Bodaboda kukata leseni ya biashara.

Bodaboda kukata leseni ya biashara.

Joined
Sep 19, 2015
Posts
64
Reaction score
9
Bodaboda wilayani Muheza wanalalamikia kitendo cha kuambiwa wakate leseni za kubeba abiria hali inayo wafanya wengi wao wakitaka kurudisha pikipiki kwa wamiliki.Wachache wa bodaboda hao wamesema kwasiku unaweza usipate abiria hata mmoja na tunashinda juani halafu unadaiwa hesabu ya bosi halafu serikali inatukandamiza tuna omba msaada juu ya hili.
 
Tujibane tuweze kuchangia serikali ipate mapato.Gharama za uendeshaji wa serikali ni kubwa kama vile...mishahara...posho...mafuta ya magari...madawa..nk nk.Tujibane mwisho wa siku tutafika pazuri.
 
safi sana. walipe kodi stahiki za serikali.
 
Kushinda juani ndo madudu gani? Hizo barabara wanazopita wanafikiri zinajengwa na nn wasipochangia...
 
Bodaboda wilayani Muheza wanalalamikia kitendo cha kuambiwa wakate leseni za kubeba abiria hali inayo wafanya wengi wao wakitaka kurudisha pikipiki kwa wamiliki.Wachache wa bodaboda hao wamesema kwasiku unaweza usipate abiria hata mmoja na tunashinda juani halafu unadaiwa hesabu ya bosi halafu serikali inatukandamiza tuna omba msaada juu ya hili.
Nalifahamu kwa kiasi:
1. Sheri ya usafirishaji wa abiria ilifanyiwa marekebisho 2009 na bunge na kanuni zake kutungwa 2010.

2. Marekebisho hayo yalilenga kuruhusu pikipiki za magurudumu matatu (maarufu bajaji) na zile za magurudumu 2 maarufu bodaboda zitambulike kisheria kama vyombo vya kubeba abiria.

3. Sheria pamoja na kanuni hizo husimamiwa na SUMATRA, hata hivyo kwa bodaboda na bajaji mamlaka ya usimamizi na utoaji wa vibali (leseni za usafirishaji wa abiria) zimekasimishwa kwa Serikali za Mitaa (Halmashauri zote) baada ya kusain MoU kati ya SUMATRA na Halmashauri.

4. Tangu 2010, pikipiki zote nchini zinapaswa kutoa huduma hiyo zikiwa na leseni ambayo hutolewa kwa mwenye pikipiki baada ya; ukaguzi wa mkaguzi wa vyombo vya moto, kuwa na dereva aliyepata mafunzo na ana leseni, chombo hicho kina bima & co.........

5. Usimamizi wa sheria hii ulikuwa mdogo, kwa sasa unafatiliwa ipasavyo nchi nzima, na Halmashauri zinabanwa ipasavyo.

6. Ile namba iliyokuwa inaimbwa kipindi cha kampeni, kwa sasa imeekwa juu ya mlima Kilimanjaro, KILA MTU ANAISOMA KIVYAKE.
 
Wanacho sema boda boda serikari ikae na wenye piki piki sio kuwasumbua wao wao ni vibarua tu.
 
Huku Iringa kunaSUMTRA ya bodaboda 70elfu kwa mwaka sijui huko kwenu
 
Inashangaza kama Bodaboda serikali iliondoa kodi kwa Bodaboda. Ni vizuri Bajeti ijayo ipitishe kuwa Bodaboda nao waanze kulipia road license na kodi nyinginezo,hata kama ni elfu 10, serikali itapata kodi ya kutosha.

Vv
 
Inashangaza kama Bodaboda serikali iliondoa kodi kwa Bodaboda. Ni vizuri Bajeti ijayo ipitishe kuwa Bodaboda nao waanze kulipia road license na kodi nyinginezo,hata kama ni elfu 10, serikali itapata kodi ya kutosha.

Vv


Well said

Serikali isiishie kulalamika haina fedha huku kuna biashara zinafanyika bila kodi na wao serikali wapo wanaona wanasikia wanapanda hizo bodaboda na wanalipa nauli lakini hawaoni wala kusikia kuwa kuna asilimia yao pale waichukue ilete maendeleo.
 
Tujibane tuweze kuchangia serikali ipate mapato.Gharama za uendeshaji wa serikali ni kubwa kama vile...mishahara...posho...mafuta ya magari...madawa..nk nk.Tujibane mwisho wa siku tutafika pazuri.
Ili hayo mapato yakatembeze mwenge
 
Wanacho sema boda boda serikari ikae na wenye piki piki sio kuwasumbua wao wao ni vibarua tu.
Kuna kitu cha kukaa hapo?
Utekelezaji tu, dereva wa bodaboda kabla hajapokea pikipiki lazima ahakikishe haidaiwi na serikali kama ilivyo kwa madereva wa magari.
 
Bado kodi ya watembea kwa miguu angalau hata sh 15000 kwa mwaka ili kuiongezea mapato serikali yetu tukufu.tufike tunapo pataka.
 
Kama muuza nyanya sokoni kwa mafungu analipa ushuru ( kodi? ) wao bodaboda ni nani hadi wasilipe??!
 
Mmeshaambiwa ile namba imeweka juu ya mlima Kilimanjaro.. Ningeshangaa nyie mbona hamuisomi?
Tulieni tu kila mtu anaisoma. Vikizidi basi tutavaa mibomi tutaingia kitaa kama ile middle east rise. Hakuna namna manake tutaishije sasa
 
Wakirudisha kodi na wasiweke mipaka ya wapi wasiende wawe free
Serikali inahitaji fedha kwa ajili ya...
1. Mwenge ukimbizwe
2. Uteuzi wa viongozi mara kwa mara
3. Kulipa posho za askari wakizuia mikutano isipokuwa ya Lipumba.
4. Kulipa vyombo vya habari kurusha live matukio ya "mkemia wa barabara" isipokuwa bunge.
5. Kununua cash bombadia mapanga shaa..

6. Kuhakikisha namba inaendelea kuwepo pale kilele cha mlima Kilimanjaro ili kila mtu aisome
 
Mmeshaambiwa ile namba imeweka juu ya mlima Kilimanjaro.. Ningeshangaa nyie mbona hamuisomi?
Tulieni tu kila mtu anaisoma. Vikizidi basi tutavaa mibomi tutaingia kitaa kama ile middle east rise. Hakuna namna manake tutaishije sasa
Wanadhani ni ule muda wa mwakajana mwishoni kupanga foleni vituo vya mafuta kisha bendera za kijani unaendelea...
 
Back
Top Bottom