutoka mashirika mengine,lakini kwa mkataba huku tukiwajengea uwezo watumishi wazawa.
 
Bodi ya ATCL Leo ikitoa mrejesho wa maamuzi yaliyofikiwa hivi karibuni imeamuru mtendaji mkuu kufukuza au kuwashusha vyeo wale wote ambao hawastaili katika nafasi walizopo!!

Bodi hiyo imedai kwamba Kuna wafanyakazi ambao wako katika nafasi ambazo hawastaili kitaaluma na kiuwezo

Ikumbukwe hivi karibuni Prof Makame Mbarawa alifanya ziara na kutoa tamko kali ambalo naona bodi imetekeleza


Tusubirie ATCL mpya!!






TBC 1
 
Back
Top Bottom